Pages

Wachina Wameanza Kukopesha Mikopo ya Bodaboda

Bodaboda Mkoani Mwanza.
Annastazia Fredy,Mwanza
KAMPUNI ya kuuza Pikipiki kutoka china (FEKON) imetoa mkopo wa Pikipiki 240 zenye thamani ya shilingi 460.8million kwa vijana wanaofanya biashara ya Bodaboda Mkoani Mwanza.
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Monarch Hotel Katibu wa jumuia ya vijana Mkoani hapa Abubakari Rubelwa alisema kuwa Kampuni hiyo imekuwa ya kwanza kukubali kutoa mkopo wa Pikipiki hizo ndani ya mwaka mmoja ili kuwawezesha vijana kumudu maisha yao.
“Tunaishukuru Kampuni ya Fekoni kwa sababu ni Kampuni iliyokubali kutukopesha Pikipiki ndani ya mwaka mmoja ambapo kila Pikipiki inagarimu shilingi 1.9million.”alisema Rubelwa.

Aidha Katibu huyo alisema kuwa awali Kampuni hiyo iliwai kutoa Pikipiki 15 zenye thamani ya shilingi 23million vijana wakalipa bila shinda ndiyo maana wameamua kuongeza Pikipiki 240 zitakazo wasaidia vijana wengi hasa walioko kwenye jumuia ya vijana Mkoani hapa.
Mmoja wa Wanachama wa umoja huo Salome Kasiani mkazi wa Kwimba alisema kuwa ajira ni kitu chochote ambacho kinaweza kukupatia pesa sio lazima uwajiriwe, watu wengi wamekuwa wanazitazama kazi ya kuendesha Pikipiki ni ya wanaume pakee yao lakini hata sisi wanawake tunaweza .

Aidha alisema kuwa atahamasisha wanawake wenzake huko Kwimba ili wajitokeze kwa wingi na kujiunga na chama ili wafaidike na chama kwa kujipatia mikopo ya pikipiki ili kuendesha maisha yao. “Mimi nawaomba wanawake wenzangu wasichaguwe kazi kusema hii kwamba ni ya mwanaume nah ii ni ya mwanamke mimi nitajivika jukumu hili kuhamasisha wanawake wajiunge na chama ili kufaidika” alisema Salome.

Prezzo - Celebration of Life (audio)

Mlipuaji wa Bomu la Arusha ni Polisi, Hatukubali Mauaji ya Aina Hii Tena -CHADEMA

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA akizungumza na Waandishi wa Habari jana tarehe 18/06/2013 Makao Makuu ya CHADEMA amesema CHADEMA inao ushahidi wa video kuwa aliyelipua bomu kwenye mkutano wa Chadema Arusha ni Polisi na Polisi wenzake wakamsaidia kutoroka

NAPE ASEMA "MBOWE NA GODBLESS LEMA WANATAKIWA WAWASILISHE USHAHIDI WA TUKIO LA BOMU LA SIVYO SHERIA ITACHUKUA MKONDO WAKE"

 CCM, Nape Nnauye Jeshi la Polisi limetishia kuwakamata Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na limesema litamhoji Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Nnauye baada ya wanasiasa hao kudai kufahamu watu waliohusika na tukio la kurushwa bomu mwishoni mwa wiki iliyopita.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Arusha jana, Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Kamishna Paul Chagonja aliwataka wanasiasa hao kuwasilisha ushahidi wa.. kile wanachofahamu kuhusu kulipuliwa kwa bomu hilo.
Juzi, Mbowe akiwa na Lema, alisema wana ushahidi wa picha za video zikiwahusisha polisi na kulipuliwa kwa bomu hilo katika Uwanja wa Soweto wakati wa mkutano wa kuhitimisha kampeni za udiwani kwa Chadema, Jumamosi iliyopita.

Mkwara wa Chagonja
Kamishna Chagonja aliwataka Mbowe na Lema kupeleka ushahidi ili kusaidia uchunguzi wa tukio hilo.
“Tunamtaka Mbowe na Lema kutoa ushahidi wa askari wetu kuhusika na tukio la bomu pale Soweto. Wasipofanya hivyo tutatumia sheria kuwalazimisha kufanya hivyo kwani yeyote mwenye ushahidi unaoweza kusaidia upelelezi wa kosa la jinai akikataa kuuwasilisha kwa vyombo husika anaweza kuchukuliwa hatua,” alisema.

Nape naye kuhojiwa
Kwa upande wake, polisi limesema litamhoji Nape ambaye alikaririwa jana akidai kuwa Chadema ndiyo waliohusika na urushaji wa bomu kwenye mkutano wao baada ya kuhisi kushindwa kwenye uchaguzi wa kata nne za Jiji la Arusha.
Kamishna Chagonja alisema watamhoji ili kusaidia kazi yao ya upelelezi. Nape aliihusisha Chadema kwa kauli alizoita za kutishia amani zilizowahi kutolewa siku za nyuma kabla ya uchaguzi wa kata za Arusha.

