Talk Show Celebrity Oprah Winfrey in Serengeti National Park

One of the world’s recognised Television talk show celebrity Oprah Winfrey is touring Serengeti National Park for what is described as private excursion.
The woman behind the popular ‘Oprah Winfrey’ shows, Oprah, who is also a famous film actress and currently playing the role of Gloria Gaines in the 2013 movie ‘The Butler,’ is reportedly, going to be in or around the Serengeti National Park for the whole week starting this weekend.
“It is going to be Oprah’s private tour,” admitted Mr Paschal Shelutete the Public Relations Manager for Tanzania National Parks (TANAPA) which manages Serengeti, the country’s second largest National Park, but which is also the most known.
Her private excursion in the Serengeti, however, won’t prevent Oprah from meeting and hold talks with the Deputy Minister for Natural Resources and Tourism, Mr Lazaro Nyalandu who is also flying to Serengeti to welcome the pop-culture doyenne and founder of television talk shows media genre.
Ever since she debuted in the 1985 film, ‘Colour Purple’ Oprah has starred in 28 other movies in addition to producing several Television Documentaries and publishing three books.
Whether we should expect her next film or TV documentary to be filmed in Serengeti is yet to be seen but the country’s popular Park, home to the legendary migration of over 2 million wildebeests and Zebras, the queen may be interested to capture a bit of the spectacular show.
Winfrey has remained the only African American to rank among America’s 400 richest people nearly every year since 1995. With a net worth of US $800 million, Winfrey is believed to be the richest African American of the 20th century.
She has also won, and nominated for, various outstanding awards including the ‘Academy Awards,’ ‘Emmy awards,’ ‘Golden Globe Award,’ ‘PGA Awards’ and got named as best talk show presenter and host several times.
Winfrey has remained the only African American to rank among America’s 400 richest people nearly every year since 1995 and is believed to be the richest African American of the 20th century.
She is also generous because in 2004, Winfrey became the first black person to rank among the 50 most generous Americans and she remained among the top 50 until 2010. By 2012 she had given away about US $400 million to educational causes.
Tanzania Daily News/ Bizu/WENN
Uchaguzi Mdogo wa Madiwani Arusha Wageuka Vurugu Tupu
Uchaguzi mdogo katika kata nne za Jiji la Arusha unafanyika leo, huku Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), ikiwapiga marufuku Mkuu wa Mkoa, Magessa Mulongo na Mkuu wa Wilaya ya Arusha, John Mongella kuingia kwenye vituo vya kupigia kura, wala kujihusisha kwa namna yoyote na zoezi la upigaji kura ikisema siyo jukumu lao kisheria.
Mbali ya NEC kupiga marufuku viongozi hao wa kisiasa kukaribia vituo hivyo, uchaguzi huo umekumbwa na matukio kadhaa likiwamo la Mbunge wa Jimbo la Arusha, Godbless Lema pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Taifa Chadema(Bavicha), John Heche, kunusurika kuswekwa rumande jana.
“RC na DC hawana haki wala mamlaka ya kujihusisha kwenye zoezi na shughuli za upigaji kura. Mwenye dhamana, wajibu na haki ya shughuli zote za upigaji kura ni Mkurugenzi wa Jiji ambaye ni mwakilishi wa NEC pamoja na maofisa wengine wanaotambuliwa kisheria,” alisema Mwenyekiti wa NEC Jaji Damian Lubuva jana.
Lema na Heche walinusurika kuswekwa rumande baada ya kufika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Arusha, wakishinikiza jeshi hilo, kukamata magari matatu waliyodai kuwa ni ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) na kubadilishwa namba yakihofiwa kwamba huenda yakatumika kuvuruga uchaguzi wa leo.
Tukio hilo la aina yake, lilitokea jana asubuhi baada ya viongozi hao, kufika polisi na kutoa taarifa hiyo, wakieleza kuwa lakini waliambiwa waondoke kwa kuwa gari kubadili namba siyo kosa ambapo pia walitakiwa kumtaja aliyewaeleza kama magari hayo yatatumika kufanya uhalifu.
