
Kwa mujibu wa Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dk Paul Kisanga mtoto huyo alifariki dunia
wakati timu ya madaktari kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MOI) na Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar es Salaam wakijitahidi kila hali kuokoa maisha yake.
Kifo hicho kinaongeza idadi ya marehemu na kuwa wanne baada ya vifo vya Amiri Ally (7), Judith Moshi (25) ambaye ni Katibu wa Baraza la Wanawake Chadema (BAWACHA)Kata ya Sokoni One jijini Arusha na Ramadhan Juma (15).
Dk Kisanga alisema hospitali hiyo juzi ilipokea majeruhi wengine 17 wa mabomu ya kutoa machozi katika eneo la Soweto wakati polisi wakitawanya wafuasi wa Chadema.
Alisema majeruhi 14 wamelazwa huku watatu wakitibiwa na kuruhusiwa ambapo pia Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari aliyekuwa amelazwa hapo kutokana na kuumia shingoni aliruhusiwa na hali yake inaendelea vizuri.