Watatu wakamatwa
Kamishna Chagonja alisema watu watatu wamekamatwa wakihusishwa na tukio la...

SAIDA KAROLI AKIONGEA KUHUSU KUZUSHIWA KUWA AMEKUFA, MSIKILIZE HAPA

SAIDA KAROLI

Video ya Wafuasi wa Chadema Walivyoatawanywa na Mabomu ya Machozi Arusha

Jeshi la polisi mkoani Arusha limetumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi na viongozi wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema waliokuwa wamekusanyika kwenye uwanja wa Soweto ulipotokea mlipuko wa bomu baada ya kukaidi amri ya kutawanyika katika eneo hilo iliyotolewa na jeshi hilo.

I Didn't Step on American Flag on Purpose -Lil Wayne

Wayne Lil Wayne says he didn't intentionally step on the American flag during the shoot for his video "God Bless Amerika" in New Orleans.
"It was never my intention to desecrate the flag of the United States of America. I was shooting a video for a song off my album entitled "God Bless Amerika". The clip that surfaced on the Internet was a camera trick clip that revealed that behind the American Flag was the Hoods of America. In the final edit of the video you will see the flag fall to reveal what is behind it but will never see it on the ground. In most people eyes including my own who were raised in that environment, the Hood is the only America they know and the only America I knew growing up. I was fortunate from my God giving talents to escape the Hood and see the other beautiful places this country has to offer but most people who are born in that environment don't get that chance. That's their view of their America. That was Dwayne M Carter from Hollygrove New Orleans view of America. That's who I'm speaking for in this song".
Wayne wrote on his Facebook wall
Watch video below..

Kimbunga ft Kala Jeremiah - Salamu (Audio)

Video ya Mahojiano Aliyofanyiwa Mtanzania Aliekamatwa na Dawa za Kulevya Misri.

Kwa zaidi ya wiki moja iliyopita habari zilisambaa kwamba binti Mtanzania aliekamatwa na dawa za kulevya nchini Misri angenyongwa siku za karibuni kutokana na hizo dawa alizokamatwa nazo.
صبايا الخير: تهريب المخدرات من الأجانب إلى داخل مصر .. لقاء مع مهربة تنزانية 
Pata nafasi kuona video ya mahojiano ya TV na msichana huyu ambae anadai alikwenda Misri kumtafuta binamu yake, begi alilokamatwa nalo ni lake ila alikua hajui kama lina dawa za kulevya

Soma SABABU ZA JESHI LA POLISI KUTUMIA NGUVU YA MABOMU JIJINI ARUSHA

viwanja vya SowetoJeshi la polisi limekipiga marufuku chama cha demokrasia na maendelo(CHADEMA)kufanya shughuli zozote za kuaga miili ya marehemu kwenye viwanja vya Soweto kwani zoezi la uchunguzi bado linaendelea kwenye viwanja hivyo .
Akizungumza ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas amesema kutokana na uchunguzi unaoendelea wa tukio la bomu kwenye viwanja hivyo imeonelea kuwa si busara kuweka mkusanyiko wa watu kwani kutaharibu upelelezi.
Kamanda Sabas amedai kuwa jeshi la polisi liliwataka viongozi wa chama hicho kuwaeleza wafuasi wao mahali sahihi watakapoweza kufanyia shughuli hiyo lakini si kwenye viwanja hivyo.
Hali kwenye viwanja hivyo imekuwa ya pilika pilika tangu juzi kwa wafuasi wa chama hicho kujikusanya tokea asubuhi hadi jioni kwa madai ya kuomboleza ..
Hata hivyo viongozi wa chama cha demokrasia na maendeleo walikaidi agizo hilo na kuanza kujikusanya uwanjani hapo pamoja na wafuasi wa CHADEMA , hali iliyoleta mvutano kati ya viongozi wa jeshi la polisi na wafuasi hao.
Wakati mabishano hayo yakiendelea, Askari Polisi mmoja alijichanganya na kuingia katikati ya wafuasi wa Chadema pembeni mwa uwanja huo ambao walikua wanasubiri kujua utaratibu wa kuaga miili ya Marehemu waliolipuliwa na bomu June 15 2013.
Baada ya hapo,Wafuasi hao hawakupenda kitendo cha Polisi kujichanganya nao hivyo ikazuka ugomvi huku wakitaka atoke, baada ya dakika kadhaa mabumu yalianza kusikika.

Baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho waliokuwepo uwanjani haponi mbunge wa jimbo la ubungo John Mnyika,Ezekia Wenje,Tundu lissu, Halima Mdee