Pages

Ludovick Aendelea Kusota Rumande

Ludovick
WAKATI Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare akiwa nje kwa dhamana mwezi mmoja sasa, mwenzake Ludovick Joseph(mwenye pingu) anaendelea kusota rumande kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana. Hayo yalibainika jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisumu, wakati kesi inayomkabili Lwakatare na mwenzake ilipotajwa mbele ya Hakimu Mkazi, Aloyce Katemana.

Wakili wa Serikali, Mkuu Ponsian Lukosi alidai mahakamani kwamba upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, wanaomba tarehe nyingine ya kutajwa na mshtakiwa Ludovick hajatimiza masharti ya dhamana.

Hakimu Katemana alikubali kuahirisha kesi hiyo hadi Julai 22 mwaka huu na aliamuru mshtakiwa aendelee kuwepo rumande hadi atakapopata wadhamini watakaotimiza masharti.

Lwakatare na Ludovick walikubaliwa dhamana baada ya kufutiwa mashitaka matatu ya ugaidi na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na kubakiwa na shitaka moja la kula njama ya kumdhuru kwa sumu Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mwananchi, Dennis Msacky.

Katemana baada ya kupitia hoja za kuomba dhamana zilizotolewa na wakili Peter Kibatala, alikubali kuwapa dhamana washtakiwa hao kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili wanaotoka katika taasisi zinazotambulika kisheria, ambao kila mmoja atasaini dhamana ya Sh milioni 10 pamoja na washitakiwa wenyewe.

Hakimu Katemana pia aliwataka washitakiwa hao kusalimisha hati zao za kusafiria mahakamani na kutotoka nje ya Dar es Salaam bila ya kuwa na kibali cha Mahakama.

Juni 10 mwaka huu, baada ya kukubaliwa dhamana, Lwakatare alidhaminiwa na kumwacha Ludovick akiendelea kusota rumande kwa kukosa wadhamini.

Hata hivyo uamuzi wa kuwapa dhamana washtakiwa hao ulikatiwa rufaa na upande wa Jamhuri katika Mahakama Kuu ya Tanzania wakipinga hatua hiyo.

Pia Jamhuri iliwasilisha maombi katika Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ikitaka ifanyie marejeo uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam wa kuyafuta mashtaka matatu ya ugaidi yaliyokuwa yakiwakabili washtakiwa hao. Uamuzi huo ulitolewa na Jaji Laurence Kaduri.

Washtakiwa hao walifikishwa kwa mara ya kwanza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Machi 18, mwaka huu wakikabiliwa na mashitaka hayo manne ya ugaidi, ambayo baadaye yalifutwa na Hakimu Emilius Mchauru baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), kudai hana nia ya kuendeleza mashitaka ya ugaidi dhidi yao.

Baada ya kufutiwa mashitaka hayo, washitakiwa hao walikamatwa tena na kufunguliwa mashitaka mengine yanayofanana na hayo mbele ya Hakimu Katemana ambayo pia yalifutwa na Jaji Kaduri. 
NA KULWA MZEE, DAR ES SALAAM
MTANZANIA

Eti Yupi Hayawani Zadi ya Wote?

Hayawani

SARS Nabs two Women with Drugs Worth Millions from Tanzanian Flight (Video)

The South African Revenue Services has made its biggest drug seizure at any border post after taking possession of Tik worth R42.6 million at OR Tambo International Airport.

ZEETOWN SOJAZ Ft FREDRIGO - CHINJACHINJA (Audio)

ZEETOWN SOJAZ Ft FREDRIGO - CHINJACHINJA

WANAFUNZI WALEVI WAKAMATWA KENYA

Polisi wa Kenya
Polisi wa Kenya wamewakamata zaidi ya wanafunzi elfu moja baada ya kupatikana wakiwa walevi mjini Nairobi wikendi hii.
Polisi waliendesha msako katika mabaa na vilabu vya burudani baada ya kupokea malalamishi kwamba watoto wa shule wamekua wakifurika kuburudika.

