Pages

NTV News Update July 9, 2013 (Video)

Taifa Stars Yaendelea na Mazoezi Kuikabili Uganda.

Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars imeendelea na mazoezi huku golikipa na nahodha wa timu hiyo Juma Kaseja akipewa somo la kuondoa msongo wa mawazo.

Ludovick Aendelea Kusota Rumande

Ludovick
WAKATI Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare akiwa nje kwa dhamana mwezi mmoja sasa, mwenzake Ludovick Joseph(mwenye pingu) anaendelea kusota rumande kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana. Hayo yalibainika jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisumu, wakati kesi inayomkabili Lwakatare na mwenzake ilipotajwa mbele ya Hakimu Mkazi, Aloyce Katemana.

Wakili wa Serikali, Mkuu Ponsian Lukosi alidai mahakamani kwamba upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, wanaomba tarehe nyingine ya kutajwa na mshtakiwa Ludovick hajatimiza masharti ya dhamana.

Hakimu Katemana alikubali kuahirisha kesi hiyo hadi Julai 22 mwaka huu na aliamuru mshtakiwa aendelee kuwepo rumande hadi atakapopata wadhamini watakaotimiza masharti.

Lwakatare na Ludovick walikubaliwa dhamana baada ya kufutiwa mashitaka matatu ya ugaidi na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na kubakiwa na shitaka moja la kula njama ya kumdhuru kwa sumu Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mwananchi, Dennis Msacky.

Katemana baada ya kupitia hoja za kuomba dhamana zilizotolewa na wakili Peter Kibatala, alikubali kuwapa dhamana washtakiwa hao kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili wanaotoka katika taasisi zinazotambulika kisheria, ambao kila mmoja atasaini dhamana ya Sh milioni 10 pamoja na washitakiwa wenyewe.

Hakimu Katemana pia aliwataka washitakiwa hao kusalimisha hati zao za kusafiria mahakamani na kutotoka nje ya Dar es Salaam bila ya kuwa na kibali cha Mahakama.

Juni 10 mwaka huu, baada ya kukubaliwa dhamana, Lwakatare alidhaminiwa na kumwacha Ludovick akiendelea kusota rumande kwa kukosa wadhamini.

Hata hivyo uamuzi wa kuwapa dhamana washtakiwa hao ulikatiwa rufaa na upande wa Jamhuri katika Mahakama Kuu ya Tanzania wakipinga hatua hiyo.

Pia Jamhuri iliwasilisha maombi katika Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ikitaka ifanyie marejeo uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam wa kuyafuta mashtaka matatu ya ugaidi yaliyokuwa yakiwakabili washtakiwa hao. Uamuzi huo ulitolewa na Jaji Laurence Kaduri.

Washtakiwa hao walifikishwa kwa mara ya kwanza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Machi 18, mwaka huu wakikabiliwa na mashitaka hayo manne ya ugaidi, ambayo baadaye yalifutwa na Hakimu Emilius Mchauru baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), kudai hana nia ya kuendeleza mashitaka ya ugaidi dhidi yao.

Baada ya kufutiwa mashitaka hayo, washitakiwa hao walikamatwa tena na kufunguliwa mashitaka mengine yanayofanana na hayo mbele ya Hakimu Katemana ambayo pia yalifutwa na Jaji Kaduri. 
NA KULWA MZEE, DAR ES SALAAM
MTANZANIA

Eti Yupi Hayawani Zadi ya Wote?

Hayawani

SARS Nabs two Women with Drugs Worth Millions from Tanzanian Flight (Video)

The South African Revenue Services has made its biggest drug seizure at any border post after taking possession of Tik worth R42.6 million at OR Tambo International Airport.

ZEETOWN SOJAZ Ft FREDRIGO - CHINJACHINJA (Audio)

ZEETOWN SOJAZ Ft FREDRIGO - CHINJACHINJA

WANAFUNZI WALEVI WAKAMATWA KENYA

Polisi wa Kenya
Polisi wa Kenya wamewakamata zaidi ya wanafunzi elfu moja baada ya kupatikana wakiwa walevi mjini Nairobi wikendi hii.
Polisi waliendesha msako katika mabaa na vilabu vya burudani baada ya kupokea malalamishi kwamba watoto wa shule wamekua wakifurika kuburudika.

