Pages

Lil Wayne's Deposition [Extended Version] Must See!!

Moto wa Ubungo Leo Asubhi


 

Jitihada za Makampuni Mbalimbali ya Zima Moto mchana wa leo zimeshindwa kuzima Moto na kuokoa mali zenye thamani ya Zaidi ya Shilingi Bilioni 30, mali ya Kampuni ya kusambaza Vifaa vya Ujenzi na Usafirishaji ya SUNDA LIMITED, iliyopo katika eneo la UBUNGO jijini Dar es Salaam.
Chanzo cha Habari cha CLOUDS FM kimeeleza kuwa Moto huo ulianza muda wa saa tano Asubuhi


Magari ya vikosi vya zimamoto yakimwaga maji ili kuzima moto huo.

Vifaa vilivyookolewa kutoka ndani ya ghara hilo.

Jitihada za kuzima moto huo zikiendelea.......

Moto huo ukizidi kusambaa...

Afande Sele - Sukari na Chai

Afande Sele - Sukari na Chai

Something From Nothing: Art Of Rap ft. Krs-One & Eminem on Freestyling

Scenes from Something From Nothing: Art Of Rap featuring KRS-One and Eminem freestyling and explaining how to freestyle.

Bibi wa Miaka 68 Auwawa Akitaka Kufunga Ndoa na Kijana wa Miaka 28

Jette Jacobs 
 Polisi wa Afrika Kusini bado wanaendelea kuchunguza tukio la kutisha linalodaiwa kufanywa na kijana wa Kinigeria mwenye umri wa miaka 28 ambae anatuhumiwa kumuua bibi wa kizungu mwenye umri wa miaka 67 huko Johannesburg.
Bibi kizee Jette Jacobs ambae ni raia wa Australia alisafiri mpaka Johannesburg kwa lengo la kufunga ndoa na mwanaume anayempenda lakini siku mbili baada ya kukutana na mwanaume huyo, bibi huyo amekutwa amefariki kwenye mazingira ya kutatanisha kwenye jiji hilo lililo kwenye list ya majiji hatari kwa uhalifu duniani.

Jette alipokwenda Johannesburg lengo lake lilikua ni kukutana kwa mara ya kwanza na mwanaume ambae wamekua wakiwasiliana kupitia mtandao wa kijamii ambao hukutanisha watu wenye hitaji la kupata mpenzi/mke/mume ambapo aliingia kwenye mapenzi na Jesse Orowo Omokoh asiemjua miaka mitatu iliyopita.
Mwili wa bibi huyu mwenye watoto sita ulikutwa kwenye guest house miezi miwili baada ya kuwasili Afrika Kusini ambapo kwa muda waliofahamiana online, Jette alikua ameshatuma kiasi cha dola za Kimarekani laki mbili kwa Omokoh na mwanaume mwingine aitwae Isaac.

Pamoja na kupewa onyo na familia yake, Jette hakusikia chochote bali alitaka kwenda South Africa toka november 2012 ili akafunge ndoa na huyu mwanaume wa Kinigeria, kwenye guest house mwili wake ulipokutwa kuna baadhi ya vitu alivyokuwa navyo havijaonekana kama vile mikufu na pesa.
Binti wa mwisho wa bibi huyu amesema mwanaume huyu wa Nigeria alitaka kuhamia Australia ili akaishi na Bibi huyu lakini bibi aligoma na kumwambia anataka kwenda kuishi nae Nigeria.

Aliyetoa Ushahidi Dhidi ya Mengi Atishiwa Maisha

Erick Kabendera
-NDUGU WAOMBA ULINZI!
Stori: Mwandishi Wetu
HUWEZI kuamini lakini ukweli ni kwamba Erick Kabendera ambaye ni mwandishi wa habari wa hapa nchini ana wasiwasi na maisha yake baada ya kwenda kutoa ushahidi uliomwangamiza mfanyabiashara maarufu Reginald Mengi ambaye sasa anatakiwa kumlipa Sarah Hermitage, raia wa Uingereza aliyekuwa amemshitaki mahakamani.
Sarah alimshitaki Mengi akidai kukashifiwa na magazeti yake na katika kesi hiyo iliyokuwa ikisikilizwa Mahakama Kuu ya London, Uingereza, jaji alimhukumu kumlipa mama huyo paundi za Uingereza milioni 1.2 (ambazo ni sawa na Shilingi Bilioni 2.9 za Kitanzania) baada ya hapo vituko vya kuisumbua familia ya Kabendera mkoani Kagera vikaanza.
Kwa mujibu wa taarifa ya Chama cha Waandishi wa Habari za Uchunguzi kiitwacho Forum for African Investigative Reporters (FAIR), familia ya Kabendera, imekuwa ikisumbuliwa na maofisa wa..

