Pages

MAPOKEZI YA MFALME MSWATI TANZANIA

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkaribisha Mfalme Mswati wa (ii) wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam leo Juni 26, 2013. Mfalme Mswati wa ii, ametua nchini kwa ajili ya
kuhudhuria Mkutano wa 'Smat Patnership' unaotarajia kuanza Juni 28 mwaka huu.
Mfalme Mswati ii,
Picha juu na chini ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na Mfalme Mswati ii, baada ya
kuwasili kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, leo Juni 26, 2013. Mfalme Mswati wa ii, ametua nchini kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa 'Smat Patnership' unaotarajia kuanza Juni 28 mwaka huu.
Mfalme Mswati ii,
Mohammed Gharib Bilal,
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika mazungumzo na Mfalme Mswati ii, mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, leo Juni 28, 2013 kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa 'Smat Patnership', unaotarajia kuanza Juni 28. Kushoto ni mke wa Mfalme Mswati.
Picha na OMR

Walinzi wa Obama Watia Fora, Mawasliano Yatazima Air Port Anytime..!!?!

Walinzi wa Obama
Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Julius Nyerere, Moses Malaki alisema jana kwamba ratiba za uwanjani
hapo zitabadilika kutokana na uzito wa ugeni huo.
Alisema kwa kawaida anapokuja kiongozi mkubwa wa
kitaifa katika uwanja huo hakuna ndege inayoruhusiwa kutua kwa kipindi cha nusu saa.
“Ni kweli hali hiyo pia itakuwapo
atakapokuja Rais Obama na safari
za ndege zitabadilika kulingana na ratiba ya kutua na kuondoka kwa
Rais huyo,” alisema Malaki.
Pia alisema ulinzi katika uwanja huo umeimarishwa
kwa mwezi mmoja sasa na tangu wakati huo,
maofisa wa usalama wa Marekani wamekuwa wakifika kwa nyakati mbalimbali.

“Sijawahi kuona ulinzi mkali kama huu, wamekuja
marais wengi hapa nchini lakini ulinzi huu ni wa kutisha, sijui
kwa sababu gani?” alisema Malaki.
Alisema awali, wakati maofisa hao walipoanza
kuwasili nchini hawakutambua ni mgeni
gani anayetarajia kufika lakini baadaye walipelekewa taarifa kuwa ni Rais
Obama na baadaye walitaarifiwa kuwa angetua saa 8.40 mchana, Julai Mosi.
Mkurugenzi huyo alisema Rais Obama atakuja
na ndege nne, moja itakayombeba,
ya pili kwa ajili ya mizigo, ya tatu itakuwa ya waandishi
wa habari na maofisa wa usalama na ya mwisho ni kwa ajili ya dharura ambayo itaegeshwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)
Malaki alisema maofisa wa Marekani wanaowasili nchini wamekuwa wakifanya shughuli mbalimbali za kuhakikisha kuwa hali ya usalama
inaimarishwa na kuwaacha wazawa wakifanya shughuli za kawaida.
“Ulinzi ni mkali mno, yapo masharti kadhaa
wanayoyataja kuwa yatatumika
kwa watu watakaoingia
eneo la uwanja au kuisogelea ndege ya Rais Obama. Jamaa
wameweka masharti magumu,” alisema.

Hasheem Thabeet Anapogeuka Mbogo Uwanjani, Cheki Video

MAPOKEZI ya TEVEZ Kama MFALME..!

Turi  
Carlos Tevez kushoto akiwasili jijini Turi
Carlos ,Tevez Carlos Tevez MSHAMBULIAJI Carlos Tevez amewasili Italia na kupata mapokezi makubwa kuelekea uhamisho wake wa Pauni Milioni 10 Juventus kutoka Manchester

Yanga Imesema Haitokwenda Kuchukuwa Zawadi Yake ya Ubingwa

Timu ya soka ya Yanga ya jijini Dar es Salaam imesema haitokwenda kuchukua zawadi yake ya ubingwa itakayotolewa julai tatu na kampuni ya simu ya Vodacom ambao ndiyo wadhamini wa ligi hiyo kwa madai ya kucheleweshewa.

