
RAIA WAVAMIA NA VIKOMBE NA VIBAKULI GARI LA MAZIWA BAADA YA GARI HILO KUPATA AJALI!

Bila kujali usalama wa afya zao, wakazi wa jiji la Dar es salaam wakikinga maziwa kwenye kontena la kampuni ya maziwa ya Tanga Fresh baada ya kichwa cha kontena hilo
kuchomoka na kuacha njia eneo la ubungo mataa leo Julai 24, 2013.likitokea Mkoani Tanga hakuna aliyejeruhiwa kwenye ajali
hiyo.




Kichwa chenye namba za usajili T 787 AFX kinachobeba kontena la maziwa kikiwa pembeni mwa barabara mara baada ya kuacha njia. Lori hilo lilitokea mkoaniTanga na tayari lilishafika Dares salaam kabla ya balaa kulisibu.
Fullshangwe.
Lewis Hamilton Missed his Mercedes More than Ex-Missus
LEWIS HAMILTON admits he missed his Mercedes’ motor more than his ex-missus ahead of this weekend’s Hungarian Grand Prix.
SunSport told you how the F1 ace was heading to the recording studio to cure his blues following his split from singer and TV presenter Nicole Scherzinger.
Hamilton, 28, spent last week in LA recording tracks but insisted his crooning was not meant as an attempt to win back The Pussycat Dolls’ star.
He said: “I was not writing love songs, as some people have been suggesting, to win anyone back. It is just something I enjoy doing and something that I am actually really good at.
“The break after the German Grand Prix was too long. I just really missed being in the car. I have been really excited about getting back in the car.
“I had time to really think about how well the season has gone for me. Everyone was talking me down at the beginning of the year.
“So many things said about whether it was right or wrong decisions, whether it was a silly mistake, but the team and I have constantly proved everyone wrong, race after race. “We are second in the constructors’ championship and I feel privileged and grateful that I have been able to contribute to that.
“I would never have thought we would have been in such a competitive position -- still within shooting distance of both championships.”
After his week in the States, Hamilton jetted to the party island of Ibiza but did not hit the all-night disco bars.
Instead he spent the day on former F1 driver Gerhard Berger’s luxury yacht with Mercedes’ non-executive chairman, Niki Lauda.
And Hamilton, who was once accused of being “dangerous” by Lauda, says he has an excellent relationship with the outspoken Austrian.
He added: “It was just a general meeting. Niki is always asking me how he can help. He asks me about the weaknesses in the team and where it can be improved on.
“You definitely would not have thought that I would have a good relationship with Niki 12 months ago. “I have always respected him, but perhaps even more now that I have spent time with him and I see the type of character he is.
“He has been spending time with me, so he can see who I am too and has perhaps created a new opinion about me.”
Hamilton is looking for victory number four here at the Hungaroring but admits he is unsure how his Mercedes will perform on the new Pirelli tyres.
He said: “I always seem to be quite strong here and the car is better this year, so I should be in a good position. “You have to be aggressive on this track and I am more aggressive than most so it tends to suit me more.
“But with the new tyres it is going to be difficult to know where we are going to be and they are going to be dominating this weekend.”
By BEN HUNT
RAISI KIKWETE: ATAKAYE JARIBU KUICHOKOZA AU KUIVAMIA NCHI YETU ATAKIONA CHA MTEMA KUNI...!
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka ngao/sime katika mnara wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya Mashujaa katika kambi ya jeshi ya Kaboya, Bukoba, mkoani Kagera leo Julai 25, 2013
Maadhimisho haya yalihudhuriwa na viongozi wakuu wa nchi akiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt Mohamed Ali Shein, Makamu wa Rais, Dkt Mohamed Gharib Bilali, Jaji Mkuu Mheshimiwa, Chande Othman na Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Othman Makungu.
Zifuatazo ni picha na taarifa ya IKULU kuhusu maadhimisho hayo.
