Pages

Gari la Zima Moto Ilipogeuzwa Gari la Matangazo na Vipaza Sauti Juu!!

Zima Moto
Zima Moto
Zima Moto
SASA KAZI IMEANZA TUOMBE MOTO USITOKEE MAANA SIJUI ITAKUWAJE JIBU MNALO WENYEWE

Chiddi Beenz Ametiririka Kuhusiana na Kutoboa Pua

Chiddi Beenz

Story ya Yule Mwanamke Aliye Chinjwa Kama Kuku na Mpenzi Wake Huko Kahama

Jessica Elialinga
VILIO vilitawala Kata ya Nyahanga wilayani hapa wakati wa kuuaga mwili wa binti Jessica Elialinga (19) aliyeuawa kinyama kwa kuchinjwa kama kuku na mpenzi wake, Musa Petro (27) mkazi wa Shunu kwa sababu zinazodaiwa ni wivu wa kimapenzi.

Jessica Elialinga baada ya kuchinjwa.
Tukio hilo lililoibua simanzi kubwa kutokana na marehemu kuhitimu Kidato cha Nne katika Shule ya Sekondari ya Kata ya Nyihogo, Kahama mwaka jana, lilijiri saa 12:45 Februari 6, mwaka huu.

Kitendo hicho kilifanyika katika banda la mbuzi lililopo nyumbani kwa kijana huyo ambaye baada ya kutekeleza mauaji na yeye alifanya jaribio la kutaka kujitoa roho kwa kisu.

Akisimulia juu ya tukio hilo, rafiki wa karibu wa Musa ambaye aliomba hifadhi ya jina lake kwa ajili ya usalama, alisema wiki moja kabla ya tukio hilo, mtuhumiwa huyo alikuwa akiwatangazia jamaa zake kwamba ana dhamira ya kumuua binti huyo kufuatia kubaini kuwa anamsaliti kimapenzi.

Musa Petro
“Unajua Musa anafanya kazi ya kuchuna ngozi za wanyama machinjio ya Wilaya ya Kahama, alitutangazia dhamira yake hiyo, lakini tulichukulia kauli yake kama mzaha.
“Alisema anataka kufanya hivyo kwa sababu amekuwa akitumia gharama kubwa kwa mpenzi wake huyo tangu walipoanza uhusiano, msichana akiwa kidato cha pili, lakini anatoka kimapenzi na mwanaume mwingine,” alisema rafiki huyo.

Hata hivyo, inadaiwa baada ya mtafaruku wa usaliti, wawili hao walipatana na kuendelea na mapenzi, lakini baada ya mwanafunzi huyo kuhitimu kidato cha nne alibadilika ambapo mwanaume alisikia kuwa tayari ana mwanaume mwingine kutoka jijini Mwanza ambaye walikubaliana kufunga pingu za maisha baada ya kumaliza masomo.
Muuaji Musa Petro, Kushoto
Muuaji Musa Petro.
Jessica Elialinga enzi za uhai wake.
Inadaiwa siku chache kabla ya mauaji hayo, rafiki mmoja wa karibu wa mtuhumiwa alikutana na marehemu njiani na kumsimamisha kwa lengo la kumweleza kauli zenye kutishia maisha yake anazozitoa mpenzi wake, lakini binti huyo hakusimama kumsikiliza.

Baada ya Musa kudaiwa kufaulu kumchinja mpenzi wake huyo na yeye kujikata koromeo na kuanguka akiwa ameishiwa nguvu, kijana mchunga mbuzi ambaye wengi katika eneo hilo humchukulia kama kaka yake Jessica, ndiye aliyekuwa wa kwanza kumshuhudia Musa akiwa katika hali hiyo.

Alipomhoji kulikoni, hakupata jibu zaidi ya kushuhudia jitihada za mtuhumiwa huyo kufungua mlango wa chumbani mwake zikishindikana.
Kijana huyo alitoa taarifa kwa watu ambao walifika na kumchukua Musa na kumkimbiza hospitali ya wilaya kuokoa uhai wake.

