Snowden amepata nyaraka hizo muhimu kutoka kwa usaidizi wa Mwanasheria wake Anatoly Kucherena ambaye amekwenda katika Uwanja wa Ndega wa Sheremetyevo kukutana na mteja wake. Nyaraka hizo amekabidhiwa Kucherena ambaye ndiye atamkabidhi Snowden anayetajwa tayari ameshabadilishiwa hadi mavazi yake tayari kwa kuingia nchini Urusi na kuendelea na mchakato wa kuomba hifadhi ya kudumu. Mwanasheria wa Snowden, Kucherena amesema iwapo mteja wake atakuwa tayari kupatiwa uraia wa Urusi atafanya kila linalowezekana ili kuhakikisha anapata nafasi hiyo ambayo huenda ikatolewa kwake bila pingamizi.
Mapema mwezi huu Snowden alijitokeza na kuomba hifadhi nchini Urusi ambapo aliambiwa mchakato wa yeye kupewa hadhi huyo huenda ungechukua hata kipindi cha miezi mitatu kabla ya kukubaliwa. Mfanyakazi huyo wa zamani wa Shirika la Kijasusi la Nchini Marekani CIA Edward Snowden amekuwa akippata hifadhi ya muda nchini Urusi kitu ambacho kimechangia kuleta mgogoro wa uhusiano baina ya Serikali za Washington na Moscow.
Mapema mwezi huu Snowden alijitokeza na kuomba hifadhi nchini Urusi ambapo aliambiwa mchakato wa yeye kupewa hadhi huyo huenda ungechukua hata kipindi cha miezi mitatu kabla ya kukubaliwa. Mfanyakazi huyo wa zamani wa Shirika la Kijasusi la Nchini Marekani CIA Edward Snowden amekuwa akippata hifadhi ya muda nchini Urusi kitu ambacho kimechangia kuleta mgogoro wa uhusiano baina ya Serikali za Washington na Moscow.