Kwa sasa wanafunzi wengi hawako shuleni baada ya waalimu wa Kenya kugoma wakitaka serikali kuwalipa marupurupu yao kutokana na ahadi iliyotolewa kwao na serikali mapema miaka ya themanini.

Mgomo huo umeingia wiki ya tatu sasa hali iliyofanya wanafunzi kukosa cha kufanya na hivyo kuanza kwenda kwenye vilabu vya burudani nyakati za usiku.
Katika kuzima tabia hii polisi mjini Nairobi mwishoni mwa wiki walifanya msako mkali katika mabaa na sehemu za burudani na kuwanasa watoto zaidi ya 1,000.

Polisi walianza kuwa na wasiwasi wakati visa vya unyang'anyi vilipoongezeka katika mji mikubwa nchini Kenya. Wasiwasi ulizidi wakati walalamikaji walipokuwa wakidai kuwa wanaowapora na kuwapiga kabari ni kundi la watoto wanaodhaniwa kuwa ni wa shule.
Na mabaa na maeneo ya burudani ilipoanza kufurika polisi wakaona ni wakati muafaka wa kuchukua hatua.

Polisi sasa wametoa onyo kwa wenye mabaa nchini kenya kuheshimu sheria za biashara.
Baada ya wanafunzi kukosa kurudi nyumbani na wengine kuripotiwa kutoroka katika shule zao za mabweni wazazi walifurika katika vituo mbali mbali vya polisi kujua hatma ya watoto wao.
Lakini wengi wa wazazi waliokuwa wamefurika katika kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi walielekeza lawama zao kwa mgomo wa sasa wa walimu unaoendelea.

Polisi wanasema mtindo huu mpya wa watoto kutoroka madarasani na kuvamia maeneo ya burudani na ma baa sio tatizo la Nairobi pekee bali limeenea katika miji mingi ya Kenya.

Na kabla mambo hayaja haribika zaidi wazazi wanamtaka rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kuingilia kati mgomu huo wa walimu kuhusu mishahara na marupurupu mbali mbali
BBC

Steve Kafire feat. Ben Pol - Everytime [Official Video] HD

Mkasi TV with Kajala (Msimu Mpya)

Richest Rappers In The World 2013 -List

diddy
  • 1. Diddy – Net Worth: $580 million (up $80 million)
  • 2. Jay-Z – Net Worth: $500 million (up $25 million)
  • 3. Dr. Dre – Net Worth: $360 million (up $100 million)
  • 4. Master P – Net Worth: $350 million (no change)
  • 5. 50 Cent – Net Worth: $260 million (up $10 million)
  • 6. Birdman – Net Worth: $150 million (up $35 million)
  • 7. Eminem – Net Worth: $140 million (up $20 million)
  • 8. Snoop Dogg – Net Worth: $130 million (up $10 million)
  • 9. Ice Cube – Net Worth: $120 million (up $20 million)
  • 10. Lil Wayne – Net Worth: $110 million (up $15 million)
  • 11. Kanye West – Net Worth: $100 million (up $10 million)
  • 12. LL Cool J – Net Worth: $85 million (up $5 million)
  • 13. Timbaland – Net Worth: $80 million (up $5 million)
  • 14. Pharrell Williams – Net Worth: $80 million (up $2.5 million)
  • 15. Akon – Net Worth: $80 million (up $2.5 million)
  • 16. Beastie Boys - $75 million each (no change)
  • 17. Ludacris – Net Worth: $75 million (up $5 million)
  • 18. Busta Rhymes – Net Worth: $65 million (up $5 million)
  • 19. Nelly – Net Worth: $60 million (no change)
  • 20. T.I. – Net Worth: $40 million (up $10 million)
  • 21. Big Boi – Net Worth: $40 million (no change)
  • 22. T-Pain – Net Worth: $35 million (up $5 million)
  • 23. Ice-T – Net Worth: $35 million (up $5 million)
  • 24. Drake – Net Worth: $30 million (up $5 million)
  • 25. Rick Ross – Net Worth: $28 million (up $3 million)
  • 26. Nicki Minaj – Net Worth $25 million (up $5 million)

WACHEZAJI WENYE IMANI YA DINI YA KIISLAM WANAVYOBADILI UTAMADUNI WA LIGI KUU YA ENGLAND

 Spain Nayim
Wakati Premier League ilipoanza mwaka 1992, kulikuwepo na mchezaji mmoja tu aliyekuwa na imani ya dini kiislam, kiungo wa Tottenham anayetoka Spain Nayim. Ligi hiyo ya juu kabisa nchini England sasa ina zaidi ya wachezaji 40 wanaofuata imani ya dini ya kiislam - na wachezaji wanaleta mabadiliko makubwa kwenye mchezo wa soka nchini England.

