Ilibainika wiki iliyopita kuwa idara ya ujasusi nchini Marekani ilikuwa inakusanya Mamilioni ya rekodi za simu na pia imekuwa ikichunguza watumizi wa mitandao. Idara ya ujasusi nchini Marekani imesema kuwa hatua ya Snowden kutoka siri hiyo ni kosa kubwa la kihalifu na anafanyiwa uchunguzi ili kufunguliwa mashtaka. Awali Snowden aliomba kupewa hifadhi katika kisiwa cha Iceland kutokana na ufichuzi wake ambao anaamini utamweka matatani baada ya kutoa siri ya serikali.
Ufichuzi huu umezua mjadala nchini Marekani kuhusu mpango wa serikali kuyataka kuchunguza mitandao suala ambalo wanasema ni kuingilia uhuru wa watu. Rais Barrack Obama ametetea mpango huo wa idara ya ujasusi kama njia mojawapo ya kupambana na ugaidi duniani na kuhakikisha kuwa Marekani inakuwa salama.
MSAMU