Watu waliobaki nyumbani walifuatilia michirizi ya damu hadi kwenye zizi la mbuzi ambako walimkuta Jessica ameshafariki dunia baada ya kuchinjwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Everest Mangala alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo alisema mtuhumiwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani Kahama katika Hospitali ya wilaya hiyo anakoendelea kupatiwa matibabu.

Uchangiaji wa Ujenzi, Maktaba ya Jamii ktk Kijiji cha Lugalo Mkoani Iringa

MAKTABA YA JAMII KATIKA KIJIJI CHA LUGALO MKOA WA IRINGATaasisi isiyokuwa ya kiserikali ina mpango wa kujenga Maktaba ya Jamii katika kijiji cha Lugalo mkoani Iringa.

TUWAFIKIE TANZANIA ORGANISATION Ni asasi isiyokua ya Kiserikali inayojiendesha sio kwa malengo ya kupata faida tunajishughulisha na uhamasishaji wa maendeleo ya elimu vijijini kuhakikisha watoto na vijana wanapata elimu bora ili waweze kuwa wabunifu na kujitegemea.

Unaweza kutuunga mkono kwa kuchangia kuanzia 1,000/= na kuendelea kuwezesha ujenzi wa maktaba ya jamii katika kijiji cha Lugalo.kwa kufanya hivyo utakua umewasidia wanafunzi na jamiii kwa ujumla ya lugalo na vijiji vya jirani kuweza kupata taarifa mbalimbali na kuelimika.Tunaamini matatizo yanayoikabili jamii yetu sisi wenyewe tunatakiwa tuwe wa kwanza kuyatatua kabla ya watu wengine kutoka nje kuja kufanya badala yetu.Mabadiliko ni mimi na wewe pamoja tunaweza.

Tutakua tunatoa taarifa ya fedha iliyopatikana kupitia hili kundi letu.Unaweza changia kupitia MPesa,Tigo Pesa au Account no yetu CRDB kama inavyoonekana kwenye picha. Pia tutakua tukiwajulisha kiasi kilichopatikana na waliochangia kupitia page yetu facebook,website yetu na kwenye wall yangu
MPESA 0754 981 629 TIGO PESA 0712 852 665 CRDB BANK A/C No. 0150450143000

For any enquiries, questions, ideas and any request of engagement, please fill free to contact us and share with us. We are always available. Please visit www.tuwafikie.org

Chadema Walitaka Jeshi la Polisi Kufanya Kazi Bila Shinikizo

Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimesema kilikuwa na taarifa za mapema juu ya uwepo wa mkakati unaoratibiwa na kufanikishwa na maafisa wa ngazi za juu wa usalama wa taifa wa kukihusisha chama hicho na njama za kumdhuru mwenyekiti wa jukwa la wahariri Absalom Kibanda ili kukidhofisha chama hicho kisiasa.

Ney wa Mitego ft Diamond Platinumz - Muziki Gani (Audio)

Dogo Janjaro in South Africa, Cape Town

The promo video of Janjaro's tour to Cape Town/South Africa

Press Briefing

White House Press Briefings are conducted most weekdays from the James S. Brady Press Briefing Room in the West Wing.

Mvua Kali Zaharibu Nyumba Kadhaa Mkoani Mtwara. (Video)

Mvua kubwa zilizonyesha mkoani Mtwara zimesababisha nyumba kadhaa mitaa ya Magomeni Matopeni na Nkana-red katika manispaa ya Mtwara/Mikindani kubomoka, zingine kuingiwa na maji na kusababisha hasara kubwa ya mali na maisha ya watu

Obama Noma

Swali kuhusu hii video? ni kweli Obama alifanya hivi au video ilitengenezwa kwa kuunganishwa?