
RAIS Jakaya Kikwete amesema kuna juhudi nyingi zinafanywa kuleta machafuko nchini na kuweka bayana kuwa wapo baadhi ya watu wanaolipwa ili kuchochea machafuko hayo kwa kutumia mgongo wa dini.
Mbali na wanaotumia dini ambao amesema Serikali itawadhibiti, Rais Kikwete pia ameonya kuwa hatakubali uchochezi wa vurugu unaofanyika kwa kupitia vyombo vya habari. Katika hilo, amesisitiza kuwa hatalifungulia gazeti la kila wiki la MwanaHalisi kwa sababu kutaka wanajeshi waasi, siyo uandishi wa habari na haukubaliki.
Rais Kikwete alisema hayo juzi mjini hapa wakati akijibu hoja zilizoibuliwa katika ripoti ya tathmini ya Mpango wa Afrika Kujitathimini Kiutawala Bora (APRM) kwa Tanzania, iliyowasilishwa hapa.
Ripoti hiyo iliwasilishwa kwa viongozi wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika wanaoshiriki APRM na Barrister Muna, ambaye alikuwa kiongozi wa jopo lililofanya tathimini kwa Tanzania.
Katika ripoti hiyo, kulitolewa changamoto kuwa zimeanza kuonekana dalili za mgawanyiko kwa misingi ya dini nchini Tanzania. Changamoto nyingine zilizoainishwa ni madai ya uhuru wa vyombo vya ...
Mbali na wanaotumia dini ambao amesema Serikali itawadhibiti, Rais Kikwete pia ameonya kuwa hatakubali uchochezi wa vurugu unaofanyika kwa kupitia vyombo vya habari. Katika hilo, amesisitiza kuwa hatalifungulia gazeti la kila wiki la MwanaHalisi kwa sababu kutaka wanajeshi waasi, siyo uandishi wa habari na haukubaliki.
Rais Kikwete alisema hayo juzi mjini hapa wakati akijibu hoja zilizoibuliwa katika ripoti ya tathmini ya Mpango wa Afrika Kujitathimini Kiutawala Bora (APRM) kwa Tanzania, iliyowasilishwa hapa.
Ripoti hiyo iliwasilishwa kwa viongozi wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika wanaoshiriki APRM na Barrister Muna, ambaye alikuwa kiongozi wa jopo lililofanya tathimini kwa Tanzania.
Katika ripoti hiyo, kulitolewa changamoto kuwa zimeanza kuonekana dalili za mgawanyiko kwa misingi ya dini nchini Tanzania. Changamoto nyingine zilizoainishwa ni madai ya uhuru wa vyombo vya ...



