Pages

Naibu Kadhi Mkuu, Sheikh Abubakar Zuber Aonya Imani za Kishirikina

Waislamu nchini wametakiwa kujiepusha na imani za kishirikina kwani kwa kufanya hivyo ni kuidhalilisha dini hiyo.
Wito huo umetolewa mwishoni mwa wiki na Naibu Kadhi Mkuu, Sheikh Abubakar Zuber katika Maulid ya Mtume (S.A.W) iliyoandaliwa na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi, Dk Najim Msenga mwishoni mwa wiki katika Halmashauri ya Bumbuli, wilayani Lushoto mkoani Tanga.

Sheikh Zubeir, ambaye pia ni Naibu Mufti wa Tanzania, alisema viongozi wa dini hiyo na mashehe kukubali kudhalilishwa na waganga wa kienyeji maarufu kwa jina la Lambalamba ni kufedhehesha uislamu na kuwataka waepuke vitendo hivyo ili kuutukuza Uislamu.

Eneo hilo la Bumbuli miezi miwili iliyopita lilikumbwa na wimbi la vurugu zilizosababishwa na kukamatwa kwa watu 32 kutokana uchochezi uliotokana na waganga hao wa Lambalamba.

Watu hao walikamatwa Aprili 21 mwaka huu Bumbuli na kusababisha wananchi kufanya vurugu iliyopelekea kuchomwa kwa kituo cha Polisi, ofisi ya Afisa Tarafa pamoja na ofisi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo .

Sheikh Zubeir aliiitaka Serikali kuchukua hatua kali dhidi ya watu kama hao ambao nia yao ni kufanya vitendo vya kuondoa kuaminiana miongoni mwa Watanzania .

Alisisitiza juu ya umuhimu wa kulinda amani iliyopo bila kubaguana kwa misingi ya dini wala rangi, ili kuendeleza umoja uliopo baina ya watanzania.

Alisema ili nchi iwe na amani, lazima vitendo viovu vidhibitiwe na kuitaka Serikali kupiga marufuku kabisa vitendo hivyo.

Alimtaka Mbunge wa Bumbuli, January Makamba kusaidia katika kudhibiti waganga hao haramu ili kulinda heshima ya Bumbuli.
‘‘Ndugu waumini wenzangu, kwa pamoja sote tuhakikishe tunailinda amani iliopo kwa gharama yoyote, kwani panapo amani kila kitu kinaweza kufanyika.’’

KINACHOWEZA KUWATOKEA AGNES NA MELISA -RIPOTI MPYA 'Raia wa kitanzania walio kamatwa na madawa'

Kabla ya kuingia mtandaoni niliweza kupata kuwasiliana na Raia mmoja anae ishi South Africa na aliweza kuniambia kinacho weza kuwatokea Raia wa kitanzania walio kamatwa na madawa ya kulevya nchini South Africa.......
chini picha za message alizokua akinitumia kijana huyo...jina tunalihifadhi......
AGNES , MELISA
AGNES MASONGANGE , MELISA
William Malecela
*Iwe Fundisho kwa wewe unaeisoma hii kama unampango na sembe jipange.
Na William Malecela

WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO na VYUO UFUNDI 2013/2014

Vodacom kufunga laini 450,000 kwa kutosajiliwa kisheria

Zaidi ya wateja 450,000 wa Kampuni ya Vodacom Tanzania huenda wakakosa fursa ya mawasiliano kutokana na kushindwa kufanya usajili wa kisheria wa namabari zao za simu na hivyo kuilazimu Vodacom
kuzifunga nambari hizo.
Uamuzi huo wa Vodacom umekuja baada ya kumalizika kwa kipindi cha usajili
wa nambari zote za simu za mkononi nchini Julai 10 mwaka huu.
Akizungumza ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa
Kampuni ya Vodacom Tanzania, Bw. Rene Meza, alisema kuwa ingawa sio jambo
linalofurahisha lakini kama kampuni ni lazima iheshimu na kuzingatia sheria
na kanuni za nchini na hivyo watazifungia nambari hizo.
“Sheria mpya ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (EPOCA) ya Mwaka
2010, imeainisha kifungu kinachoelekeza Makampuni ya Mawasiliano, namna
ambavyo wateja wake wanatakiwa kusajili namba zao za simu za mikonon
“Tulikuwa na muda wa kutosha kwa wateja wetu kutekeleza wajibu huo wa
kisheria huku tukitoa fursa na njia nyingi zaidi kuwawezesha kusajili
nambari hizo kwa urahisi na wepesi kutumia maduka yetu na pia mawakala wa
M-pesa nchi nzima na kwamba baada ya kumalizika kwa muda wa ukomo wa
kufanya hivyo hatuna budi kuitekeleza sheria kwa vitendo kwa kuzifungia
nambari zote ambazo hazijasajiliwa.”Alisema Meza.
Meza amesema hadi kufikia Julai 10, kampuni yake imebaini kuwa takribani
laini 450,000 hazijasajiliwa na ndizo ambazo zitakazofungwa.
“Tunapenda kuwashukuru wateja wetu kwa muitikio wao wa kujisajili na pia
kwa uvumilivu wao wakati wa utekelezaji wa utaratibu huu wa usajili wa
nambari za simu na uhakiki wa namba na taarifa za wateja ,”alisema.Meza
na kuongeza “Tumekuwa na mafanikio makubwa kutokana na idadi kubwa ya
wateja wetu kujitokeza kusajili nambari zao, hili ni jambo jema kwao na
kwetu sisi, na ni Imani yangu kwamba wale wote waliojisajili wataendelea
kufurahia huduma za mtandao wa Vodacom.”
Kuhakiki usajili wa nambari Mteja wa Vodacom anaweza kupiga *106 #.
Usajili wa namba za simu si chaguo mbali ni suala linaloendana na Sheria
mpya ya EPOCA, ambayo inaelekeza wateja wanaotumia namba za simu ambazo
hazijasajiliwa na ni kosa kwa mteja kutumoia nambari ambayo haijasajiliwa
huku akikabiliwa na adhabau ya ya Shilingi 500,000 au kifungo cha miezi
mitatu au vyote kwa pamoja.
Awali Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilitoa tarehe ya mwisho ya
kusitisha zoezi la usajili wa namba za simu za mikononi kuwa Juni 1, 2013
kabla ya kusogeza mbele hadi Julai 10, 2013 ili kuwapa fursa wateja ambao
hawajakamilisha usajili kufanya hivyo kuepuka kukatiwa mawasiliano.

Mhina Shabani.
Media Executive
0764 61 54 81

Wakandarasi Waagizwa Kuendelea na Ujenzi

Waziri wa ujenzi Dk. John Magufuli amewaagiza wakandarasi jijini Dar es Salaam waliositisha kuendelea na kazi kufuatia baadhi ya watu kufungua kesi mahakamani kuendelea na kazi ya kujenga barabara hata kama inapita mlangoni bila kubomoa nyumba zao hadi kesi itakapoisha huku akiwataka watu waliogoma kupisha mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni kuondoka haraka kabla hawajabomolewa.

MAN U WAANZA MAZOEZI LEO, CHINI YA KOCHA MPYA DAVIS MOYES

David Moyes
David Moyes ameanza zama mpya Manchester United kwa kuingia uwanjani kuungana na wachezaji kuwafundisha katika Uwanja wa mazoezi wa klabu, Carrington leo.
Kocha huyo mpya wa United aliungana na Msaidizi wake, Steve Round na alikuwa akifanya kazi yeye mwenyewe tofauti na kocha aliyemtangulia, Sir Alex Ferguson, ambaye alifurahia kuwaachia Mike Phelan na Rene Meulensteen kukochi timu.
Mchezaji anayetaka kuondoka, Wayne Rooney, mchezaji mpya, Wilfried Zaha na kocha mchezaji, Ryan Giggs walikuwa miongoni mwa walioshiriki mazozi hayo ya leo.
David Moyes

Zaha alilazimika kufanya vizuri ili kupambana na tetesi kwamba atatolewa kwa mkopo akakusanye uzoefu baada ya kusajiliwa kwa Pauni Milioni 15 kutoka Crystal Palace.

Na winga huyo kinda wa umri wa miaka 20 kwa kuonyesha kufurahia kuanza kazi United, ameposti picha akiwa na jezi ya mazoezi ya timu hiyo akitweet: "Siku kubwa ya kwanza #MUFC,".

David Moyes
Danny Welbeck na Rio Ferdinand
Danny Welbeck na Rio Ferdinand Wayne Rooney Wayne Rooney alikuwepo leo, ingawa alimaliza vibaya msimu uliopita kwa kutofautiana na Sir Alex Ferguson

MKOLONI,JUMA NATURE na MAPACHA -BILA SABABU (Audio)


