
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na Msemaji wa Jeshi la Polisi, ASP, Advera Senso, baadhi ya silaha zilizosalimishwa na idadi yake katika mabano ni pamoja na shortgun (29), gobore (352), SMG (11), riffle (20), bastola (22), airgun (1), rocket launcher (2) na SAR (2).
Kutokana na tatizo la kuzagaa na matumizi holela ya silaha zinazomilikiwa isivyo halali na kinyume cha sheria nchini, Desemba 4, mwaka jana, Waziri Nchimbi aliagiza kuwa katika kipindi cha mwezi mmoja mtu yeyote ama kikundi chochote kinachomiliki silaha kinyume cha sheria kuzisalimisha katika vituo vya polisi au ofisi yoyote ya serikali iliyo karibu nao.
Waziri Nchimbi aliagiza pia silaha hizo kusalimishwa kwa wenyeviti wa serikali za mitaa, vijiji, vitongoji, wakuu wa wilaya, mikoa na madhehebu ya dini.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, zoezi hilo limefanyika kote nchini kuanzia ...
Kutokana na tatizo la kuzagaa na matumizi holela ya silaha zinazomilikiwa isivyo halali na kinyume cha sheria nchini, Desemba 4, mwaka jana, Waziri Nchimbi aliagiza kuwa katika kipindi cha mwezi mmoja mtu yeyote ama kikundi chochote kinachomiliki silaha kinyume cha sheria kuzisalimisha katika vituo vya polisi au ofisi yoyote ya serikali iliyo karibu nao.
Waziri Nchimbi aliagiza pia silaha hizo kusalimishwa kwa wenyeviti wa serikali za mitaa, vijiji, vitongoji, wakuu wa wilaya, mikoa na madhehebu ya dini.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, zoezi hilo limefanyika kote nchini kuanzia ...