Pages

MAGAZETI YA UDAKU HATARINI KUFUNGIWA , NI KUTOKA BUNGENI

MAGAZETI YA UDAKU
MAGAZETI yanayochapisha picha zenye kukiuka maadili hususan za wanawake kwa kuwageuza malighafi ya kujiingizia kipato, yamemulikwa bungeni huku Serikali ikihojiwa sababu za kutoyachukulia hatua.
Mbunge wa Konde, Khatib Saidi Haji (CUF) alihoji hayo kwenye swali la nyongeza baada ya kujibiwa swali la msingi ambalo alitaka kufahamu ni aina gani ya makosa yanaweza kusababisha Serikali kuyafungia magazeti kama ilivyotokea kwa gazeti la Mwanahalisi.
Katika majibu ya msingi, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla alitaja sababu mbalimbali za kufungia magazeti hayo.
HabariLeo