Pages

Mjengo Anaoishi Babu wa Loliondo kwa Sasa

Babu wa Loliondo Babu wa Loliondo Babu wa Loliondo Babu wa Loliondo
Hii ni nyumba aliyokuwa anaishi Babu Ambi kabla Dozi ya Kikombe haijachanganya

Simba vs Yanga Jumamosi, Soma Viingilio

Simba na Yanga Kiingilio cha chini kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Yanga itakayochezwa Jumamosi (Mei 18 mwaka huu) kitakuwa sh. 5,000. Kiingilio hicho kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648.
Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu kiingilio ni sh. 7,000, viti vya rangi ya chungwa itakuwa sh. 10,000, VIP C kiingilio ni sh. 15,000, VIP B itakuwa sh. 20,000 wakati VIP A yenye viti 748 tu tiketi moja itapatikana kwa sh. 30,000.

Tiketi zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mchezo huo utakaoanza saa 10 kamili jioni.
Mwamuzi wa mechi hiyo atakuwa Martin Saanya kutoka Morogoro ambapo atasaidiwa na Samuel Mpenzu wa Arusha, na Jesse Erasmo kutoka Morogoro. Mwamuzi wa akiba ni Hashim Abdallah wa Dar es Salaam.
Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya wakati mtathmini wa waamuzi (referees assessor) ni Leslie Liunda.

GELLY WA RHYMES APIGWA ROBA NA VIBAKA

Gelly wa Rhymes
Star wa single ya mama ntilie Gelly wa Rhymes usiku wa jana haukuwa mzuri kwake baada ya kuvamiwa na vibaka akiwa njiani kuelekea club bilcanas kwenda kutoa support kwa Hemed aliyekuwa akizindua wimbo wake mpya wa rest of my life.
Taarifa zinasema kuwa vibaka hao walimkaba na kumsababishia majeraha maeneo ya usoni na hawakumfanyia madhara makubwa na hilo lilipelekea kushindwa kufika kwenye show ya mshikaji wake Hemed,na taarifa hii ni kwa mujibu wa mc wa show hiyo iliyofanyika usiku wa juzi club bilcanas ambapo kabla haijafika zamu ya Gelly kuperfome mc alitoa taalifa hizo,TEENTZ inaendelea kufuatilia kujua undani wa mkasa huo.

BBall Kitaa Day One At Gymkhana Dar Es Salaam Tanzania

BREAKING NEWS: ZAIDI YA WANAFUNZI 30 WA SHULE YA SECONDARI MANZESE WANAANGUKA HOVYO NA KUZIMIA

SECONDARI MANZESE
Wanafunzi wa shule ya secondari manzese zaidi ya 30 muda huu wanaanguka hovyo hovyo na kusema a mane no yasiyoeleweka kutokana na kinachohisiwa kuna nguvu za Giza zimetanda shuleni hapo huku wakijibamiza kwenye miti:
MANZESE SECONDARI
Mmoja wa wanafunzi wa shule ya Sekondari Manzese aliyeanguka na kuweweseka.Mpaka sasa haijafahamika chanzo cha wanafunzi wa shule hiyo kukimbia ovyo,kuanguka na kuweweseka.
Picha:Zainab Chondo wa ITV

SIASA na MAPENZI, Angalia Tweets za Diva Zinazomuhusu Zitto Kabwe, Dharau tupu

Diva

Madai ya Flora Lyimo Kubakwa na Mbunge

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaSifael Paul na Erick Evarist
BINTI mrembo aitwaye Flora Bahati Lyimo anamtuhumu mbunge mmoja ‘mtata’ wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaloongozwa na Spika Anne Makinda (jina tunalo) kuwa amembaka, Uwazi lina kisa cha aibu ya karne.

Flora Bahati Lyimo.
Katika uchunguzi wake, hivi karibuni gazeti hili lilielezwa kuwa kuna habari ya kashfa nzito inayomtafuna mbunge huyo anayetokea Kanda ya Kaskazini lakini haikufafanua kwamba inahusu nini.