Uchaguzi Kenya: Uhuru Kenyatta Aongoza,Watu 22 Wauawa

Uchaguzi Kenya
Kura zikihesabiwa kwenye kituo kilichopo Viwanja vya Kibera Social, jijini Nairobi baada ya wananchi wa Kenya kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo jana. Picha na AFP

Matokeo ya awali ya uchaguzi mkuu nchini Kenya yanaonyesha kuwa Uhuru Kenyatta, mtoto wa Rais wa Kwanza wa Kenya, Mzee Jomo Kenyatta anaongoza, huku akifuatiwa kwa karibu na aliyekuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Raila Odinga.

Kama alivyo Uhuru, Raila pia ni mtoto wa mmoja wa waasisi wa taifa la Kenya, ambaye alikuwa Makamu wa Mzee Kenyatta, Jaramong Oginga Odinga.

Hadi majira haya ya saa 6.45 usiku wa kuamkia leo, Uhuru ambaye ni mgombea wa TNA alikuwa amepata kura 744,648 sawa na asilimia 56.1 wakati Raila ambaye ni mgombea wa ODM alikuwa akifuatia kwa kupata kura 527, 780 sawa na asilimia 39.7.
Matokeo hayo ni kutoka katika vituo zaidi ya 5000 kati ya...

Australian Miners Consider Lawsuit After Getting Fired Over ‘Harlem Shake’ Video

The ‘Harlem Shake’ miners plan a lawsuit seeking reinstatement after they were sacked by Barminco and banned from working in all mining sites owned by the company around the world.
Fifteen people getting sacked by an Australian mining company Barminco over “Harlem Shake” video are reportedly mulling a lawsuit seeking reinstatement. Words are, only half of them appeared in the video and the others simply watched their friends doing the convulsive dance to the Baauer goofy track without taking part in it.

Tangazo. Hii Sio ya Kukosa!!!

SHEREHE ZA MIAKA 3 YA VIJIMAMBO NA TAMASHA LA UTAMADUNI WA KISWAHILI MAREKANI

Vijimambo Blog ya Vijimambo ikishirikiana na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Washington, DC, nchini Marekani na Jumuiya ya Watanzania waishio Washington DC, Maryland na Virginia wanapanga kusheherekea miaka 3 ya Vijimambo kwa kuendeleza Lugha na Utamaduni wa Kiswahili. Madhumuni ya hili tamasha ni kuendeleza lugha na utamaduni wa Kiswahili hapa Marekani ili watoto wa Watanzania wanaoishi huku Marekani waweze kuendeleza matumizi ya lugha hii na utamaduni wake kizazi hadi kizazi.

Sherehe zitafanyika
July 6, 2013 hapa DMV kwenye Hall la Hampton Conference Center uliopo
207 w Hampton Pl,
Capitol Height, MD

Mambo mengi yatakuwepo, Vikundi mbalimbali vya utamaduni, vyakula vya Kitanzania, Wasanii kutoka nyumbani na hapa Marekani yote ni kudumisha utamaduni wa kiswahili Marekani ya Kaskazini

TEGA SIKIO HABARI ZAIDI ZITAFUATA
-------------------------------------------------------
kwa wajasiliamali ambao wangepenga kudhamini na kuijipatia meza ya kutangaza bidhaa au shughuli wazifanyazo tafadhali wasiliana 301 613 5165 Asante
Vijimambo

President Obama Makes a Personnel Announcement

President Obama nominates Ernest Moniz as the next Secretary of Energy, Gina McCarthy as Administrator of the Environmental Protection Agency, and Sylvia Mathews Burwell as Director of the Office of Management and Budget. March 4, 2013.