Tarehe 5 February, 2012, Newcastle United ilicheza na Aston Villa kwenye uwanja wa St James' Park na baada ya dakika 30 za mchezo huo, Demba Ba alifunga bao kwa upande wa Newcastle. Akakimbia mpaka kwenye kibendera na kuungana na msenegali mwenzie Cisse. Wachezaji hao wawili wenye imani kali ya dini yao walishangilia kwa kusujudu.

Kukua kwa idadi ya wachezaji wa kiislam inazidi kukua kila siku baada nguvu ya soka kuongezeka kwenye anga ya kimataifa.

Maskauti wa kusaka vipaji wamesambaa dunia nzima kusaka vipaji vipya na premier league imekuwa kivutio zaidi kutokana na umaarufu na ukubwa wa mishahara ya wachezaji.

Vijana wadogo kutoka maeneo ya Afrika Magharibi, kaskazini na hata au kwenye maeneo wanayoishi watu wenye kipato cha chini kwenye viunga vya mji wa Paris - vijana hawa sasa wamekuwa mastaa wakubwa.

Wanaweza wakawa matajiri na maarufu kwa kwa sasa wakichezea kwenye vilabu vya kiingereza, lakini wengi wao bado hawajasahau mizizi ya utamaduni wao, kitu ambacho kinawaongoza na kuwaunganisha pamoja majaribu ya kidunia - imani yao ya kiislamu.

Wakati mchezaji wa ubora wa Demba Ba, ambaye aliondoka Newcastle mwaka uliopita na kujiunga na Chelsea, anaposema kwamba ni mtu anayefuata kwa umakini imani ya dini yake, baadhi wanaweza kutoa hoja kama vilabu vinaweza kusikiliza matakwa yao.

Wachezaji wa kiislam wanapewa mahitaji yao muhimu yanayoendana na imani ya dini yao - kuanzia chakula, mavazi, na pia huwa wanapewa muda wa kufanya ibada zao - hii ni zaidi kwa wanasoka ambao bado wanakuwa wanaishi kwenye zile academy.

Mpaka hivi karibuni, wachezaji wote wa Premier League ambao wanashinda zawadi ya mchezaji bora wa mechi wamekuwa wakizawadia chupa ya shampeni.

Lakini kwa wachezaji wa kiislam, vilevi vimekatwaza. Hivyo wakati kiungo wa Manchester City Yaya Toure alipokataa kiustaarabu kupokea zawadi wakati akifanyiwa mahojiano kwenye Television - akisema kwamba ni kinyume na imani ya dini yake, waratibu wa 'man of the match' ikabidi wakae na kufikiria cha kufanya.

Shampeni iliondolewa kama zawadi na badala yake sasa wachezaji wote wanaoshinda tuzo ya 'man of the match' watakuwa wanapokea kikombe kidogo.

Wakati Liverpool waliposhinda ubingwa wa kombe la ligi katika fainali ya mwaka 2012, wachezaji wa Liverpool wakiongozwa na nahodha wa Steven Gerrard waliondoa nguo za daktari wa timu, ambaye ni muislam, nje ya chumba cha kubadilishia nguo ili vilevi visije vikamwagikia nguo hizo.

Bado kunakuwepo na changamoto nyingi sana wakati waislamu wakiwa kwenye ibada ya mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Ni vipi wachezaji ambao hawali wala kunywa kwa masaa zaidi ya 12 wanaweza kucheza kwa kiwango cha juu kwa dakika 90?

