Pages

Rick Ross Aongezewa Ulinzi Na Polisi

Rick Ross Aongezewa Ulinzi Na Polisi
 Rapper kutoka Label ya Maybach Music Group [MMG], Rick Ross ameongezewa ulinzi na jeshi la polisi la New Yorkbaada ya rapper huyo kupata vitisho vya kuuwawa tena kutoka kwa watu wasiojulikana.
Kwa mujibu wa TMZ, rapper Rozay huyo atakuwa na ulinzi wa Masaa 24 kutoka kwa polisi hao wa NY.
Ross anaetamba kwa sasa na album yake ya GOD FORGIVES I DONT na pia mixtape BLACK BAR MITZVAH yupo katika maandalizi ya album yake ya 4 inayokwenda kwa jina la MASTERMIND

Sakata la Binti Kiziwi Kukamatwa na Madawa ya Kulevya China

 Jacqueline Patric 
SIKU chache baada ya mrembo wa video ya wimbo wa Binti Kiziwi wa Ally Mohammed ‘Z. Anto’, Sandra Khan ‘Binti Kiziwi’ kutiwa nguvuni kwa tuhuma za kunaswa na madawa ya kulevya nchini China, Jacqueline Patrick ‘Jack’ ambaye ni modo kiwango Bongo, amesema anajua kila kitu kuhusu tukio la kukamatwa kwake, Amani linakuhabarisha.
Akizungumza na mwandishi wetu katika mahojiano maalum juzi, jijini Dar es Salaam kuhusu uvumi ulioenea kwamba yeye ndiye aliyemchoma Binti Kiziwi kwa polisi na kusababisha kudakwa kwake, alisema tuhuma hizo si za kweli bali ni mbinu za watu wanaotaka kumchafua.

“Ngoja nikuambie ukweli, siku Binti Kiziwi anakamatwa mimi nilikuwepo uwanja wa ndege na niliona kila kitu. Unajua mwanzo alianza kulalamikia tumbo kumsumbua ghafla, akachukuliwa na kupelekwa kupewa huduma ya kwanza.
“Akiwa huko kwenye matibabu alipigwa ultrasound ndipo alipogundulika kuwa kumbe alikuwa na vitu tumboni.Katika hali kama hiyo unadhani ni mjinga gani anaweza kujitokeza na kudai huyo ni ndugu yake?”

“Mimi sijui chochote lakini nilichojua yule ni Binti Kiziwi na ni Mtanzania mwenzangu, tena staa kama mimi kwa hiyo sikuwa na sababu ya kumchoma ila ilivyogundulika hivyo nisingeweza kujitokeza maana na mimi pia ningetakiwa kuisaidia polisi kwenye uchunguzi.
“Kubwa kuliko yote, yeye ni ndugu yangu kabisa. Mama yake na mama yangu ni ndugu, nisingeweza kumchoma.”
“Jambo la muhimu nililoamua kufanya ilikuwa ni kutoa taarifa kwa ndugu zake wengine ili waweze kumsaidia.
Nilifanya hivyo kwa wakati. Siku zote nimekuwa karibu naye, hata nikienda China huwa nakwenda kumtembelea gerezani,” alisema Jack.

Masheikh, Askofu Waingia Matatani kwa Uchochezi

Masheikh, Askofu
POLISI mkoani Mwanza wanamshikilia Imamu wa Msikiti wa Ijumaa, huku likitangaza kuwasaka masheikh wawili wengine pamoja na Askofu (majina yote yanahifadhiwa) kwa kuhusika na uchochezi wa kidini.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ernest Mangu alisema Imamu huyo wa msikiti alitiwa mbaroni kwa madai ya kubainika kwamba wanahusika na usambazaji wa CD za uchochezi ambazo zimekuwa zikihamasisha vurugu pamoja na mauaji ya kidini ikiwa ni pamoja na suala la kuchinja.

Kwa upande wake Askofu Mpemba wa Kanisa la Tanzania Field Evangelist yeye anasakwa kutokana na kutoa mkanda wa video (DVD) yenye jina la ‘Inuka Chinja Ule’ wakati mashehe wawili wanasakwa kwa kuhusika na uandaaji wa mikanda ya video mitatu (DVD) zenye majina ya ‘Unafiki katika Sensa, Kadhia ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar pamoja na Uadui wa Makafiri’.

Wakati huohuo, Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) Mkoa wa Morogoro, limesema huenda likajitenga na Bakwata Taifa kufuatia hatua ya Sheikh Mkuu, Mufti Issa Shaaban bin Simba kumvua madaraka Sheikh wa Mkoa wa Morogoro, Yahya Semwali bila kufuata utaratibu.
Mwananchi

Yule Mtoto Mlemavu wa Ngozi (Albino) Aliyekatwa Mkono wa Kushoto Mkoani Tabora Huyu Hapa

Mwigulu Matonange(10
Mtoto Mwigulu Matonange (10)ambaye amekatwa mkono wa kushoto na watu wasiojulikana mkoani tabora akiwa na baba yake Gimbishi kwa mwaka huu walemavu wa ngozi(Albino)wamekua wakikatwa mikono ya kushoto, ikiwa ni tofauti na miaka mitatu iliyopita ambapo waliokumbwa na ukatili huo walikatwa mikono ya kulia.
--
BAADA ya kuibuka upya kwa matukio ya kuuawa na kukatwa viungo vya miili kwa watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), wanaharakati nchini wameitaka Serikali kuchunguza kwa kina sababu za mauaji hayo, kuimarisha ulinzi hasa katika maeneo wanayoishi watu wa kundi hilo.