NYATI MWEUPE NGORONGORO kw MARA ya KWANZA

NYATI MWEUPE
WAHIFADHI watafiti na wataalamu kadhaa, wako katika harakati za kumsaka Nyati wa ajabu anayedaiwa kuwa na rangi ya maziwa, ambaye hivi karibuni ameonekana katika mwambao wa bonde kuu la Ngorongoro (Kreta) na kusababisha tafrani kubwa.
Kwa mujibu wa mtalaam wa ikolojia katika mamlaka hiyo, Patrice Mattay, uwepo wa nyati (mbogo) huyo wa aina yake hifadhini hapo, kumeibua suala jipya katika utafiti wa wanyama pori, kwani hakujawahi kuwepo Nyati mwenye rangi nyeupe popote duniani. Kwa kawaida Nyati huwa anangozi yenye rangi nyeusi.
Nyati huyo mweupe aligundulika kwa mara ya kwanza na maafisa wa polisi wanaofanya kazi katika kituo cha polisi kilichopo ndani ya hifadhi hiyo, ambao wanasema mnyama huyo hupita katika maeneo ya kituo hicho majira ya asubuhi akiwa miongoni mwa mbogo wengine takribani 20. Ngorongoro ina nyati wapatao 350.

“Ni kweli hata mimi binafsi nimemshuhudia Nyati huyo mweupe akikatiza katika sehemu mbalimbali za hifadhi ya Ngorongoro majira ya asubuhi akiwa katika kundi la mbogo wengine,” alisema mkuu wa kituo cha Ngorongoro Afisa wa Polisi, JJ Paul.

Hadi sasa ni maaskari wanaofanya doria katika maeneo ya hifadhi hiyo, hususan nyakati za asubuhi, ndio wanaothibitisha kwa kiwango kikubwa kumuona Nyati huyo wa ajabu ambaye sasa anatarajiwa kuwa atakuwa kivutio kipya cha utalii nchini.

Meneja Uhifadhi katika mamlaka ya Ngorongoro, Amiyo T. Amiyo amesema tayari shirika lake limekwisha tuma askari wake kadhaa kumsaka Nyati huyo wa ajabu, ili kubaini eneo ambalo anapatikana kwa ajili ya kuwezesha utafiti zaidi.

“Na kwa mtu yeyote mwenye kutuletea taarifa kuhusu Nyati huyo mweupe zitakazotuwezesha kumpata mnyama huyo, basi naye pia atazawadiwa ipasavyo,” alisema Amiyo.

Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro ndiyo inayoongoza kwa kupata watalii wengi nchini na kwa mujibu wa Ofisa Utalii wa Shirika hilo, Asantaeli Melita, zaidi ya wageni 585,000 hutembelea eneo hilo, na hasa Kreta, kila mwaka.

Idadi ya wanyamapori walioko Ngorongoro kwa sasa inafikia 300,000 wengi wao wakiwa ndani ya bonde lenyewe huku baadhi na hasa twiga wakiishi nje ya Kreta.

Mbali na Mbogo wa jabu aliyegunduliwa hivi karibuni, eneo la Ngorongoro pia lina maajabu mengine kadhaa, ukiwemo kilima cha mchanga unaotembea bila kusambaratika, idadi kubwa ya Kakakuona, mnyama anayedaiwa kuwa na uwezo wa kutabiri, pamoja na idadi kubwa ya wanyama adimu kama Mbwa-mwitu na Faru.

Blog Zote za Tanzania Sasa Zinapatikana Ndani ya Blog Moja (Directory)

Tanzania DirectoryAcha kuzunguka blog kibao bila kupata habari uliyokua unaitafuta,
Blog ni moja tu Bongo Blogs ndio unatakiwa kukumbuka halafu nyinginezo zooote utazipata ndani yake (Bongo Blogs) bofya link..
 >> Bongo Blogs
 http://bongoblogs.blogspot.com
Blog yako ya Taifa

Iran to Assign e-mail Addresses to All Citizens.

Iran
Iran will give its citizens individual email addresses in a move to aid interaction between state authorities and the people.
It is unclear whether the initiative will add to regulations on internet use imposed by Iran’s conservative Islamist leadership, which is wary of secular cultural influences it blames on the West.

President-elect Hassan Rouhani, a relative moderate who takes office next month, has called for less state intervention in people’s private lives, including less filtering of the internet and a loosening of press regulation.

Official figures show that more than half of the Islamic republic’s 75 million people use the internet.
But authorities have tried to limit access with tools including a filter that blocks many websites on the grounds they are offensive or criminal.

In March, authorities blocked software used to get around the filter.
Many people said they experienced slower internet speeds ahead of the June 14 election in Iran, which critics saw as an apparent attempt to make it harder to organize pro-reform candidate rallies via social media.

Communications minister Mohammad Hassan Nami did not say whether the national email addresses would be mandatory or how they might affect Iranians’ use of their own private addresses.

But he said the official addresses must be used for electronic communication with government agencies.