Aidha, viongozi wa vyama vyote vya siasa ambao sio mawakala wala wagombea, wamepigwa marufuku kuingia kwenye vituo vya kupigia kura, wala kujihusisha kwa namna yoyote na zoezi la upigaji kura badala yake wakiwa ni wakazi wa kata husika kupiga kura na kuondoka maeneo hayo.
Mwenyekiti wa NEC, alitoa tamko la kuzuia viongozi hao jana alipozungumza na waandishi wa habari kuelezea mipango na mikakati ya tume yake katika kufanikisha zoezi hilo linalofanyika baada ya kuahirishwa mara mbili.
Mbele ya makamu wake Jaji Mkuu mstaafu wa Zanzibar, Jaji Hamid Mohamoud Hamid, Jaji Lubuva alitaja orodha ya watu 12 wenye haki kisheria kuingia kwenye vituo vya kupigia kura na kujihusisha na zoezi la upigaji, kuhesabu, kujumlisha kura kuwa ni msimamizi wa kituo, msimamizi msaidizi wa kituo, mawakala wa vyama na wapiga kura.
Wengine ni Mkurugenzi wa Uchaguzi, mgombea, mjumbe wa NEC, Ofisa wa NEC, Mratibu wa NEC mkoa, askari polisi au mtu yeyote anayehusika na usalama katika kituo cha kupiga kura, mtu anayemsaidia mpigakura asiyejiweza na mwangalizi wa uchaguzi aliyeidhinishwa na NEC kimaandishi na katika utaratibu uliowekwa.
Uchaguzi huo unafanyika leo baada ya kuahirishwa Juni 16, mwaka huu, baada ya bomu la kutupa kwa mkono kulipuka kwenye mkutano wa Chadema wa kufunga kampeni kwenye Viwanja vya Soweto, Arusha.
Agizo la kupiga marufuku kujihusisha na Uchaguzi Mkuu wa Mkoa(Mulongo) na Mkuu wa Wilaya(Mongella) ambao ni makada na wajumbe wa Kamati za Siasa na Halmashauri za Mkoa na Wilaya za CCM, limekuja wakati kukiwa na tuhuma kutoka kwa vyama vya upinzani, hasa Chadema kuwa wanatumia nyadhifa zao kukibeba chama tawala.
Akizungumzia kunusurika kuwekwa rumande, Heche alisema kutokana na majibu ya polisi wao wakiomba wapewe hata fursa ya kuandika maelezo kuhusu tukio hilo au wapewe polisi kwenda kuzikamata gari hizo, lakini waligomewa, ndipo likatolewa agizo la kukamatwa kuwekwa rumande kwa Lema.
“Mimi niligoma nikasema kwa nini akamatwe wakati tunaleta wote taarifa hapa basi watukamate wote, jukumu la polisi ni kuchunguza kwa kuwa sisi tuna taarifa magari hayo yatatumika kuteka vijana wetu na kuvuruga uchaguzi,”alisema Heche.
Alitaja magari hayo (namba tunazo) kuwa moja ni la CCM Wilaya ya Arusha na magari mengine mawili.
Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Aman Golugwa alisema kuwa wanashangazwa na polisi kukataa kukamata magari hayo na kwamba katika uchunguzi wao wamebaini moja ya namba mpya za magari hayo ni za moja ya kampuni ya nje ya Arusha.
“Tumeshangaa, badala ya polisi kuchunguza wanataka kukamata viongozi wetu, kweli hii ni halali?”alihoji Golugwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas hakupatikana jana kuzungumzia tukio hilo, baada ya simu yake kupigwa bila majibu huku ikielezwa kuwa alikuwa wilayani Monduli katika sherehe za kutoa kamisheni wanajeshi wa Chuo cha Maofisa wa Jeshi Monduli(TMA), ambapo Rais Jakaya Kikwete alikuwapo na viongozi wengine.
