Pages

"Kamati ya Nishati na Madini na POAC Zimevunjwa Ili Kuficha Ufisadi wa Bomba la Gesi" Zitto -Video

Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mh. Zitto Kabwe amesema vitendo anavyofanya Spika wa Bunge havikubaliki na anavifanya kwa makusudi ili kulinda ufisadi nchini. Zitto aliyasema hayo katika Viwanja vya Temeke alipokuwa akihutubia Wananchi katika Mkutano maalum wa kuwapokea Wabunge wa CHADEMA.