Na Deodatus Balile, Dar es Salaam
Tanzania haitarudi nyuma katika kupeleka majeshi huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kama sehemu ya kikosi cha kuingilia kati cha Umoja wa Mataifa, licha ya maonyo mawili ya maandishi kutoka kikundi cha waasi cha March 23rd Movement (M23), maafisa wa Tanzania wasema.

Waasi wa M23 wakiondoka toka milimani tarehe 30 Novemba, 2012, baada ya kuondoka kijiji cha Karuba cha mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. [Na Phil Moore/AFP]Mkuu wa kijeshi wa M23 Jenerali Sultani Makenga (katikati) akiwaashiria baadhi ya maafisa wake karibu na mji wa Sake, mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, tarehe 30 Novemba, 2012.
Tanzania haitarudi nyuma katika kupeleka majeshi huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kama sehemu ya kikosi cha kuingilia kati cha Umoja wa Mataifa, licha ya maonyo mawili ya maandishi kutoka kikundi cha waasi cha March 23rd Movement (M23), maafisa wa Tanzania wasema.
Salva Rweyemamu, mkurugenzi wa mawasiliano wa raisi wa Tanzania, aliiambia Sabahi kuwa serikali ilipokea barua mbili kutoka kikundi cha M23, ambacho kinapigana ili kuiangusha serikali ya Kongo.

Barua ya kwanza ilielekezwa kwa Mwenyekiti Mkutano wa Kimataifa wa Maziwa Makuu, Raisi wa Uganda Yoweri Museveni, na nyakala kupelekwa kwa wakuu wote wa serikali wa kanda hiyo, akiwemo Raisi wa Tanzania Jakaya Kikwete.
Barua ya pili ilitumwa kwa spika wa Bunge la Taifa Anne Makinda na kutiwa saini na Bertrand Bisimwa, mkuu mpya wa tawi la kisiasa la M23, iliyofika bunge la Tanzania siku ya Jumamosi (tarehe 20 Aprili), vyanzo viliiambia Sabahi.
Katika barua hiyo, M23 iliwataka wabunge wa Dar es Salaam kuishauri serikali dhidi ya kupeleka majeshi huko DRC, na hata kutishia "mauaji" ya majeshi ya Tanzania na wapiganaji wa M23 ikiwa Tanzania itaendelea mbele na upelekaji wa majeshi yake huko.
Kurejesha amani "Lengo la majeshi ya Tanzania sio kuwaua Wakongo bali kurejesha amani," naibu Spika wa Bunge la Taifa la Tanzania Job Ndugai aliiambia Sabahi. "M23 wataona hili kuwa ni..