NEC ‘yahamishia’ ofisi Arusha
Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC), ‘imehamishia’ kwa muda ofisi zake jijini Arusha kuhakikisha zoezi la kura katika Kata za Themi, Kimandolu, Elerai na Kaloleni linafanyika kwa ufanisi.
Pamoja na Mwenyekiti wa wa NEC, Makamu wake, makamishna wanne na Mkurugenzi wa NEC, Julius Mallaba pia wapo Arusha kusimamia zoezi hilo.
Makamishna wa NEC waliopo Arusha ni Jaji wastaafu John Mkwawa, Mary Longway, Profesa Amon Chariga na Mchaka Mchanga, walioambatana na watendaji kadhaa wa tume hiyo kutoka Dar es Salaam.
Akijibu swali la kwa nini wote wako jijini Arusha, Jaji Lubuva alisema wingi na uwepo wao umetokana na hali na mazingira halisi ya siasa za Jiji la Arusha kwa kuzingatia sababu za uchaguzi huo kuahirishwa mara mbili Juni 16 na 30, mwaka huu.
“Pamoja na ukweli kwamba Mkurugenzi wa Jiji ndiye msimamizi wa uchaguzi akisaidiana na watendaji wengine, mimi na makamishna wengine wa NEC tuko hapa kwa ajili ya kusimamia utendaji, kutoa ushauri na ufafanuzi kwa karibu zaidi pale jambo lolote linapojitokeza,” alisema Jaji Lubuva.
Wapiga kura kutoruhusiwa kukaa karibu na vituo vya kura
Akizungumzia maandalizi na taratibu zitakazotumika leo, Jaji Lubuva alisema wapiga kura wanashauriwa kurejea nyumbani kusubiri matokeo mara baada ya kupiga kura, badala ya kukaa karibu na vituo ili kuepuka mikusanyiko kutokana na Jiji la Arusha kukumbwa na milipuko ya mabomu.
Hata hivyo, wakati Jaji Lubuva akiwataka wananchi kuepuka mikusanyiko kwa hofu ya mabomu, mkutano mkubwa wa Injili unaohubiriwa na Askofu Emanuel Lazaro unaendelea katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid.
Karatasi za kura na fomu za matokea zabadilishwa rangi
Kutokana na zoezi la kupiga kura Arusha kuahirishwa Juni 16, mwaka huu baada ya karatasi za kura na fomu za matokeo kusambazwa, Jaji Lubuva alisema NEC imebadilisha rangi za karatasi hizo na fomu za matokeo kuepuka udanganyifu na hujuma yoyote.
Taarifa zinasema NEC imelazimika kubadilisha karatasi za kura na fomu za matokeo baada ya baadhi ya karatasi za kura za awali kudaiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha na hazipatikana hadi leo.
Kauli ya Chadema kuhusu wapigakura kurejea majumbani
Chadema kimekataa ushauri wa NEC wa kutaka wananchi kurejea nyumbani baada ya kupiga kura, badala yake kimesisitiza kuwa wafuasi wa chama hicho watakaa umbali wa zaidi ya mita 100 kutoka vituo vya kupigia kura kama sheria inavyoelekeza.
Mwananchi
Mbali ya NEC kupiga marufuku viongozi hao wa kisiasa kukaribia vituo hivyo, uchaguzi huo umekumbwa na matukio kadhaa likiwamo la Mbunge wa Jimbo la Arusha, Godbless Lema pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Taifa Chadema(Bavicha), John Heche, kunusurika kuswekwa rumande jana.
“RC na DC hawana haki wala mamlaka ya kujihusisha kwenye zoezi na shughuli za upigaji kura. Mwenye dhamana, wajibu na haki ya shughuli zote za upigaji kura ni Mkurugenzi wa Jiji ambaye ni mwakilishi wa NEC pamoja na maofisa wengine wanaotambuliwa kisheria,” alisema Mwenyekiti wa NEC Jaji Damian Lubuva jana.