Baadhi ya wachezaji wanasisitiza kutimiza ibada ya kufunga. Wengine wanaweza kufunga wakiwa kwenye mazoezi lakini sio kwenye mechi. Klabu zinajaribu kwa kila hali kufuata matakwa ya imani za wachezaji wao, lakini haiwezi kuwa kipindi rahisi kwa wachezaji au makocha.

Kiungo wa Arsenal Abou Diaby, 27, anasema: "Arsenal wangependa mie nisifunge, lakini wanaelewa kwamba huu ni wakati muhimu kwangu na wanajaribu kwa kila hali kufanya mambo yaende kiurahisi."

Ba, 28, anakiri kwamba amewahi kuwa na matatizo na makocha wake kuhusu suala la kufunga, lakini anasema amekuwa imara kusimamia imani yake.

"Mara zote nimekuwa na kocha ambaye amekuwa hana furaha na jambo la kufunga, nimekuwa nawaambia: 'Sikiliza, nitafunga. Ikiwa kiwango changu bado kipo vizuri nitaendelea kucheza; ikiwa jambo hilo ni baya basi usinipange kwenye timu, hivyo tu.'"

Mchezaji wa zamani wa Stoke Mamady Sidibe, 33, anasisitiza: "Kuna wachezaji ambao wanafunga na wanafanya vizuri uwanjani, na kunakuwa hamna tatizo lolote. Kwa upande wangu mie wakati wa Ramadhani siku ya mechi sifungi ili nisiwape visingizio watu wengine."

Bahati nzuri kwa pande zote mbili, Ramadhan mwaka huu inaisha August 7, siku 10 mbele kabla ya msimu mpya wa Premier League kuanza.
Mikataba ya udhamini nayo imekuwa ikileta utata. Timu ambazo zinatangaza biashara ya kamari na mikopo kwenye jezi zao zimekuwa zikiwaweka wachezaji wa kiislamu kwenye wakati mgumu, kwasababu wanakuwa wanatumika kutangaza biashara ambazo zinaenda kinyume na imani ya dini yao. Mwezi uliopita Papis Cisse alisema kwamba anapanga kuongea na Newcastle na wadhamini wao wapya, Wonga, kwa sababu alikuwa na mashaka kwamba imani yake haiwezi kumruhusu kuonekana akiwa amevaa jezi ya kuipromoti kampuni hiyo ya kamari, pia kukawa na tishio kwamba baadhi ya wachezaji wengine waislamu wa Newcatle kama vile Ben Arfa, Moussa Sissoko and Mapou Yanga-Mbiwa, wangefuata mkumbo, lakini kwa bahati nzuri hawa wengine jana walionekana wakifanya mazoezi huku wakiwa na vizibao vyenye nembo ya Wonga, ingawa bado Cisse ambaye hakuwepo mazoezini bado anaonekana kutokuwa tayari kuitangaza Wonga.

Golikipa wa Wigan Ali Al-Habsi ambaye anatajwa kuwa na asili ya Tanzania visiwani, lakini ni raia wa Oman, analizungumzia hili suala: "Sisi wachezaji na hivi vitu vinatoka kutoka klabu, hatuwezi kufanya chochote kuhusu suala la udhamini, tunachopaswa ni kufanya kazi yetu. Pia waislamu wote wanajua kwamba kamari ni dhambi - hili limeandikwa kwenye vitabu vitakatifu na pia mawaidha yanatolewa kila siku hivyo mie nikivaa shati ya Wonga haimanishi kwamba nimesema watumie."

Mashabiki pia wamekuwa wakijifunza vitu vingi kupitia wachezaji wa kiislamu.
Baadhi ya watoto wanaocheza kwenye viwanja vya bustani ya Newcastle wamekuwa wakionekana wakisujudu kila pale mchezaji mwenzao anapofunga goli.

Wanaweza wasiwe wanaelewa hasa nini kitendo hicho kinamaanisha, lakini ni ishara kwamba matendo ya wachezaji wa kiislamu yameanza kufahamika katika utamduni wa kiingereza.
BY AIDAN CHARLIE SEIF

2Pac Shakur The Lost Interview (Video)