Pages

Nyota wa Airtel Rising Stars Kwenda Nigeria

Airtel Rising StarsTimu za wavulana na wasichana wenye umri chini ya miaka 17 ambazo zitaiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya kimataifa ya Airtel Rising Stars zinaingia kambini jijini Dar es Salaam kesho (Alhamisi September 5) kufanya maandalizi ya mwisho kabla ya kukwea pipa kwenda nchini Nigeria kushiriki michuano hiyo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo (Jumatano Sept 4), Ofisa Uhusiano wa Airtel Tanzania Jane Matinde alisema wachezaji hao chipukizi watashughulikia na kukamilisha hati zao za kusafiria kati ya kesho, Alhamisi na Ijumaa. “Kwa upende wetu kila kitu kimekamilika kwa ajili ya safari kuelekea kwenye mashindano hayo ya kimataifa ambayo yatashirikisha timu kutoka sehemu mbali mbali barani Afrika,” alisema.

Jumla ya wavulana na wasichana 32 walifuzu kwenda kuiwakilisha Tanzania kwenye mashindano hayo baada ya kuonyesha uwezo mkubwa wa kusakata kabumbu wakati wa fainali za Taifa za Airtel Rising Stars zilizofanyika jijini Dar es Salaam mwezi Juni. Mashindano haya ya kimataifa yanafanyika kwa mara ya pili mwaka huu yakiwa na lengo la kutoa fursa zaidi kwa wachezaji chipukizi kuendeleza vipaji vyao.

Kwa mara ya kwanza mashindano ya kimataifa ya Airtel Rising Stars yalifanyika jijini Nairobi mwaka jana ambapo Tanzania iliwakilishwa na timu ya wavulana pekee ambayo hata hivyo ilitolewa hatua za awali huku timu ya Nigeria ikitawazwa kuwa mabingwa.

“Kulingana na kiwango cha kuridhisha cha wachezaji waliochaguliwa mwaka huu nina imani kwamba timu zetu za Tanzania – wasichana na wavulana – wana nafasi nzuri ya kufanya vizuri,” anasema Matinde ambaye ni mmoja wa maofisa wa Airtel Tanzania waliongoza na timu kwenye mashindano hayo.

Airtel imeanzisha mashindano haya ya vijana barani Afrika kwa nia ya kusaidia upatikanaji wa vijana wenye vipaji vya soka kuanzia ngazi ya chini kabisa hadi ngazi ya Taifa. Airtel Rising Stars inatoa fursa kwa vijana kudhihirisha uwezo wao kwa makocha wa Taifa na kimataifa na kuweza kujiendeleza zaidi kisoka.

Hivi sasa Airtel Rising Stars ni moja ya matukio muhimu ya kisoka kwenye kalenda ya Shirikisho la Mpira wa miguu nchini (TFF). Huanzia katika hatua ya usajili ikifuatiwa na mechi za mtoano ili kupata wachezaji nyota wa kuunda timu za mikoa ambazo huchuana katika ngazi ya Taifa.

Airtel inaendesha muchuano hii kwa kushirikiana na klabu maarufu duniani ya Manchester United ambayo hutoa ushauri wa kiufundi na michuano hii imekuwa na hamasa kubwa katika nchi zote zinazoshiriki.

CHEKI MH.SUGU ALIVYOCHEZEA KICHAPO BUNGENI

Joseph Mbilinyi
Askari wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakimdhibiti Mbunge wa Chadema kutoka jimbo la Mbeya Mjini Mh. Joseph Mbilinyi 'Sugu' wakati akitolewa ndani ya Ukumbi wa Bunge,baada ya kupishana kauli na waheshimiwa wenzake.

JWTZ Yatoa Sababu 200 Zilizoifanya Tanzania Ipambane na Waasi wa M23

JWTZ
Ushiriki wa Tanzania katika Operesheni ya Ulinzi wa Amani nchini DRC, unatokana na mgogoro kati ya Serikali DRC na waasi hususan kikundi cha waasi cha M23. Mgogoro huo ulianza mwezi Aprili 2012 ambapo kikundi cha M23 kilijitoa katika Jeshji la serikali ya DRC na kuanzisha mapigano hali iliyopelekea hali ya usalama nchini DRC kuwa mbaya.

Kufuatia hali hiyo mbaya ya usalama, wakati wa kikao cha International Conference on the Great Lakes Region kilichofanyika tarehe 12 Julai 2012 mjini Addis Ababa, Ethiopia, Mhe. Rais Joseph Kabila aliwasilisha ombi kwa Wakuu wa Nchi za Maziwa Makuu ambazo Rwanda, Uganda, Tanzania, na DRC akaomba nchi wanachama wa Maziwa Makuu zisaidie kuwapokonya silaha waasi wa M23.
Wakuu wa nchi za Maziwa Makuu walikubaliana na ombi hilo na kutoa maelekezo kwa Mawaziri wa Ulinzi ambao walikutana tarehe 01 hadi 2 Agosti 2012 na kujadili maelekezo ya Wakuu wa nchi za Maziwa Makuu. Mawaziri wa Ulinzi walikubaliana kuwa ni muhimu kwa vikundi vyote vya Waasi (ADF, FDLR na M23) kushughulikiwa na wakawasilisha mapendekezo yao kwa Wakuu wa Nchi za Maziwa Makuu.

