Pages

Rapper 50 Cent has Removed His Son From His Will..!!

Rapper 50 Cent
 Marquise
Fiddy, as he is known by his fans, sent volatile text messages to his 16-year-old son Marquise in November last year, saying he planned to cut the boy and his mother off.

According to the Daily Mail, the texts came to light a day after the rapper was also shown to have sent abusive texts to his son in January this year, calling the kid a “s**t head”, “motherf***er” and “f***ing stupid”. In his January tirade, 50 Cent also demands a paternity test and tell his son to delete his number, saying “f*** you stop texting me”.

The rapper’s angry outburst allegedly stemmed from a poorly co-ordinated custody visitation. 50 Cent claims he went to see his son, but was left standing outside the house as no one answered the door. The rapper insisted that Marquise knew he was waiting outside and that he had spotted him peering at his father through the blinds.

“I don't have a son anymore,” tweeted the rapper after the incident.

This family feud, however, has been a long time in the making. In November, 2012, Fiddy wrote to his son: “If I died today would it matter to you? I’m changing my will. It’s a simple question.”

Marquise’s response highlighted the breakdown in the relationship between father and son.

“And this is coming from someone that didn't wish me a happy birthday.”

When Fiddy responded with his threat to remove Marquise and his mother from his will, the teenager replied: “I don't care about money, that's my last concern, of course we all like nice things but it's not everything.”
In his defence, 50 Cent claims that Marquise’s mother was the one texting back, and not his son.
 Marquise
Meanwhile, the rapper also has legal issues to deal with. He has been charged with one count of misdemeanour domestic violence and four counts of vandalism after he allegedly kicked a woman and destroyed $7000 worth of property at her condominium in Los Angeles last month.
According to Los Angeles City Attorney Frank Mateljan, 50 Cent kicked in a door and destroyed a piece of furniture, a chandelier and a television set.
“The altercation apparently started from an allegation of infidelity on her part,” Mateljan said.

The rapper faces a maximum penalty of five years in jail and $46 000 in fines if he is convicted.

How to Prepare For The Summer Fasts: Ramadan Kareem 2013 (Video)

Ratiba ya Ramadhani DMV

 Ratiba ya Ramadhani DMV

Ramadan Wishes from DarSlam Team

Ramadan Wishes

Ramadan Kareem

ZITTO KABWE AWATAKA WANANCHI WAGOME KUILIPA KODI YA SIMU YA SH. 1000 KWA SABABU ILIPITISHWA KINYEMELA

 kodi ya line ya simu
Sakata la kodi ya line ya simu limeendelea kuwakuna wanasiasa wetu ambao wamekuwa wakifunguka kwa nyakati mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii.
Baada ya January Makamba, Zitto Kabwe naye amefunguka na kudai kuwa kodi hiyo ni batili na ilipitishwa kinyemela kwa sababu ilikuwa imeshaondolewa....
Huu ni ujumbe wake aliouweka katika account yake ya facebook:
 kodi ya line ya simu
Baada ya kauli hiyo,Zitto Kabwe aliandamwa na maswali mengi sana toka kwa wananchi wakidai kuwa "Makamba alisema tuwalaumu ninyi maana ninyi wabunge ndo mlibariki kodi hii"
Zitto naye alishindwa kulijibu swali hilo na kuwataka wananchi "wachukue simu zao, wawapigie wabunge wao wawaulize ni kwa nini walipitisha kodi hii"
 January Makamba, Zitto kabwe
"Anasema hiyo kwa sababu wabunge ndio waliopitisha.Wabunge ndio wawakilishi wa wananchi.Jambo likipita bungeni hao ndio wa kwanza kulaumiwa.Yupo sahihi kabisa.Mpigie mbunge wako simu muulize kwa nini alikubali au hakupinga kodi hii"

Naibu Kadhi Mkuu, Sheikh Abubakar Zuber Aonya Imani za Kishirikina

Waislamu nchini wametakiwa kujiepusha na imani za kishirikina kwani kwa kufanya hivyo ni kuidhalilisha dini hiyo.
Wito huo umetolewa mwishoni mwa wiki na Naibu Kadhi Mkuu, Sheikh Abubakar Zuber katika Maulid ya Mtume (S.A.W) iliyoandaliwa na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi, Dk Najim Msenga mwishoni mwa wiki katika Halmashauri ya Bumbuli, wilayani Lushoto mkoani Tanga.

Sheikh Zubeir, ambaye pia ni Naibu Mufti wa Tanzania, alisema viongozi wa dini hiyo na mashehe kukubali kudhalilishwa na waganga wa kienyeji maarufu kwa jina la Lambalamba ni kufedhehesha uislamu na kuwataka waepuke vitendo hivyo ili kuutukuza Uislamu.

Eneo hilo la Bumbuli miezi miwili iliyopita lilikumbwa na wimbi la vurugu zilizosababishwa na kukamatwa kwa watu 32 kutokana uchochezi uliotokana na waganga hao wa Lambalamba.

Watu hao walikamatwa Aprili 21 mwaka huu Bumbuli na kusababisha wananchi kufanya vurugu iliyopelekea kuchomwa kwa kituo cha Polisi, ofisi ya Afisa Tarafa pamoja na ofisi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo .

Sheikh Zubeir aliiitaka Serikali kuchukua hatua kali dhidi ya watu kama hao ambao nia yao ni kufanya vitendo vya kuondoa kuaminiana miongoni mwa Watanzania .

Alisisitiza juu ya umuhimu wa kulinda amani iliyopo bila kubaguana kwa misingi ya dini wala rangi, ili kuendeleza umoja uliopo baina ya watanzania.

Alisema ili nchi iwe na amani, lazima vitendo viovu vidhibitiwe na kuitaka Serikali kupiga marufuku kabisa vitendo hivyo.

Alimtaka Mbunge wa Bumbuli, January Makamba kusaidia katika kudhibiti waganga hao haramu ili kulinda heshima ya Bumbuli.
‘‘Ndugu waumini wenzangu, kwa pamoja sote tuhakikishe tunailinda amani iliopo kwa gharama yoyote, kwani panapo amani kila kitu kinaweza kufanyika.’’

KINACHOWEZA KUWATOKEA AGNES NA MELISA -RIPOTI MPYA 'Raia wa kitanzania walio kamatwa na madawa'

Kabla ya kuingia mtandaoni niliweza kupata kuwasiliana na Raia mmoja anae ishi South Africa na aliweza kuniambia kinacho weza kuwatokea Raia wa kitanzania walio kamatwa na madawa ya kulevya nchini South Africa.......
chini picha za message alizokua akinitumia kijana huyo...jina tunalihifadhi......
AGNES , MELISA
AGNES MASONGANGE , MELISA
William Malecela
*Iwe Fundisho kwa wewe unaeisoma hii kama unampango na sembe jipange.
Na William Malecela

WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO na VYUO UFUNDI 2013/2014

Vodacom kufunga laini 450,000 kwa kutosajiliwa kisheria

Zaidi ya wateja 450,000 wa Kampuni ya Vodacom Tanzania huenda wakakosa fursa ya mawasiliano kutokana na kushindwa kufanya usajili wa kisheria wa namabari zao za simu na hivyo kuilazimu Vodacom
kuzifunga nambari hizo.
Uamuzi huo wa Vodacom umekuja baada ya kumalizika kwa kipindi cha usajili
wa nambari zote za simu za mkononi nchini Julai 10 mwaka huu.
Akizungumza ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa
Kampuni ya Vodacom Tanzania, Bw. Rene Meza, alisema kuwa ingawa sio jambo
linalofurahisha lakini kama kampuni ni lazima iheshimu na kuzingatia sheria
na kanuni za nchini na hivyo watazifungia nambari hizo.
“Sheria mpya ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (EPOCA) ya Mwaka
2010, imeainisha kifungu kinachoelekeza Makampuni ya Mawasiliano, namna
ambavyo wateja wake wanatakiwa kusajili namba zao za simu za mikonon
“Tulikuwa na muda wa kutosha kwa wateja wetu kutekeleza wajibu huo wa
kisheria huku tukitoa fursa na njia nyingi zaidi kuwawezesha kusajili
nambari hizo kwa urahisi na wepesi kutumia maduka yetu na pia mawakala wa
M-pesa nchi nzima na kwamba baada ya kumalizika kwa muda wa ukomo wa
kufanya hivyo hatuna budi kuitekeleza sheria kwa vitendo kwa kuzifungia
nambari zote ambazo hazijasajiliwa.”Alisema Meza.
Meza amesema hadi kufikia Julai 10, kampuni yake imebaini kuwa takribani
laini 450,000 hazijasajiliwa na ndizo ambazo zitakazofungwa.
“Tunapenda kuwashukuru wateja wetu kwa muitikio wao wa kujisajili na pia
kwa uvumilivu wao wakati wa utekelezaji wa utaratibu huu wa usajili wa
nambari za simu na uhakiki wa namba na taarifa za wateja ,”alisema.Meza
na kuongeza “Tumekuwa na mafanikio makubwa kutokana na idadi kubwa ya
wateja wetu kujitokeza kusajili nambari zao, hili ni jambo jema kwao na
kwetu sisi, na ni Imani yangu kwamba wale wote waliojisajili wataendelea
kufurahia huduma za mtandao wa Vodacom.”
Kuhakiki usajili wa nambari Mteja wa Vodacom anaweza kupiga *106 #.
Usajili wa namba za simu si chaguo mbali ni suala linaloendana na Sheria
mpya ya EPOCA, ambayo inaelekeza wateja wanaotumia namba za simu ambazo
hazijasajiliwa na ni kosa kwa mteja kutumoia nambari ambayo haijasajiliwa
huku akikabiliwa na adhabau ya ya Shilingi 500,000 au kifungo cha miezi
mitatu au vyote kwa pamoja.
Awali Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilitoa tarehe ya mwisho ya
kusitisha zoezi la usajili wa namba za simu za mikononi kuwa Juni 1, 2013
kabla ya kusogeza mbele hadi Julai 10, 2013 ili kuwapa fursa wateja ambao
hawajakamilisha usajili kufanya hivyo kuepuka kukatiwa mawasiliano.

Mhina Shabani.
Media Executive
0764 61 54 81