Lema na Heche walinusurika kuswekwa rumande baada ya kufika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Arusha, wakishinikiza jeshi hilo, kukamata magari matatu waliyodai kuwa ni ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) na kubadilishwa namba yakihofiwa kwamba huenda yakatumika kuvuruga uchaguzi wa leo.
Tukio hilo la aina yake, lilitokea jana asubuhi baada ya viongozi hao, kufika polisi na kutoa taarifa hiyo, wakieleza kuwa lakini waliambiwa waondoke kwa kuwa gari kubadili namba siyo kosa ambapo pia walitakiwa kumtaja aliyewaeleza kama magari hayo yatatumika kufanya uhalifu.
Aidha, viongozi wa vyama vyote vya siasa ambao sio mawakala wala wagombea, wamepigwa marufuku kuingia kwenye vituo vya kupigia kura, wala kujihusisha kwa namna yoyote na zoezi la upigaji kura badala yake wakiwa ni wakazi wa kata husika kupiga kura na kuondoka maeneo hayo.
Mwenyekiti wa NEC, alitoa tamko la kuzuia viongozi hao jana alipozungumza na waandishi wa habari kuelezea mipango na mikakati ya tume yake katika kufanikisha zoezi hilo linalofanyika baada ya kuahirishwa mara mbili.
Mbele ya makamu wake Jaji Mkuu mstaafu wa Zanzibar, Jaji Hamid Mohamoud Hamid, Jaji Lubuva alitaja orodha ya watu 12 wenye haki kisheria kuingia kwenye vituo vya kupigia kura na kujihusisha na zoezi la upigaji, kuhesabu, kujumlisha kura kuwa ni msimamizi wa kituo, msimamizi msaidizi wa kituo, mawakala wa vyama na wapiga kura.
Wengine ni Mkurugenzi wa Uchaguzi, mgombea, mjumbe wa NEC, Ofisa wa NEC, Mratibu wa NEC mkoa, askari polisi au mtu yeyote anayehusika na usalama katika kituo cha kupiga kura, mtu anayemsaidia mpigakura asiyejiweza na mwangalizi wa uchaguzi aliyeidhinishwa na NEC kimaandishi na katika utaratibu uliowekwa.
Uchaguzi huo unafanyika leo baada ya kuahirishwa Juni 16, mwaka huu, baada ya bomu la kutupa kwa mkono kulipuka kwenye mkutano wa Chadema wa kufunga kampeni kwenye Viwanja vya Soweto, Arusha.
Agizo la kupiga marufuku kujihusisha na Uchaguzi Mkuu wa Mkoa(Mulongo) na Mkuu wa Wilaya(Mongella) ambao ni makada na wajumbe wa Kamati za Siasa na Halmashauri za Mkoa na Wilaya za CCM, limekuja wakati kukiwa na tuhuma kutoka kwa vyama vya upinzani, hasa Chadema kuwa wanatumia nyadhifa zao kukibeba chama tawala.
Akizungumzia kunusurika kuwekwa rumande, Heche alisema kutokana na majibu ya polisi wao wakiomba wapewe hata fursa ya kuandika maelezo kuhusu tukio hilo au wapewe polisi kwenda kuzikamata gari hizo, lakini waligomewa, ndipo likatolewa agizo la kukamatwa kuwekwa rumande kwa Lema.
“Mimi niligoma nikasema kwa nini akamatwe wakati tunaleta wote taarifa hapa basi watukamate wote, jukumu la polisi ni kuchunguza kwa kuwa sisi tuna taarifa magari hayo yatatumika kuteka vijana wetu na kuvuruga uchaguzi,”alisema Heche.
Alitaja magari hayo (namba tunazo) kuwa moja ni la CCM Wilaya ya Arusha na magari mengine mawili.
Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Aman Golugwa alisema kuwa wanashangazwa na polisi kukataa kukamata magari hayo na kwamba katika uchunguzi wao wamebaini moja ya namba mpya za magari hayo ni za moja ya kampuni ya nje ya Arusha.
“Tumeshangaa, badala ya polisi kuchunguza wanataka kukamata viongozi wetu, kweli hii ni halali?”alihoji Golugwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas hakupatikana jana kuzungumzia tukio hilo, baada ya simu yake kupigwa bila majibu huku ikielezwa kuwa alikuwa wilayani Monduli katika sherehe za kutoa kamisheni wanajeshi wa Chuo cha Maofisa wa Jeshi Monduli(TMA), ambapo Rais Jakaya Kikwete alikuwapo na viongozi wengine.
NEC ‘yahamishia’ ofisi Arusha
Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC), ‘imehamishia’ kwa muda ofisi zake jijini Arusha kuhakikisha zoezi la kura katika Kata za Themi, Kimandolu, Elerai na Kaloleni linafanyika kwa ufanisi.
Pamoja na Mwenyekiti wa wa NEC, Makamu wake, makamishna wanne na Mkurugenzi wa NEC, Julius Mallaba pia wapo Arusha kusimamia zoezi hilo.
Makamishna wa NEC waliopo Arusha ni Jaji wastaafu John Mkwawa, Mary Longway, Profesa Amon Chariga na Mchaka Mchanga, walioambatana na watendaji kadhaa wa tume hiyo kutoka Dar es Salaam.
Akijibu swali la kwa nini wote wako jijini Arusha, Jaji Lubuva alisema wingi na uwepo wao umetokana na hali na mazingira halisi ya siasa za Jiji la Arusha kwa kuzingatia sababu za uchaguzi huo kuahirishwa mara mbili Juni 16 na 30, mwaka huu.
“Pamoja na ukweli kwamba Mkurugenzi wa Jiji ndiye msimamizi wa uchaguzi akisaidiana na watendaji wengine, mimi na makamishna wengine wa NEC tuko hapa kwa ajili ya kusimamia utendaji, kutoa ushauri na ufafanuzi kwa karibu zaidi pale jambo lolote linapojitokeza,” alisema Jaji Lubuva.
Wapiga kura kutoruhusiwa kukaa karibu na vituo vya kura
Akizungumzia maandalizi na taratibu zitakazotumika leo, Jaji Lubuva alisema wapiga kura wanashauriwa kurejea nyumbani kusubiri matokeo mara baada ya kupiga kura, badala ya kukaa karibu na vituo ili kuepuka mikusanyiko kutokana na Jiji la Arusha kukumbwa na milipuko ya mabomu.
Hata hivyo, wakati Jaji Lubuva akiwataka wananchi kuepuka mikusanyiko kwa hofu ya mabomu, mkutano mkubwa wa Injili unaohubiriwa na Askofu Emanuel Lazaro unaendelea katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid.
Karatasi za kura na fomu za matokea zabadilishwa rangi
Kutokana na zoezi la kupiga kura Arusha kuahirishwa Juni 16, mwaka huu baada ya karatasi za kura na fomu za matokeo kusambazwa, Jaji Lubuva alisema NEC imebadilisha rangi za karatasi hizo na fomu za matokeo kuepuka udanganyifu na hujuma yoyote.
Taarifa zinasema NEC imelazimika kubadilisha karatasi za kura na fomu za matokeo baada ya baadhi ya karatasi za kura za awali kudaiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha na hazipatikana hadi leo.
Kauli ya Chadema kuhusu wapigakura kurejea majumbani
Chadema kimekataa ushauri wa NEC wa kutaka wananchi kurejea nyumbani baada ya kupiga kura, badala yake kimesisitiza kuwa wafuasi wa chama hicho watakaa umbali wa zaidi ya mita 100 kutoka vituo vya kupigia kura kama sheria inavyoelekeza.
