Pages

Polisi wambana Lwakatare. -Dk. Slaa: Video ya Lwakatare ni Feki


Lwakatare alikamatwa juzi makao makuu ya chama hicho na kupelekwa katika Makao Makuu ya Polisi kwa mahojiano.
Polisi wamezidi kumbana Mkuu wa Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare baada ya kupekua nyumbani kwake kwa siku ya pili mfululizo.

Lwakatare, ambaye ni mbunge wa zamani wa Jimbo la Bukoba Mjini kupitia CUF, alikamatwa juzi mchana kwa kutuhumiwa kwa kufanya uchochezi wa uvunjifu wa amani baada ya kunaswa kwenye picha ya video iliyorushwa kwenye mitandao ya kijamii

Upekuzi wa pili
Nyaronyo Kicheere, ambaye ni Mwanasheria wa Lwakatare, aliliambia gazeti hili jana kuwa mteja wake, ambaye anashikiliwa na polisi hao, alipelekwa nyumbani kwake Kimara-King’ong’o jijini Dar es Salaam kwa ajili ya upekuzi huo.

Ilikuwa mara ya pili kwa Lwakatare kupekuliwa kwani mara ya kwanza ilikuwa juzi jioni baada ya kuhojiwa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi. Lwakatare, ambaye alitolewa Kituo cha Kati cha Polisi, alipelekwa jana kwa msafara wa magari mawili ya polisi chini ya ulinzi mkali.

Nyaronyo alisema kuwa msafara huo uliondoka saa 10.00 jioni kwa ajili ya safari hiyo ya Kimara wakitokea katikati ya Jiji la Dar es Salaam kilipo Kituo cha Kati cha Polisi. Alisema kuwa uamuzi huo ulifikiwa baada ya...

Rais Kikwete Amezindua Jengo la Kitivo cha Sayansi Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro.

 Morogoro
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua pazia kuzindua rasmi jengo la Kitivo cha Sayansi la Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro leo Machi 14, 2013 mjini Morogoro. Kushoto kwake ni Mkuu wa Chuo hicho Mama Mwantumu Malale.
Jengo la Kitivo cha Sayansi Chuo Kikuu cha Kiislamu
 Juma Mikidadi Mtupa
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo juu ya ujenzi wa jengo la kitivo cha Teknohama toka kwa Bw. Hamza Mustafa Njozi kabla ya kuzindua rasmi jengo la Kitivo cha Sayansi la Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro leo Machi 14, 2013 mjini Morogoro. Kushoto kwake ni Mkuu wa..

Balozi Apokonywa Ubalozi Baada ya Kutembea Uchi

Afrika Kusini nchini China,
Lassy Chiwayo ambae ni balozi wa Afrika Kusini nchini China, amerudishwa nyumbani baada ya mkataba wake kukatishwa kutokana na kukumbwa na kile kinachodaiwa kuwa matatizo ya kiafya.
Gazeti la Daily Teleghraph limeripoti kwamba moja kati ya sababu kubwa ni tatizo kwenye akili yake ambapo inadaiwa balozi huyo ilifikia mpaka kutembea mtaani bila nguo.

Magazeti mbalimbali yameripoti kwamba balozi huyo alikua na mtindo wa kupotea nyumbani huko China alikokua anaishi, alikua anapotea kwa siku kadhaa alafu baadae anakuja kukutwa akiwa mtupu bila nguo.

Lassy mwenye umri wa miaka 44 akiwa ni mmoja wa watu wa karibu ambao waliwahi kufungwa gereza moja na rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela, amekanusha taarifa zake za kuwa na matatizo ya akili pamoja na kutembea uchi, akisema hayo yote ni mambo mapya kuyasikia.

Imeripotiwa kwamba Lassy ambae ni baba wa watoto watatu amekumbwa na mfululizo wa matukio hivi karibuni ambapo la mwisho linalokumbukwa ni moto kulipuka nyumbani kwake na kuteketeza mali kama gari la kifahari la Porsche, quad bike na mali nyingine

Gari la Zima Moto Ilipogeuzwa Gari la Matangazo na Vipaza Sauti Juu!!

Zima Moto
Zima Moto
Zima Moto
SASA KAZI IMEANZA TUOMBE MOTO USITOKEE MAANA SIJUI ITAKUWAJE JIBU MNALO WENYEWE

Chiddi Beenz Ametiririka Kuhusiana na Kutoboa Pua

Chiddi Beenz

Story ya Yule Mwanamke Aliye Chinjwa Kama Kuku na Mpenzi Wake Huko Kahama

Jessica Elialinga
VILIO vilitawala Kata ya Nyahanga wilayani hapa wakati wa kuuaga mwili wa binti Jessica Elialinga (19) aliyeuawa kinyama kwa kuchinjwa kama kuku na mpenzi wake, Musa Petro (27) mkazi wa Shunu kwa sababu zinazodaiwa ni wivu wa kimapenzi.

Jessica Elialinga baada ya kuchinjwa.
Tukio hilo lililoibua simanzi kubwa kutokana na marehemu kuhitimu Kidato cha Nne katika Shule ya Sekondari ya Kata ya Nyihogo, Kahama mwaka jana, lilijiri saa 12:45 Februari 6, mwaka huu.

Kitendo hicho kilifanyika katika banda la mbuzi lililopo nyumbani kwa kijana huyo ambaye baada ya kutekeleza mauaji na yeye alifanya jaribio la kutaka kujitoa roho kwa kisu.