Tarehe 7 Agosti 2012, Wakuu wa nchi za Maziwa Makuu walikutana tena mjini Kampala, Uganda na kupanga mkakati wa kuanzishwa kwa ‘Neutral Intervention Force (NIF)’ na nchi wanachama wa Nchi za Maziwa Makuu zikaombwa kuchangia askari watakaounda ‘Neutral Intervention Force (NIF)’ambapo Tanzania iliombwa na ikahadi kuchangia kikosi kimoja. Kikao hiki kilitoa maelekezo ya hatua inayofuata kwa Mawaziri wa Ulinzi wa Maziwa Makuu.

Tarehe 7 hadi 8 Sep 2012, Mawaziri wa Ulinzi wa maziwa Makuu, walikutana na kujadili utekelezaji wa uanzishwaji wa ‘Neutral Intervention Force (NIF)’. Wakaunda ‘Military Assessment Team (MAT)’ kufanya tathmini ya tishio. Timu hiyo ililifanya tathmini na kuwasilisha taarifa yake kwenye kikao cha Mawaziri wa Ulinzi kilichofanyika tarehe 25 Oktoba 2012 mjini Goma, DRC na baadaye taarifa hiyo iliwasilishwa kwa Wakuu wa Nchi za Maziwa Makuu ambao waliagiza kushirikishwa kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika (SADC), Umoja wa Afrika(AU) na Umja wa Mataifa(UN) ili kufanikisha mkakati huo.

Nchi wanachamma wa SADC na Nchi za Maziwa Mkuu kwa pamoja walikubaliana na kupendekeza SADC Standby Brigade ipelekwe DRC kama ‘Neutral Intervention Force (NIF)’. Kufuatia ridhaa hiyo nchi wanachama wa SADC ziliombwa kuchangia ambapo nchi mbalimbali wanachama zilikubali kuchangia, lakini Umoja wa Mataifa(UN) ilizipitisha nchi za Tanzania, Afrika Kusini na Malawi kuchangia askari nguvu ya Brigedi moja kuunda NIF ya MONUSCO.

Aidha, Umoja wa Mataifa mwezi Januari 2013 uliridhia mapendekezo ya Wakuu wa Nchi za Maziwa Makuu na Nchi wanachama wa SADC ya kuundwa ‘Neutral Intervention Force (NIF)’ na kupelekwa DRC. Kufuatia idhini hiyo tarehe 28 Machi 2013, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipitisha Azimio (Resolution) namba 2098 (2013) na kutoa jukumu maalumu la ulinzi wa amani nchini DRC, likijumuisha ushiriki wa Neutral Intervention Force (NIF) kama sehemu ya MONUSCO, na ikaitwa ‘Force Intervention Brigade (FIB)’ ambayo kikosi cha Tanzania ni sehemu ya Brigade hiyo.

Kwa mantiki hiyo ieleweke kwamba, Kikosi cha Tanzania kilichopo DRC ni sehemu ya SADC standby brigade iliyotoa mchango wake katika Jeshi la Umoja wa Mataifa (MONUSCO). Kinafanya kazi chini ya Force Commander, MONUSCO na majukumu yake ni:
Kuzuia waasi kujitanua (Prevention of Expansion)
Kuvunja nguvu za waasi (Neutralization)
Kuwapokonya silaha makundi yote ya waasi.

Kwa kuzingatia kuwa kikosi chetu kiko chini ya majeshi ya Umoja wa Mataifa ya MONUSCO, inamanisha kuwa Operesheni hiyo ni ya Umoja wa Mataifa, Tanzania haipigani na M-23 na haina tatizo na Rwanda kuhusiana na Operesheni hiyo na ridhaa ya kikosi chetu kwenda DRC ilikubaliwa pia na Rwanda, nchi ambayo ni mwanachama wa nchi za Maziwa Makuu. Aidha, Rwanda imesaidia sana kwa kuruhusu kikosi cha Tanzania kupitisha watu, vifaa na zana katika nchi yake kupeleka DRC.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi.
6/9/2013
Dar es Salaam.

CHOKOCHOKO BUNGENI: HIVI NDIVYO MBUNGE WA MBEYA SUGU ALIVYO MPIGA ASKARI WA BUNGE

ChidiBenz na Nonini -Get Down (Audio) na Playlist

ChidiBenz na Nonini -Get Down

PICHA ZA RAIS KIKWETE ALIPOKUTANA NA KAGAME KAMPALA LEO

Jakaya Kikwete
Rais Jakaya Kikwete leo amefanya mazungumzo na Rais Paul Kagame wa Rwanda katika mkutano wa saba wa kimataifa wa nchi za maziwa makuu, unaofanyika Kampala, Uganda.
Haijafahamika mara moja walichozungumza, hizi ni picha za mkutano wao.
Jakaya Kikwete
Paul Kagame wa Rwanda
Paul Kagame wa Rwanda
Marais hao wamekutana wakati ambapo uhusiano kati ya nchi hizo mbili unaendelea kuzorota.

How 12 of The World’s Biggest Websites Looked Like at the Beginning

Even the greatest among us had humble beginnings. This is just as true for websites, however, as it is for people.
GoogleGoogle.com (1998)
Even online giants like Amazon, YouTube, Facebook and Twitter were once itty-bitty websites with monochrome homepages, poorly-thought-out logos and boring or stark turn-of-the-century designs.
Mashable,Facebook.com (2004)
YoutubeYoutube.com (2005)
Yahoo
Yahoo.com (1995)
Twitter.com (2006)
Amazon
Amazon.com (1995)
WikipediaWikipedia.org (2001)
MySpaceMySpace.com (2003)
Apple.com (1996) Microsoft
http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2013/09/in2ea.png Microsoft.com