Mwananchi
Sheikh wa Wilaya Arushiwa Tindikali
Sheikh Makamba anayekaimu nafasi hiyo alikutwa na hayo kati ya Saa 4:00 hadi 5:00 usiku wa kuamkia juzi akitoka kusali Tarawei na alilazwa wodi namba nne katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru kwa matibabu.
Jicho la kushoto la Sheikh huyo limeathirika, huku akiwa amebabuka na kuvimba usoni, kifuani, mkono wa kushoto na mgongoni.
Akizungumza kwa taabu kitandani kwake alikolazwa, Sheikh Makamba ambaye pia ni Imamu wa Msikiti wa Sekei wilayani Arumeru alisema alimwagiwa tindikali muda mfupi baada ya kurejea nyumbani kwake akitoka kuswali.
“Nilipotoka Msikitini, nilisindikizwa hadi nyumbani na vijana wawili nilioongozana nao kutoka msikitini ambao walihakikisha nimeingia ndani salama. Lakini kabla ya kulala nilitoka nje kwa ajili ya kujisaidia kwenye choo cha nje ndipo nilimwona mtu amesimama pembeni ya nyumba nikiwa najitahidi kumwangalia ili nimtambue, ghafla alinimwagia kitu cha majimaji usoni,” alisema Sheikh Makamba.
Ingawa hataki kuingia kwa undani kuhusu anaowatuhumu na sababu za kumwagiwa tindikali, Sheikh Makamba alisema anadhani jambo hilo linatoakana na ugomvi wa madaraka msikitini hapo.
Katibu wa Bakwata Wilaya ya Arumeru, Sheikh Yahaya Husein Mwangela aliwaomba polisi kuchunguza tukio hilo ili kuondoa hofu miongoni mwa viongozi wa Bakwata.
Hili ni tukio la pili kwa viongozi wa Bakwata Arusha kumwagiwa tindikali baada ya Oktoba mwaka jana, Katibu wa Baraza hilo Mkoa wa Arusha, Abdukarim Njonjo kulipuliwa na kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu. Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa hadi juzi kulikuwa hakuna mtu aliyekamatwa.
ri imeanza upelelezi na uchunguzi wa kina wa tukio hilo kubaini wahusika.
Hadi jana jioni, hakuna mtu aliyekuwa akishikiliwa polisi kwa mahojiano kuhusu tukio hilo.
Mwananchi
NEC Yawataka Wakazi Arusha Kuondoka Vituoni Baada ya Kupiga Kura
Tume ya Taifa ya uchaguzi( NEC) imetoa tamko kuhusu uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata nne za jiji la Arusha unaotarajiwa kufanyika Jumapili hii na kuwataka wakazi wa Arusha kuwa watulivu na kuondoka katika vituo baada ya kupiga kura zao.
Blog Zote za Tanzania Zinapatikana Ndani ya Blog Moja (Directory) - Bongo Blogs

>> Bongo Blogs
http://bongoblogs.blogspot.com
Blog yako ya Taifa
Tanzania's Hadzabe. Bushman at the Lake Eyasi (Video)
The Hadza, or Hadzabe, are an ethnic group in north-central Tanzania, living around Lake Eyasi in the central Rift Valley and in the neighboring Serengeti Plateau. The Hadza number just under 1000. Some 300--400 Hadza live as hunter-gatherers, much as their ancestors have for thousands or even tens of thousands of years; they are the last full-time hunter-gatherers in Africa.
STARS YALAZWA 1-0 NA UGANDA, HASHEEM THABEET wa NBA AWA KIVUTIO KIKUBWA KWA MASHABIKI UWANJANI
Mtanzania anayecheza kikapu katika Ligi ya Marekani maarufu kama NBA, Hasheem Thabeet, amekuwa kivutio kikubwa kwa mashabiki wa soka kwenye Uwanja wa Taifa,Dar.
Thabeet anayecheza katika timu ya Thunder, aliibuka na kuwasalimia mashabiki wakati Taifa Stars ikivaa Uganda nao walimshangilia kwa nguvu sana.
