
KAMPUNI ya Msama Promotions, imekamata watu watatu wakiwatuhumu kuuza kazi za wasanii kinyume na taratibu.
Akizungumza na Dira ya Mtanzania, Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama (pichani), alisema vijana hao walikamatwa katika eneo la Ubungo jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Dira ya Mtanzania, Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama (pichani), alisema vijana hao walikamatwa katika eneo la Ubungo jijini Dar es Salaam.
Waliokamatwa katika tuklio hilo
ni Malik Sultan, Ally Msangi, Edward Michael na Sijali Andrew ambao
walikuwa na CD feki 322 za wanamuziki mbalimbali na wasanii wengine.
Msama alisema zoezi la kukamata wezi wa kazi za wasanii linaendelea
kwa kufanya uchunguzi katika maeneo sugu ambako hatua inayofuata ni kwa
wale wanauza kazi hizo mikononi.
Aidha Msama analishukuru
Jeshi la Polisi kwa ushirikiano wanaoendelea kuutoa kwa timu ya vijana
wake wanaosaka wezi wa kazi za wasanii.
No comments:
Post a Comment