In this first episode of 2013 Kali TV covers Black Girls Ignite Africa Workshop in Maryland which Chardelle Moore was invited to talk as Kali TV Host on her role as young woman in the media. Kali TV also travelled to NY to cover Yoliswa Cele US Africa Synergy Ambassador fundraising event which focuses on helping kids in Kwazulu Natal. We also featured Young African Professional Network (YAP) end of the year party and also visited Sibusiso Kunene a South African Immigrant who feeds homeless every tuesday in Washington DC.
Huenda Mwanamuziki Joseph Chameleone wa Uganda Akafunguliwa Mashitaka ya Mauaji!
Gazeti la Sunday Mail la Uganda limeripoti kwamba Polisi wa nchi hiyo wanaendesha uchunguzi ambapo huenda wakamfungulia mashitaka ya mauaji mwanamuziki Jose Chameleone, mke wake Daniella na kundi la muziki la Leon Island.
Ni kutokana na kifo cha Robert Karamagi (27) aliyefariki katika Hospitali ya Mulago baada ya majeraha aliyoyapata nyumbani kwa mwanamuziki huyo huko Seguku Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Kajjansi Ibrahim Saiga alisema wamechukua ushahidi mbalimbali kutoka kwa majirani na mashuhuda walioona, ushahidi ambao unapingana na ule uliotolewa na familia ya Mayanja.
Pamoja na kusema faili la uchunguzi huo litapelekwa kwa Mwendesha Mashitaka wa Serikali (DPP) kwa ushauri, Saiga alisema pia baba wa Karamagi alikana kwamba mwanaye alijimwagia mafuta na kujiwasha moto, pia alisema mwanaye alipomwita hospitalini alimwambia aliteswa, akafungwa kamba, akamwagiwa mafuta na kuchomwa moto na mwanamuziki huyo pamoja na wenzake wa kundi lake.
Ni kutokana na kifo cha Robert Karamagi (27) aliyefariki katika Hospitali ya Mulago baada ya majeraha aliyoyapata nyumbani kwa mwanamuziki huyo huko Seguku Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Kajjansi Ibrahim Saiga alisema wamechukua ushahidi mbalimbali kutoka kwa majirani na mashuhuda walioona, ushahidi ambao unapingana na ule uliotolewa na familia ya Mayanja.
Pamoja na kusema faili la uchunguzi huo litapelekwa kwa Mwendesha Mashitaka wa Serikali (DPP) kwa ushauri, Saiga alisema pia baba wa Karamagi alikana kwamba mwanaye alijimwagia mafuta na kujiwasha moto, pia alisema mwanaye alipomwita hospitalini alimwambia aliteswa, akafungwa kamba, akamwagiwa mafuta na kuchomwa moto na mwanamuziki huyo pamoja na wenzake wa kundi lake.
Jose Chameleone akihojiwa na NTV Uganda na kusema kwamba hilo swala wameliacha kwenye mikono ya polisi, gazeti la sunday mail limeripoti pia kwamba alhamisi iliyopita Jose Chameleone alihojiwa na wapelelezi kwa muda mrefu lakini aliachiwa kwa dhamana.
Jaji Mkuu Azindua Kitabu cha Sheria Chenye Maandiko ya Kesi Mbalimbali Pamoja na Jarida la Makala
Wanachuo Kipawa Sasa Kulipa Ada kwa M-Pesa

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo eneo la Kipawa kilipo chuo hicho Dar es Salaam, Mkuu wa Ukuzaji Biashara; M-Pesa Jackson Kiswaga amesema kuanza kwa huduma hiyo ni mwendelezo wa azima ya Vodacom ya kuyaleta maisha ya watanzania kiganjani kupitia teknolojia ya simu za mkononi. Amesema katika mipango ya kuwezesha malipo ya ..
Mwandishi wa Redio Kwizera Issa Ngumba Ameuliwa Porini na Watu Wasiojulikana!!

