Mama mzazi wa mtoto huyo ambae Jina lake na la mtoto wake kwa sasa yamehifadhiwa na mtandao huu kutokana na sababu za kimaadili ,alisema kuwa wakati tukio hilo likitokea yeye alikuwa akiendelea na shughuli zake nyumbani na kusikia sauti ya mtoto wake akilia kwa uchungu kulalamika kubakwa .
Hata hivyo alisema baada ya kutoka nje na kuelekea eneo hilo ambalo sauti ilisikika alishuhudia kijana huyo akiendelea kumbaka mtoto wake jambo lilopelekea kupiga kelele kuomba msaada kwa wananchi ili kusaidia kumkamata mtuhumiwa huyo wa ubakaji.
Mwanamke huyo alisema kuwa jitihada za wananchi wa eneo hilo la Mwangata kumkamata mtuhumiwa ziliweza kufanikiwa pamoja na mtuhumiwa huyo kutaka kujaribu kukimbia eneo hilo.
Huyu ndie mtoto aliyebakwa na jemba hilo
Hivyo alisema kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo wa ubakaji kulepelekea wananchi wenye hasira kali kuanza kumwadhibu kwa kichapo na hata kutaka kumchoma moto kabla ya baadhi ya wananchi kutumia busura na kutaka afikishwe kituo cha polisi.
Mtuhumiwa huyo amefikishwa katika kituo kikuu cha polisi mjini Iringa huku akiwa hoi kwa kichapo na kupelekea kuvuja damu kupita kiasi kichwani kutokana na kichapo alichokipata kutoka kwa wananchi.