BAO pekee la Dennis Iguma dakika ya 46 jioni hii limeiwezesha Uganda kuibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Tanzania kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kujiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kwenye michuano ya Ubingwa wa Mataifa wa Mataifa Afrika (CHAN), inayohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee.

Amri Kiemba akipasua ngome ya Uganda katika mchezo wa leo Uwanjqa wa Taifa, Dar es Salaam.
Iguma aliifungia The Cranes bao hilo, baada ya kutokea piga nikupige langoni mwa Stars kufuatia krosi maridadi ya Brian Majwega, ambaye leo alikuwa mwiba mkali kwa Taifa Stars.
Hadi mapumziko hakuna timu iliyofanikiwa kuona lango la mwenzake na kwa ujumla katika dakika zote hizo 45 hakukuwa na shambulizi la kutisha kwa pande zote.
Brian Majwega alifanikiwa kumgeuza uchochoro Erasto Nyoni na kuingia ndani mara kadhaa, lakini pasi na krosi zake ziliokolewa na mabeki wa Stars inayofundishwa na Mdenmark, Kim Poulsen.
Mrisho Ngassa alipewa mipira mirefu kadhaa, lakini mabeki wa Uganda wakiongozwa na mkongwe, Nahodha wao, Hassan Wasswa walisimama imara kumdhibiti.
Mashambulizi mengine ya Stars yalipitia kwa John Bocco ‘Adebayor’, ambaye alikuwa anapigiwa mipira mirefu, lakini alidhibitiwa pia. Timu zote zilicheza sawa kipindi cha kwanza.
Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko, Stars ikiwapumzisha beki Erasto Nyoni na kiungo Mwinyi Kazimoto na kuwaingiza David Luhende na Haroun Chanongo, lakini walikuwa ni Uganda wanaofundishwa na makocha wa zamani wa klabu ya Yanga, Mserbia Milutin Sredojevic ‘Micho’ anayesaidiwa na Sam Timbe waliobuka vinara.
Lakini baada ya kufungwa Stars, waliongeza kasi na nguvu ya uchezaji na kufanikiwa tu kulitia misukosuko lango la Uganda na si kupata bao japo la kusawazisha.
Matokeo hayo yanamaanisha Stars itahitaji kushinda ugenini kuanzia mabao 2-0 wiki mbili zijazo ili isonge mbele, vinginevyo itakuwa imetupwa nje ya mashindano hayo.
Katika mchezo wa leo kikosi cha Stars kilikuwa; Taifa Stars; Juma Kaseja, Erasto Nyoni/David Luhende, Shomary Kapombe, Aggrey Morris, Kevin Yondan, Frank Domayo, Amri Kiemba, Salum Abubakar, John Bocco ‘Adebayor’, Mwinyi Kazimoto/Haruna Chanongo na Mrisho Ngassa.
The Cranes; Hamza Muwonge, Hassan Wasswa, Nico Wadada, Brian Majwega, Savio Kabugo, Richard Kasaga, Dennis Iguma, Said Kyeyune, Joseph Mpanda, Patrick Edema/Ivan Ntege na Tonny Odur/Frank Kalanda.

Mshambuliaji wa timu ya Taifa (Taifa Stars),John Boko (14) akiwa na mpira mbele ya Beki wa timu ya Uganda ( The Cranes) katika mchezo wa kuwania tiketi ya kucheza Kombe la mashindano ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN),uliomalizika hivi punde kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Taifa Stars imekubali kipigo cha Bao 1-0 kutoka kwa Uganda.


Mrisho Ngassa akitaka kuwatoka Mabeki wa Uganda wakati wa mchezo wa kuwania tiketi ya kucheza Kombe la mashindano ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN),uliomalizika hivi punde kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Taifa Stars imekubali kipigo cha Bao 1-0 kutoka kwa Uganda.


Subscribe to:
Posts (Atom)