Taarifa kutoka Kigoma zilizotufikia hivi punde zinadai kuwa mwili wa mwanahabari huyo umekutwa nje kidogo na mkoa wa Kigoma.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kigoma RPC Kishai amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwa bado jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi zaidi .
Mbunge wa jimbo la Kigoma Zitto Kabwe pia amepata kuzungumza na mtandao huu na kudai kuwa ameguswa na kifo cha mtangazaji huyo na kutaka jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina dhidi ya kifo chake
Pia Kabwe ameeleza jinsi ambavyo mwanahabari huyo alivyoweza kuifanya kazi yake kwa jamii ya Kigoma kwa ufanisi zaidi na kuwa wakati mwingine yeye kama mbunge alikuwa akizunguka na mwanahabari huyo katika jimbo lake.
" Kweli nimeguswa sana na kifo cha kusikitisha cha mwanahabari huyo nilimfahamu vema kwa utendaji kazi wake ila nawapa pole sana waandishi wote nchini kwa msiba huu mkubwa .....na zaidi nitapata kueleza mengi mara baada ya uchunguzi"
Taarifa za awali zilizotolewa na Jeshi la Polisi wilayani Kakonko baada ya kupotea kwa mwanahabari huyo zilisema kuwa Bw Ngumba alipotea tangu January 05 mwaka huu majira ya saa 11 jioni ambapo alimuaga mke wake Bi. Rukia Yunus kuwa anakwendwa Muhange senta wilayani Kakonko na kwamba hajarudi nyumbani hadi sasa.
Kufuatia tukio hilo jeshi la polisi kwa kushirikiana na wananchi wa Kijiji cha Muhange wanaendelea kumtafuta katika mapori ya kijiji hicho baada ya rafiki zake kueleza kuwa aliwaanga kuwa anakwenda kutafuta dawa msituni.

Aidha jeshi la polisi Wilayani Kibondo liliomba kampuni za mitandao ya simu anayotumia Bw Ngumba kusaidia kutambua simu zake zilipotumika kwa mara ya mwisho ili kurahisisha upatikanaji wake. Akizungumza kwa njia ya simu, Mke wa Bw Issa Ngumba, Bi Rukia Yunus amesema kuwa wananchi walio wengi ambao walikuwa wakimtafuta maporini wamerudi kijiji hapo baada ya kumkosa.
Maswali yaliyo jitokeza!!
1. Kawaida redio hiyo hutangaza taarifa/habari za aina gani?
2. Ngumba amekuwa akiandika habari/taarifa za aina gani?
3. Je, ni mwandishi mwololo au ana mtima wa nyundo?
... 4. Je, ni mtafiti/mchunguzi na mchambuzi (alikuwa na kipindi maalum redioni)?
5. Mahusiano yake na wenzake yalikuwa ya namna gani?
6. Mahusiano yake na wenye chombo yalikuwaje?
7. Mara ya mwisho aliandika habari zipi (zilihusu nini, nani na wapi)?
8. Anafahamika kwa kuandika nini kilichosisimua nywele za wengi?
9. Kazi yake iliyowahi kuibua mjadala miongoni mwa wenzake, mwajiri na wasomaji?
10. Alikuwa anapanga kufanya nini/kufuatilia nini (kile ambacho wenzake walifahamu)?
11. Alikuwa na uhusiano wowote na polisi (upi)?
12. Uhusiano wake na watawala wilayani ulikuwa wa aina gani?
13. Je, ni mwandishi aliyejua mambo mengi na ya ndani ya utawala wilayani?
14. Je, ni mwandishi aliyejua biashara za wazi na siri za "wakubwa?"
15. Mbali na kituo chake cha redio, alikuwa akipeleka wapi kazi zake (zipi)?
16. Uhusiano na mkewe ulikuwa wa aina gani (kwa mujibu wa watu wa karibu)?
17. Alikuwa na tabia gani (majivuno, ukarimu, wepesi/uzito wa kuelewa, ushabiki wa mambo (yapi); au alikuwa mpigania haki, mpenda kujielimisha na mtafutaji aliyetaka kuleta mabadiliko katika kazi/maisha/familia yake (vipi)?
18. Alikuwa na watoto (wangapi, wako wapi)?
Maswali haya nimempelekea pia mwandishi Kayanda aliyeko Kigoma. Ni muhimu tujue angalau haya machache.
1. Kawaida redio hiyo hutangaza taarifa/habari za aina gani?
2. Ngumba amekuwa akiandika habari/taarifa za aina gani?
3. Je, ni mwandishi mwololo au ana mtima wa nyundo?
... 4. Je, ni mtafiti/mchunguzi na mchambuzi (alikuwa na kipindi maalum redioni)?
5. Mahusiano yake na wenzake yalikuwa ya namna gani?
6. Mahusiano yake na wenye chombo yalikuwaje?
7. Mara ya mwisho aliandika habari zipi (zilihusu nini, nani na wapi)?
8. Anafahamika kwa kuandika nini kilichosisimua nywele za wengi?
9. Kazi yake iliyowahi kuibua mjadala miongoni mwa wenzake, mwajiri na wasomaji?
10. Alikuwa anapanga kufanya nini/kufuatilia nini (kile ambacho wenzake walifahamu)?
11. Alikuwa na uhusiano wowote na polisi (upi)?
12. Uhusiano wake na watawala wilayani ulikuwa wa aina gani?
13. Je, ni mwandishi aliyejua mambo mengi na ya ndani ya utawala wilayani?
14. Je, ni mwandishi aliyejua biashara za wazi na siri za "wakubwa?"
15. Mbali na kituo chake cha redio, alikuwa akipeleka wapi kazi zake (zipi)?
16. Uhusiano na mkewe ulikuwa wa aina gani (kwa mujibu wa watu wa karibu)?
17. Alikuwa na tabia gani (majivuno, ukarimu, wepesi/uzito wa kuelewa, ushabiki wa mambo (yapi); au alikuwa mpigania haki, mpenda kujielimisha na mtafutaji aliyetaka kuleta mabadiliko katika kazi/maisha/familia yake (vipi)?
18. Alikuwa na watoto (wangapi, wako wapi)?
Maswali haya nimempelekea pia mwandishi Kayanda aliyeko Kigoma. Ni muhimu tujue angalau haya machache.
Silaha 439 Zasalimishwa Kwa Hiari Polisi

