Taarifa zilizothibitishwa na mmoja wa ndugu za Marehemu, zinasema kuwa Marehemu Steven Kanumba alifariki majira ya saa nane usiku, muda mfupi baada ya kutokea mzozo kati yake yake na rafiki yake wa kike ambaye ni msanii mwenzake wa filamu.
Aliendelea na kuigiza filamu nyingi ambazo zilimpatia umaarufu mkubwa kiasi cha kusafiri mara kadhaa nchi za nje, ambako alitambulika kama mmoja wa wasanii wenye vipaji vikubwa ambaye aliitangaza fani ya filamu nchini Tanzania maarufu kama Bongo Movies.
Tangu kuanza kutangazwa kwa taarifa za kifo chake mapema alfajiri, mamia kwa maelfu ya watu wamekuwa wakimiminika kwa wingi nyumbani kwa marehemu, huku vyombo vingi vya habari vikizipa kipaumbele mara kwa mara taarifa za kifo cha msanii huyo.
No comments:
Post a Comment