Pages

How to Prepare For The Summer Fasts: Ramadan Kareem 2013 (Video)

Ratiba ya Ramadhani DMV

 Ratiba ya Ramadhani DMV

Ramadan Wishes from DarSlam Team

Ramadan Wishes

Ramadan Kareem

ZITTO KABWE AWATAKA WANANCHI WAGOME KUILIPA KODI YA SIMU YA SH. 1000 KWA SABABU ILIPITISHWA KINYEMELA

 kodi ya line ya simu
Sakata la kodi ya line ya simu limeendelea kuwakuna wanasiasa wetu ambao wamekuwa wakifunguka kwa nyakati mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii.
Baada ya January Makamba, Zitto Kabwe naye amefunguka na kudai kuwa kodi hiyo ni batili na ilipitishwa kinyemela kwa sababu ilikuwa imeshaondolewa....
Huu ni ujumbe wake aliouweka katika account yake ya facebook:
 kodi ya line ya simu
Baada ya kauli hiyo,Zitto Kabwe aliandamwa na maswali mengi sana toka kwa wananchi wakidai kuwa "Makamba alisema tuwalaumu ninyi maana ninyi wabunge ndo mlibariki kodi hii"
Zitto naye alishindwa kulijibu swali hilo na kuwataka wananchi "wachukue simu zao, wawapigie wabunge wao wawaulize ni kwa nini walipitisha kodi hii"
 January Makamba, Zitto kabwe
"Anasema hiyo kwa sababu wabunge ndio waliopitisha.Wabunge ndio wawakilishi wa wananchi.Jambo likipita bungeni hao ndio wa kwanza kulaumiwa.Yupo sahihi kabisa.Mpigie mbunge wako simu muulize kwa nini alikubali au hakupinga kodi hii"

Naibu Kadhi Mkuu, Sheikh Abubakar Zuber Aonya Imani za Kishirikina

Waislamu nchini wametakiwa kujiepusha na imani za kishirikina kwani kwa kufanya hivyo ni kuidhalilisha dini hiyo.
Wito huo umetolewa mwishoni mwa wiki na Naibu Kadhi Mkuu, Sheikh Abubakar Zuber katika Maulid ya Mtume (S.A.W) iliyoandaliwa na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi, Dk Najim Msenga mwishoni mwa wiki katika Halmashauri ya Bumbuli, wilayani Lushoto mkoani Tanga.

Sheikh Zubeir, ambaye pia ni Naibu Mufti wa Tanzania, alisema viongozi wa dini hiyo na mashehe kukubali kudhalilishwa na waganga wa kienyeji maarufu kwa jina la Lambalamba ni kufedhehesha uislamu na kuwataka waepuke vitendo hivyo ili kuutukuza Uislamu.

Eneo hilo la Bumbuli miezi miwili iliyopita lilikumbwa na wimbi la vurugu zilizosababishwa na kukamatwa kwa watu 32 kutokana uchochezi uliotokana na waganga hao wa Lambalamba.

Watu hao walikamatwa Aprili 21 mwaka huu Bumbuli na kusababisha wananchi kufanya vurugu iliyopelekea kuchomwa kwa kituo cha Polisi, ofisi ya Afisa Tarafa pamoja na ofisi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo .

Sheikh Zubeir aliiitaka Serikali kuchukua hatua kali dhidi ya watu kama hao ambao nia yao ni kufanya vitendo vya kuondoa kuaminiana miongoni mwa Watanzania .

Alisisitiza juu ya umuhimu wa kulinda amani iliyopo bila kubaguana kwa misingi ya dini wala rangi, ili kuendeleza umoja uliopo baina ya watanzania.

Alisema ili nchi iwe na amani, lazima vitendo viovu vidhibitiwe na kuitaka Serikali kupiga marufuku kabisa vitendo hivyo.

Alimtaka Mbunge wa Bumbuli, January Makamba kusaidia katika kudhibiti waganga hao haramu ili kulinda heshima ya Bumbuli.
‘‘Ndugu waumini wenzangu, kwa pamoja sote tuhakikishe tunailinda amani iliopo kwa gharama yoyote, kwani panapo amani kila kitu kinaweza kufanyika.’’

KINACHOWEZA KUWATOKEA AGNES NA MELISA -RIPOTI MPYA 'Raia wa kitanzania walio kamatwa na madawa'

Kabla ya kuingia mtandaoni niliweza kupata kuwasiliana na Raia mmoja anae ishi South Africa na aliweza kuniambia kinacho weza kuwatokea Raia wa kitanzania walio kamatwa na madawa ya kulevya nchini South Africa.......
chini picha za message alizokua akinitumia kijana huyo...jina tunalihifadhi......
AGNES , MELISA
AGNES MASONGANGE , MELISA
William Malecela
*Iwe Fundisho kwa wewe unaeisoma hii kama unampango na sembe jipange.
Na William Malecela

WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO na VYUO UFUNDI 2013/2014

Vodacom kufunga laini 450,000 kwa kutosajiliwa kisheria

Zaidi ya wateja 450,000 wa Kampuni ya Vodacom Tanzania huenda wakakosa fursa ya mawasiliano kutokana na kushindwa kufanya usajili wa kisheria wa namabari zao za simu na hivyo kuilazimu Vodacom
kuzifunga nambari hizo.
Uamuzi huo wa Vodacom umekuja baada ya kumalizika kwa kipindi cha usajili
wa nambari zote za simu za mkononi nchini Julai 10 mwaka huu.
Akizungumza ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa
Kampuni ya Vodacom Tanzania, Bw. Rene Meza, alisema kuwa ingawa sio jambo
linalofurahisha lakini kama kampuni ni lazima iheshimu na kuzingatia sheria
na kanuni za nchini na hivyo watazifungia nambari hizo.
“Sheria mpya ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (EPOCA) ya Mwaka
2010, imeainisha kifungu kinachoelekeza Makampuni ya Mawasiliano, namna
ambavyo wateja wake wanatakiwa kusajili namba zao za simu za mikonon
“Tulikuwa na muda wa kutosha kwa wateja wetu kutekeleza wajibu huo wa
kisheria huku tukitoa fursa na njia nyingi zaidi kuwawezesha kusajili
nambari hizo kwa urahisi na wepesi kutumia maduka yetu na pia mawakala wa
M-pesa nchi nzima na kwamba baada ya kumalizika kwa muda wa ukomo wa
kufanya hivyo hatuna budi kuitekeleza sheria kwa vitendo kwa kuzifungia
nambari zote ambazo hazijasajiliwa.”Alisema Meza.
Meza amesema hadi kufikia Julai 10, kampuni yake imebaini kuwa takribani
laini 450,000 hazijasajiliwa na ndizo ambazo zitakazofungwa.
“Tunapenda kuwashukuru wateja wetu kwa muitikio wao wa kujisajili na pia
kwa uvumilivu wao wakati wa utekelezaji wa utaratibu huu wa usajili wa
nambari za simu na uhakiki wa namba na taarifa za wateja ,”alisema.Meza
na kuongeza “Tumekuwa na mafanikio makubwa kutokana na idadi kubwa ya
wateja wetu kujitokeza kusajili nambari zao, hili ni jambo jema kwao na
kwetu sisi, na ni Imani yangu kwamba wale wote waliojisajili wataendelea
kufurahia huduma za mtandao wa Vodacom.”
Kuhakiki usajili wa nambari Mteja wa Vodacom anaweza kupiga *106 #.
Usajili wa namba za simu si chaguo mbali ni suala linaloendana na Sheria
mpya ya EPOCA, ambayo inaelekeza wateja wanaotumia namba za simu ambazo
hazijasajiliwa na ni kosa kwa mteja kutumoia nambari ambayo haijasajiliwa
huku akikabiliwa na adhabau ya ya Shilingi 500,000 au kifungo cha miezi
mitatu au vyote kwa pamoja.
Awali Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilitoa tarehe ya mwisho ya
kusitisha zoezi la usajili wa namba za simu za mikononi kuwa Juni 1, 2013
kabla ya kusogeza mbele hadi Julai 10, 2013 ili kuwapa fursa wateja ambao
hawajakamilisha usajili kufanya hivyo kuepuka kukatiwa mawasiliano.

Mhina Shabani.
Media Executive
0764 61 54 81

Wakandarasi Waagizwa Kuendelea na Ujenzi

Waziri wa ujenzi Dk. John Magufuli amewaagiza wakandarasi jijini Dar es Salaam waliositisha kuendelea na kazi kufuatia baadhi ya watu kufungua kesi mahakamani kuendelea na kazi ya kujenga barabara hata kama inapita mlangoni bila kubomoa nyumba zao hadi kesi itakapoisha huku akiwataka watu waliogoma kupisha mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni kuondoka haraka kabla hawajabomolewa.

MAN U WAANZA MAZOEZI LEO, CHINI YA KOCHA MPYA DAVIS MOYES

David Moyes
David Moyes ameanza zama mpya Manchester United kwa kuingia uwanjani kuungana na wachezaji kuwafundisha katika Uwanja wa mazoezi wa klabu, Carrington leo.
Kocha huyo mpya wa United aliungana na Msaidizi wake, Steve Round na alikuwa akifanya kazi yeye mwenyewe tofauti na kocha aliyemtangulia, Sir Alex Ferguson, ambaye alifurahia kuwaachia Mike Phelan na Rene Meulensteen kukochi timu.
Mchezaji anayetaka kuondoka, Wayne Rooney, mchezaji mpya, Wilfried Zaha na kocha mchezaji, Ryan Giggs walikuwa miongoni mwa walioshiriki mazozi hayo ya leo.
David Moyes

Zaha alilazimika kufanya vizuri ili kupambana na tetesi kwamba atatolewa kwa mkopo akakusanye uzoefu baada ya kusajiliwa kwa Pauni Milioni 15 kutoka Crystal Palace.

Na winga huyo kinda wa umri wa miaka 20 kwa kuonyesha kufurahia kuanza kazi United, ameposti picha akiwa na jezi ya mazoezi ya timu hiyo akitweet: "Siku kubwa ya kwanza #MUFC,".

David Moyes
Danny Welbeck na Rio Ferdinand
Danny Welbeck na Rio Ferdinand Wayne Rooney Wayne Rooney alikuwepo leo, ingawa alimaliza vibaya msimu uliopita kwa kutofautiana na Sir Alex Ferguson