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na Msemaji wa Jeshi la Polisi, ASP, Advera Senso, baadhi ya silaha zilizosalimishwa na idadi yake katika mabano ni pamoja na shortgun (29), gobore (352), SMG (11), riffle (20), bastola (22), airgun (1), rocket launcher (2) na SAR (2).
Kutokana na tatizo la kuzagaa na matumizi holela ya silaha zinazomilikiwa isivyo halali na kinyume cha sheria nchini, Desemba 4, mwaka jana, Waziri Nchimbi aliagiza kuwa katika kipindi cha mwezi mmoja mtu yeyote ama kikundi chochote kinachomiliki silaha kinyume cha sheria kuzisalimisha katika vituo vya polisi au ofisi yoyote ya serikali iliyo karibu nao.
Waziri Nchimbi aliagiza pia silaha hizo kusalimishwa kwa wenyeviti wa serikali za mitaa, vijiji, vitongoji, wakuu wa wilaya, mikoa na madhehebu ya dini.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, zoezi hilo limefanyika kote nchini kuanzia ...
Kutokana na tatizo la kuzagaa na matumizi holela ya silaha zinazomilikiwa isivyo halali na kinyume cha sheria nchini, Desemba 4, mwaka jana, Waziri Nchimbi aliagiza kuwa katika kipindi cha mwezi mmoja mtu yeyote ama kikundi chochote kinachomiliki silaha kinyume cha sheria kuzisalimisha katika vituo vya polisi au ofisi yoyote ya serikali iliyo karibu nao.
Waziri Nchimbi aliagiza pia silaha hizo kusalimishwa kwa wenyeviti wa serikali za mitaa, vijiji, vitongoji, wakuu wa wilaya, mikoa na madhehebu ya dini.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, zoezi hilo limefanyika kote nchini kuanzia ...
Mbunge wa Kenya Atinga Bungeni na Kiduku -Mohawk



Subscribe to:
Posts (Atom)