Amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama, Rais Jakaya Kikwete ametangaza operesheni kali ya kuwasaka majambazi wanaojihusisha na uhalifu ikiwemo utekaji wa magari na wahamiaji haramu itayoanza wiki mbili zijazo na ameagiza wahusika kuanza kujisalimisha wao na silaha wanazomiliki kinyume na utaratibu.