Akisimulia juu ya tukio hilo, rafiki wa karibu wa Musa ambaye aliomba hifadhi ya jina lake kwa ajili ya usalama, alisema wiki moja kabla ya tukio hilo, mtuhumiwa huyo alikuwa akiwatangazia jamaa zake kwamba ana dhamira ya kumuua binti huyo kufuatia kubaini kuwa anamsaliti kimapenzi.

Musa Petro
“Unajua Musa anafanya kazi ya kuchuna ngozi za wanyama machinjio ya Wilaya ya Kahama, alitutangazia dhamira yake hiyo, lakini tulichukulia kauli yake kama mzaha.
“Alisema anataka kufanya hivyo kwa sababu amekuwa akitumia gharama kubwa kwa mpenzi wake huyo tangu walipoanza uhusiano, msichana akiwa kidato cha pili, lakini anatoka kimapenzi na mwanaume mwingine,” alisema rafiki huyo.

Hata hivyo, inadaiwa baada ya mtafaruku wa usaliti, wawili hao walipatana na kuendelea na mapenzi, lakini baada ya mwanafunzi huyo kuhitimu kidato cha nne alibadilika ambapo mwanaume alisikia kuwa tayari ana mwanaume mwingine kutoka jijini Mwanza ambaye walikubaliana kufunga pingu za maisha baada ya kumaliza masomo.
Muuaji Musa Petro, Kushoto
Muuaji Musa Petro.
Jessica Elialinga enzi za uhai wake.
Inadaiwa siku chache kabla ya mauaji hayo, rafiki mmoja wa karibu wa mtuhumiwa alikutana na marehemu njiani na kumsimamisha kwa lengo la kumweleza kauli zenye kutishia maisha yake anazozitoa mpenzi wake, lakini binti huyo hakusimama kumsikiliza.

Baada ya Musa kudaiwa kufaulu kumchinja mpenzi wake huyo na yeye kujikata koromeo na kuanguka akiwa ameishiwa nguvu, kijana mchunga mbuzi ambaye wengi katika eneo hilo humchukulia kama kaka yake Jessica, ndiye aliyekuwa wa kwanza kumshuhudia Musa akiwa katika hali hiyo.

Alipomhoji kulikoni, hakupata jibu zaidi ya kushuhudia jitihada za mtuhumiwa huyo kufungua mlango wa chumbani mwake zikishindikana.
Kijana huyo alitoa taarifa kwa watu ambao walifika na kumchukua Musa na kumkimbiza hospitali ya wilaya kuokoa uhai wake.

Watu waliobaki nyumbani walifuatilia michirizi ya damu hadi kwenye zizi la mbuzi ambako walimkuta Jessica ameshafariki dunia baada ya kuchinjwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Everest Mangala alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo alisema mtuhumiwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani Kahama katika Hospitali ya wilaya hiyo anakoendelea kupatiwa matibabu.

Uchangiaji wa Ujenzi, Maktaba ya Jamii ktk Kijiji cha Lugalo Mkoani Iringa

MAKTABA YA JAMII KATIKA KIJIJI CHA LUGALO MKOA WA IRINGATaasisi isiyokuwa ya kiserikali ina mpango wa kujenga Maktaba ya Jamii katika kijiji cha Lugalo mkoani Iringa.

TUWAFIKIE TANZANIA ORGANISATION Ni asasi isiyokua ya Kiserikali inayojiendesha sio kwa malengo ya kupata faida tunajishughulisha na uhamasishaji wa maendeleo ya elimu vijijini kuhakikisha watoto na vijana wanapata elimu bora ili waweze kuwa wabunifu na kujitegemea.

Unaweza kutuunga mkono kwa kuchangia kuanzia 1,000/= na kuendelea kuwezesha ujenzi wa maktaba ya jamii katika kijiji cha Lugalo.kwa kufanya hivyo utakua umewasidia wanafunzi na jamiii kwa ujumla ya lugalo na vijiji vya jirani kuweza kupata taarifa mbalimbali na kuelimika.Tunaamini matatizo yanayoikabili jamii yetu sisi wenyewe tunatakiwa tuwe wa kwanza kuyatatua kabla ya watu wengine kutoka nje kuja kufanya badala yetu.Mabadiliko ni mimi na wewe pamoja tunaweza.

Tutakua tunatoa taarifa ya fedha iliyopatikana kupitia hili kundi letu.Unaweza changia kupitia MPesa,Tigo Pesa au Account no yetu CRDB kama inavyoonekana kwenye picha. Pia tutakua tukiwajulisha kiasi kilichopatikana na waliochangia kupitia page yetu facebook,website yetu na kwenye wall yangu
MPESA 0754 981 629 TIGO PESA 0712 852 665 CRDB BANK A/C No. 0150450143000

For any enquiries, questions, ideas and any request of engagement, please fill free to contact us and share with us. We are always available. Please visit www.tuwafikie.org

Chadema Walitaka Jeshi la Polisi Kufanya Kazi Bila Shinikizo

Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimesema kilikuwa na taarifa za mapema juu ya uwepo wa mkakati unaoratibiwa na kufanikishwa na maafisa wa ngazi za juu wa usalama wa taifa wa kukihusisha chama hicho na njama za kumdhuru mwenyekiti wa jukwa la wahariri Absalom Kibanda ili kukidhofisha chama hicho kisiasa.

Ney wa Mitego ft Diamond Platinumz - Muziki Gani (Audio)

Dogo Janjaro in South Africa, Cape Town

The promo video of Janjaro's tour to Cape Town/South Africa