Maadhimisho haya yalihudhuriwa na viongozi wakuu wa nchi akiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt Mohamed Ali Shein, Makamu wa Rais, Dkt Mohamed Gharib Bilali, Jaji Mkuu Mheshimiwa, Chande Othman na Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Othman Makungu.
Zifuatazo ni picha na taarifa ya IKULU kuhusu maadhimisho hayo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa yeyote ambaye atajaribu kuchezea usalama na mipaka ya Tanzania atakiona cha mtema kuni.
Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) liko imara tayari kulinda mipaka ya Tanzania wakati wowote na saa yoyote.
Rais Kikwete ametoa ujumbe huo mzito leo, Alhamisi, Julai 25, 2013, wakati alipozungumza na wananchi wakati Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa kwenye Kambi la JWTZ ya Kaboya, Wilaya ya Muleba, Mkoa wa Kagera.
Mara baada ya kushuhudia sherehe za kumbukumbu hizo ambako miongoni mwa mambo mengine
ametembelea makaburi ya askari wa Tanzania waliopoteza maisha yao wakati wa kuikomboa nchi kutokana na uvamizi wa Idi Amin wa Uganda na kuona silaha zilizotumika katika vita hivyo vya 1978/79, Rais Kikwete amewaambia mamia kwa mamia ya wananchi waliohudhuria sherehe hizo:
“Laleni usingizi salama. Msisikilize maneno ya mitaani kwa sababu Jeshi letu liko imara kabisa kulinda nchi yetu na mipaka yake. Yeyote atakayejaribu kuivamia ama kuichokoza nchi yetu atakiona cha mtema kuni. Nchi iko salama na Jeshi liko imara kulinda nchi yetu,” amesema Rais Kikwete na kuongeza:
“Ujumbe wetu mkubwa wa leo ni kwamba tuko tayari wakati wote na, saa yeyote kuilinda nchi yetu na mipaka yake. Hatuna nchi nyingine. Hivyo, kamwe hatuwezi kumruhusu yeyote kuicheza nchi yetu, ama kuichezea ama kuimega nchi hii. Kama tulivyoshughulika na Amin naye tutashughulika naye vivyo hivyo.”
Rais Kikwete amesema kuwa shughuli ya kulinda amani ni ghali mno: “Na moja ya gharama hizo ni makaburi haya ya ndugu zetu ambao wamelala hapa baada ya kupoteza maisha yao katika vita dhidi ya Nduli Idi Amin. Tutaendelea kuwaenzi kwa sababu hawa walijitolea maisha yao kulinda mipaka ya nchi yetu, kulinda amani ya nchi yetu na usalama wake na wetu sote.”
Kiasi cha askari 619 waliopoteza maisha yao wamelazwa kwenye makaburi hayo ya Kaboya.
Rais Kikwete amesema kuwa Serikali yake kwa ushauri wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania inaangalia jinsi gani ya kuwahudumia vizuri zaidi askari wa Tanzania ambao walipata vilema katika vita hivyo na bado wanaendelea kuishi.
“Nimesikia kuna malalamiko lalamiko kuhusu ubora wa jinsi tunavyowahudumia na hivyo tutazungumza na Jeshi kuhusu njia bora zaidi ya jinsi ya kuwahudumia. Hawa ni mashujaa wetu, ni watu waliojitolea maisha yao kuweza kulinda uhuru wetu. Tunaendelea kuwashukuru na kuwaenzi. Hii ndiyo sababu sherehe za leo ni sherehe kubwa kwa nchi yetu.”
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
25 Julai, 2013
Watu Zaidi ya 75 Wamekufa Nchini Hispania Kufuatia Ajali Mbaya ya Treni Kuacha Njia na Kupinduka.
Watu takriban 77 wamekufa na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa kati ya abiria 218 baada ya treni moja ya abiri kuacha njia na kuanguka kaskazini magharibi mwa Hispania.
Mabehewa yote 8 ya treni hiyo iliyokuwa ikitoka Madrid kuelekea Ferrol yameanguka karibu na mji wa Santiago de Compostela.