Wakati wanaharakati hao wakieleza hayo, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu amesema mauaji hayo yanatokana na baadhi ya watu kuwa na imani za kishirikina, kwamba wakipata viungo vya watu wenye ulemavu watapata utajiri.
Alisema tayari Serikali imemuagiza Ofisa Maendeleo ya Jamii Rukwa ambao ulikumbwa na mauaji hayo, kukutana na maofisa maendeleo wa wilaya zote za mkoa huo kwa ajili ya kuwapa elimu wananchi.

Katika miaka ya hivi karibuni, jumla ya albino 72 wameuawa, 34 wamenusurika, wengi wao kwa kukatwa viungo au kuumizwa. Makaburi 15 yamefukuliwa na viungo kuchukuliwa na kumekuwa na majaribio manne ya kufukua makaburi.Kwa habari zaidi Bofya na Endelea....>>>>>>

Ni Lil Wayne vs Pitbull. Lazma Kinuke Soon!

Lil Wayne ameamua kujibu diss ya Pitbull kwenye Twitter. Ugomvi huo ulianza baada ya Lil Wayne kudiss team ya Miami Heat na kusema kwamba amelala na mke wa Chris Bosh.
Wasanii kama Trick Daddy na Pitbull hawakupenda maneno hayo. Pitbull aliamua kumdiss Lil Wayne kwenye wimbo wake mpya “Harlem Shake (Welcome 2 Dade County).

Mtanzania Apewa Uwaziri Rwanda

Paul Kagame
RAIS Paul Kagame wa Rwanda amemteua Mtanzania, Profesa Silas Rwakabamba kuwa Waziri wa Miundombinu wa nchi hiyo katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyofanyika Jumatatu iliyopita.

Kabla ya uteuzi huo, Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda. Ni mmoja wa mawaziri wanaoingiza sura mpya katika Baraza la Rais Kagame ambalo amelifanyia mabadiliko kwa kuunda wizara nyingine mpya.

Sura nyingine mpya katika Baraza hilo ambalo liliapishwa juzi Ikulu ya Rwanda ni pamoja na Seraphine Mukantabana (Wakimbizi na Menejimenti ya Maafa) na Oda Gasinzigwa (Ofisi ya Waziri Mkuu- Familia na Jinsia).

Akizungumza kwa simu na mwandishi wetu jana, mdogo wa Profesa Rwakabamba, Timothy Rwamushaija anayeishi Dar es Salaam, alisema ndugu yake alizaliwa katika Kijiji cha Bushagara, Wilaya ya Muleba mkoani Kagera.

Alisema Profesa Rwakabamba alikuwa Mtanzania aliyeamua ...

Sijue Sifa za Kila Mkoa wa Tanzania

Sijue Sifa za Kila Mkoa

Lulu Akanusha Kuomba Msaada

Lulu
LULU ambaye kwa sasa yupo uraiani kwa dhamana huku kesi yake ya tuhuma za kuua bila kukusudia ikiendelea, amesema kuwa hajafungua taasisi yoyote wala kuomba
misaada kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook. "Nasikia tu kwa watu eti sijui ninataka wasanii waigizaji kwa ajili ya taasisi yangu, mara nimetoa namba ya simu watu wanichangie ili nitengeneze filamu, sijafanya kitu kama hicho na wala siwezi nahitaji kutulia na kuangalia mambo yangu,"alisema.
Hivi karibuni kupitia facebook kumeonekana akaunti inayotumia picha na majina ya Lulu kwa kuwaomba wadau wa filamu wamchangie fedha kwa njia ya m-pesa na tigo-pesa.
Lulu anatuhumiwa kuhusika na kifo cha aliyekuwa msanii wa filamu, Steven Kanumba, kilichotokea mwaka jana.

Homeless Man's Astonishment After Donors Pledge Him $150,000 for Returning Diamond Engagement Ring

Homeless
KCTV 5 - Homeless: Billy Ray Harris's good deed has earned him over $150,000 (KCTV 5)
A homeless man has become the centre of a global fundraising campaign - after returning a diamond engagement ring to a bride-to-be who dropped it in his coffee cup.

Sarah Darling lost her ring on the streets of Kansas City when she it unknowingly dropped it into a cup belonging to Billy Ray Harris.
She desperately dashed back to the scene the next day after realising it was missing, and was overjoyed when Harris returned the valuable jewellery straight back to her.

The feel-good story has touched so many people that an online fundraising page for homeless Harris has since pulled $150,000 in less than a fortnight.
The act of selflessness by Harris, who sleeps under a bridge and spends his days in a square in Kansas City, has since been described as a 'miracle' by Ms Darling's fiance, Bill Krejci.

Mr Krejci, who set up the online donations page himself, said the act of generosity 'makes you realise that there are good people out there'.
The donations, which on Tuesday afternoon stood at $151,000, are currently enough for Harris to..
Read more..

Scam Series #13

Scam Series #13
Dear Friend.
Greetings to you and your family, I am the manager of bill and exchange in THE BANK, I have a business of 5.5 Million United State Dollars to be transfer to your account for investment in your country, if you are ready to assist me get back to me, I will give you full details on how the fund will be transfer to you.

Be rest assured that everything will be handled confidentially because, this is a great opportunity we cannot afford to miss, as it will make our family profit a lot.
It has been 6 years go, that most of the greedy African Politicians used our bank to launder money overseas through the help of their Political advisers.
Most of the funds which they transferred out of the shores of Africa were gold and oil money that was..