Kama Uliikosa, Video ya Wema Sepetu Alivotoka Nduki EATV

Baada ya wema kukataa kujibu maswali yanayo muhusu diamond sam alimlazisha na wema akavua mic na kuondoka huku akimuacha meneger wake.

Rais wa Sri Lanka, Mahinda Rajapaksa Kuwasili Nchini kwa Ziara ya Kitaifa ya Siku Mbili.27, 2013

Sri Lanka Mahinda RajapaksaRais wa Sri Lanka Mahinda Rajapaksa
Rais wa Sri Lanka, Mhe. Mahinda Rajapaksa anatarajiwa kuwasili nchini tarehe 27 Juni, 2013 kwa ziara ya kitaifa ya siku mbili. Siku ya kwanza ya ziara yake, Mhe. Rajapaksa atafanya mazungumzo rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete na kushiriki Dhifa ya Kitaifa.

Tarehe 28 Juni 2013, Mhe. Rajapaksa atatembelea Hekalu la Kibudha lililopo Upanga, Jijini Dar es Salaam lililojengwa na Sri Lanka miaka 93 iliyopita.

Aidha, Mhe. Rajapaksa anatarajiwa kushiriki katika Jukwaa la Ushirikiano kwa Manufaa ya Wote (Global 2013 Smart Partnership Dialogue) utakaofanyika kuanzia tarehe 28 Juni hadi 01 Julai 2013. Ataondoka nchini tarehe 29 Juni 2013 kurejea nchini kwake.

IMETOLEWA NA: WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, DAR ES SALAAM
26 JUNI, 2013

Princely Trafficking (Saudi Drug Smuggling)

Documentary about Saudi Prince Nayef Al-Shaalan, who was sentenced in absentia to ten years in jail on charges of involvement in a cocaine-smuggling gang. The prince was one of ten people handed jail terms in connection with an operation which landed two tonnes of cocaine outside Paris in 1999. He was accused of using his diplomatic immunity to smuggle drugs to France on board a private jet. Was the grandson of founding Saudi monarch Abdulaziz, and son-in-law to the Saudi deputy defence minister, trying to covertly raise money for black operations?

Unaikumbuka Hii?

Unaikumbuka Hii

ULINZI WA OBAMA HAUJAWAHI TOKEA AFRICA

Wasp Class 
Dar es Salaam. Ulinzi katika ziara ya Obama ni wa hali ya juu kuliko ulinzi wa aliyewahi kupewa Rais yeyote wa Marekani kwa safari yake ya Afrika mwaka huu.
Tayari jeshi la nchi hiyo limewasili nchini, kuweka mambo sawa na kukagua maeneo yote ya karibu na sehemu atakazotembelea na kupita wakati wa ziara hiyo. Maaskari na majasusi zaidi ya 500 wapo Dar es Salaam kuhakikisha usalama huo na kuweka vifaa mbalimbali vya mawasiliano Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam.
Licha ya hilo, ziara yake kutakuwa na askari 1,687 wakataokuja kwa meli maalumu kubwa ya kivita iliyosheheni silaha mbalimbali, ikiwamo ndege sita za kivita aina ya AV-8B Harrier na helikopta za kivita 23, ambazo zinatarajiwa kupasua anga la Tanzania kuimarisha ulinzi.
Meli hiyo ya kisasa aina ya Wasp Class (Uk 1), pia itakuwa imebeba meli nyingine zaidi ya tano maalumu kwa kubeba vifaru, magari ya deraya, askari na vifaa vingine itatia nanga Bahari ya Hindi kuongeza nguvu iwapo lolote litatokea.
Taarifa inaonyesha italazimika kuwapo kwa meli tatu za aina hiyo wakati wa ziara yake nchini Senegal, Tanzania na Afrika Kusini kwani mwendo wake siyo kasi hivyo kulazimika kutumia zote hizo kwa ajili hiyo.
Meli hiyo kubwa imeundwa kuwezesha askari wa Marekani kuingia kwa urahisi eneo la vita kwa brigedi nzima, kwani wanaweza kutumia aina zote za vita majini, angani na ardhini. Ni meli aina hiyo zilizotumika vita vya Marekani na Iraq. Licha ya mitambo ya kivita, ina hospitali kubwa yenye uwezo wa kulaza zaidi ya wagonjwa ya 600.