Taarifa za vyombo vya habari zinasema huenda treni hiyo ilikuwa ikienda kwa mwendo kasi wa mara mbili ya kipimo chake katika eneo lenye kona.
Maafisa mjini humo hawajasema lolote kuhusiana na chanzo cha ajali hiyo huku wachambuzi wa mambo wakisema ni ajali mbaya zaidi ya treni kutokea nchini Hispania katika kipindi cha miaka 40.
Ajali kubwa ya treni kuwahi kutokea nchini humo ilikuwa mwaka 1972 wakati watu 77 walipokufa baada ya treni kuacha njia huko Andalusia eneo la kusini.
JEURI YA HELA HII CHRIS BROWN ALICHORA GARI LAKE LIFANANE NA KIATU CHAKE
Gari jipya la kifahari la Chris Brown aina ya Lamborghini Aventador baada ya kupigwa rangi lifanane na raba zake.
Raba alizonunua hivi karibuni aina ya Nike Air Foamposites.
Gari hilo la kifahari lilivyokuwa wakati akilinunua.
Ni Msimu wa NaneNane..!!
Kwako wewe ulio na matangazo ya aina yoyote na ukubwa wa saiz yoyote ikiwa ni
pamoja kama unakodisha au unauza Shamba, Nyumba, Gari, Duka, Saluni,
Ofisi,Kiwanda, Kampuni na Kadhalika.
Pia ni fursa kwako kua Sponsor wetu
kwa matangazo ya muda mrefu.
Kumbuka mtandao wetu ni maarufu
unatembelewa na watu wote ulimwenguni kutokana na mfumo wetu wa
usambazaji wa habari ktk tovuti zetu nyingine pia mitandao ya kijamii.
..Hii ni nafasi yako. Wahi sasa..!! Bei ni nafuu sana.
Kwa maelewano
usisite kutuandikia Barua pepe kupitia darslam@rocketmail.com
Pia tunapokea habari mbalimbali buree.
Bila kusahau Blog yako ya Taifa ..Bongo Blogs - Blog za Bongo
Bila kusahau Blog yako ya Taifa ..Bongo Blogs - Blog za Bongo
Inakupa fursa husika.
Kazi ni kwako...!
Kutoka South Africa, Mmiliki wa Home Shopping Center Akipata Matibabu Baada ya Kumwagiwa Tindikali
MFANYABIASHARA maarufu na Mmiliki wa maduka ya Home Shopping Center(HSC), Said Mohamed Saad, ambaye wiki iliyopita alimwagiwa tindikali maeneo ya Msasani City Mall, jijini Dar es Salaam, sasa yuko Afrika Kusini kwa matibabu zaidi. Hali yake inadaiwa kuendelea vizuri, lakini kuna uwezekano wa jicho lake moja kutokuona kabisa baada ya kuathirika sana, lakini jicho la pili liko salama.
Wiki iliyopita majira ya saa moja jioni, mfanyabiashara huyo alimwagiwa tindikali na mtu mmoja ambaye hakufahamika na mara baada ya kutenda tukio hilo, mhusika alikimbia huku mlinzi wa eneo hilo akijaribu kumkimbiza pasipo mafanikio baada ya kuteleza na kuanguka.
Hatua hiyo ilitoa mwanya kwa mtuhumiwa kutoroka eneo la tukio kwa kutumia usafiri aina ya pikipiki.
Hapo awali ilidaiwa kuwa Saad alikuwa anaweza kuzungumza japo amefungwa mashine sehemu ya pua kwa ajili ya kumsaidia kupumua.
Matukio ya watu kumwagiwa tindikali yameonekana kushamiri nchini katika siku za hivi karibuni.
Tukio la kumwagiwa tindikali mmiliki huyo wa Home Shopping Centre, limekuja ikiwa ni takribani wiki mbili tangu Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha, Said Juma Makamba naye ajeruhiwe vibaya usoni kwa kumwagiwa maji maji yanayosadikiwa kuwa ni tindikali majira ya usiku akiwa nyumbani kwake.
Subscribe to:
Posts (Atom)