Kwa sasa wanafunzi wengi hawako shuleni baada ya waalimu wa Kenya kugoma wakitaka serikali kuwalipa marupurupu yao kutokana na ahadi iliyotolewa kwao na serikali mapema miaka ya themanini.

Mgomo huo umeingia wiki ya tatu sasa hali iliyofanya wanafunzi kukosa cha kufanya na hivyo kuanza kwenda kwenye vilabu vya burudani nyakati za usiku.
Katika kuzima tabia hii polisi mjini Nairobi mwishoni mwa wiki walifanya msako mkali katika mabaa na sehemu za burudani na kuwanasa watoto zaidi ya 1,000.

Polisi walianza kuwa na wasiwasi wakati visa vya unyang'anyi vilipoongezeka katika mji mikubwa nchini Kenya. Wasiwasi ulizidi wakati walalamikaji walipokuwa wakidai kuwa wanaowapora na kuwapiga kabari ni kundi la watoto wanaodhaniwa kuwa ni wa shule.
Na mabaa na maeneo ya burudani ilipoanza kufurika polisi wakaona ni wakati muafaka wa kuchukua hatua.

Polisi sasa wametoa onyo kwa wenye mabaa nchini kenya kuheshimu sheria za biashara.
Baada ya wanafunzi kukosa kurudi nyumbani na wengine kuripotiwa kutoroka katika shule zao za mabweni wazazi walifurika katika vituo mbali mbali vya polisi kujua hatma ya watoto wao.
Lakini wengi wa wazazi waliokuwa wamefurika katika kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi walielekeza lawama zao kwa mgomo wa sasa wa walimu unaoendelea.

Polisi wanasema mtindo huu mpya wa watoto kutoroka madarasani na kuvamia maeneo ya burudani na ma baa sio tatizo la Nairobi pekee bali limeenea katika miji mingi ya Kenya.

Na kabla mambo hayaja haribika zaidi wazazi wanamtaka rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kuingilia kati mgomu huo wa walimu kuhusu mishahara na marupurupu mbali mbali
BBC

Steve Kafire feat. Ben Pol - Everytime [Official Video] HD

Mkasi TV with Kajala (Msimu Mpya)

Richest Rappers In The World 2013 -List

diddy
  • 1. Diddy – Net Worth: $580 million (up $80 million)
  • 2. Jay-Z – Net Worth: $500 million (up $25 million)
  • 3. Dr. Dre – Net Worth: $360 million (up $100 million)
  • 4. Master P – Net Worth: $350 million (no change)
  • 5. 50 Cent – Net Worth: $260 million (up $10 million)
  • 6. Birdman – Net Worth: $150 million (up $35 million)
  • 7. Eminem – Net Worth: $140 million (up $20 million)
  • 8. Snoop Dogg – Net Worth: $130 million (up $10 million)
  • 9. Ice Cube – Net Worth: $120 million (up $20 million)
  • 10. Lil Wayne – Net Worth: $110 million (up $15 million)
  • 11. Kanye West – Net Worth: $100 million (up $10 million)
  • 12. LL Cool J – Net Worth: $85 million (up $5 million)
  • 13. Timbaland – Net Worth: $80 million (up $5 million)
  • 14. Pharrell Williams – Net Worth: $80 million (up $2.5 million)
  • 15. Akon – Net Worth: $80 million (up $2.5 million)
  • 16. Beastie Boys - $75 million each (no change)
  • 17. Ludacris – Net Worth: $75 million (up $5 million)
  • 18. Busta Rhymes – Net Worth: $65 million (up $5 million)
  • 19. Nelly – Net Worth: $60 million (no change)
  • 20. T.I. – Net Worth: $40 million (up $10 million)
  • 21. Big Boi – Net Worth: $40 million (no change)
  • 22. T-Pain – Net Worth: $35 million (up $5 million)
  • 23. Ice-T – Net Worth: $35 million (up $5 million)
  • 24. Drake – Net Worth: $30 million (up $5 million)
  • 25. Rick Ross – Net Worth: $28 million (up $3 million)
  • 26. Nicki Minaj – Net Worth $25 million (up $5 million)