VYANZO
Baada ya kutulia na kupekua kwenye vyanzo vyake, Uwazi lilibaini kuwa kashfa inayomlenga mheshimiwa huyo ni ya ubakaji na tayari imefikishwa mahakamani huko London nchini Uingereza.
Habari hiyo ilielezwa ‘kijuujuu’ hivyo gazeti hili likamtafuta Flora ambaye ni Mtanzania anayetokea mkoani Kilimanjaro ambaye anaishi katika Jiji la London kikazi.

MAZITO
Alipopatikana Flora alibanwa kisawasawa ndipo akaibua mazito huku akieleza tukio zima lilivyofanyika kwa data na vielelezo vya kila aina ikiwemo barua ya Mahakama ya Crown ya London.
“Ni kweli mheshimiwa … (anamtaja jina) alinibaka Agosti, mwaka jana. Yeye na makada wenzake wa chama chake walikuja hapa London kwa ziara ya kichama na kwa kuwa mimi sina chama nilikwenda kuhudhuria mkutano wao kwa kuwa nina mtandao wangu (blog) hivyo nilitaka kupata habari za kuingiza kwa sababu ni za watu wa nyumbani (Tanzania).
Spika Anne Makinda. MAZOEA YAANZA
Akiendelea kuweka wazi kisa hicho, Flora anasema: “Nikiwa kwenye mkutano….(jina la mbunge) alinifuata akaniuliza nimeandika watu wangapi waliohudhuria mkutano huo, nikamjibu 50 akaniambia niongeze idadi hiyo ili ionekane mkutano ulikuwa na watu (Watanzania waishio Uingereza) wengi.
“Hapo ndipo alipoanza kunizoea. Alitaka kunipa kadi ya...

Cat Knocks On Door At Machine Gun Rate - Gatto che Bussa la Porta

Muslim Footballer Franck Ribery Runs The Length of The Pitch to Avoid Beer During Title Celebrations!! (Video)

Muslim Franck Ribéry was left “p****d off” after Bayern Munich teammates ignored pleas to soak him with beer during the Bundesliga champions’ title celebrations.
Former Manchester City defender Jerome Boateng proved to be the Frenchman’s bête noire when he poured a large glass of Bavarian beer over Ribéry. Ribéry said after the celebrations: “I won’t talk to Boateng again, he knows that I’m Muslim. I’m p*** off.”
A notorious prankster, Ribéry’s best act involved pouring water on former Bayern goalkeeper Oliver Kahn from the rooftop.
Manuel Neuer also got carried away when he threw beer on an unassuming girl who had laid out the celebratory beverages. The Germany goalkeeper wheeled away in celebration.
Bayern are on course for a unique debut, as they face Borussia Dortmund in the Champions League final in London next week before taking on Stuttgart in the DFB-Pokal final in June.

Zitto Kabwe Amempa Afande Sele Dollar 1,000 Kwaajili ya Kurekodi Video!!

Mfalme wa Rhymes Selemani Msindi a.k.a Afande SeleMfalme wa Rhymes Selemani Msindi a.k.a Afande Sele wakati alipo hudhuria kwenye uzinduzi wa msimu mpa wa Clouds fm ulioenda sawa na semina kuhamasisha vijana kujitambua kwa kutumia fursa za kiuchumi zilizopo nchini, Lakini pia kulikua na uzinduzi wa kampeni kubwa ya kupinga Uharamia wa kazi za kisanii / Anti Piracy, Afande alibahatika kupata ahadi ya dola elfu moja kutoka mbunge wa kigoma kaskazini Zito Kabwe, mh zito alisema anatoa kiasi hicho cha pesa ili afande aka shoot musiq video ya ngoma yake aliyoitoa hivi karibuni inaitwa "Dini tumeletewa" Mbunge Zito Kabwe amesema kutokana na ubora wa ngoma hiyo anatoa mchango huo ili ikafanyike video bora itakayodumu muda mrefu na kuwafikia watu wengi, ili ikawa elimishe watanzania na vijana kwa ujumla umuhimu wa kupendana na kuacha kubaguana katika misingi ya dini.
Ngoma hii "Dini tumeletewa" imekuja baada Kutokea mauaji ya viongozi wa dini pamoja na shambulizi la bomu lililofanywa hivi karibuni katika kanisa moja huko Arusha na kuua watu kadhaa. zaidi Sikiliza sauti Afande akifunguka kuhusu ishu hiyo:

SIKILIZA Dini tumeletewa by Afande Sele