President Obama welcomes the 1972-1973 Miami Dolphins to the White House to honor their 1973 Super Bowl win and their undefeated season. August 20, 2013.
Soma Mambo100 Usiyoyajua Kuhusu Chokochoko za Rwanda kwa Tanzania

Historia ya Rwanda ni ndefu iliyojaa misukosuko ya kisiasa, kupinduana, vita na mauaji ya wenyewe kwa wenye yaliyosababishwa na ubaguzi wa kikabila.
Rwanda imekuwa ikipita katika vipindi vigumu na vya hatari. Vipindi hivi hufuatana na mauaji ya raia wa nchi hiyo, sio tu kutokana na sababu za ukabila bali pia uongozi mbaya wa kisiasa.
Mwaka 1959, mtawala wa Kitutsi aliyekuwa akiitawala nchi hiyo na kulalamikiwa kuwa utawala wake ulikuwa ukiwaneemesha zaidi Watutsi walio wachache, uliangushwa na Wanyarwanda wa Kabila la Kihutu.
Mabadiliko haya yalifuatiwa na mauaji ya takriban Watutsi 150,000. Walioponea chupuchupu walikimbilia nchi mbalimbali jirani na Rwanda.
Ni wakati huu wazazi wa Rais wa sasa wa Rwanda, Paul Kagame walikimbilia nchi jirani, Uganda yeye akiwa na umri wa miaka miwili.
Baada ya hapo, Wahutu wakaunda Chama cha PARMEHUTU, kikiongozwa na Gregoire Kayibanda, ambaye baadaye alikuwa Rais wa Rwanda.
Mtu angedhani wakati huo kuwa kwa sababu uongozi wa nchi hiyo ulichukuliwa na kudhibitiwa na mtu kutoka kabila la Wahutu waliokuwa asilimia 88 ya Wanyarwanda wakati ule, (Watutsi wakiwa asilimia 11 na asilimia moja Watwa), kusingekuwa na chokochoko tena. Utawala ungekuwa wa amani, wapi?
Mapinduzi ya kijeshi
Kinyume na matarajio, Julai 5, 1973 Serikali hii nayo ilipinduliwa. Mapinduzi haya yalifanywa na jeshi la Wahutu wakiongozwa na Meja Jenerali Juvenal Habyarimana, ambaye naye alikuwa Mhutu.
Cha ajabu, licha ya tofauti hizo za kikabila, mapinduzi hayo yalifanywa na Wahutu walio wengi wakishirikiana na Watutsi wachache. Hii ilitokana na malalamiko kuwa Rais Kayibanda alikuwa akiendesha nchi kama familia yake, akipitisha uamuzi bila kushirikiana na viongozi wengine.
Baada ya mapinduzi hayo, kiongozi huyo mpya alibadilisha mambo mengi ikiwa ni pamoja na kusambaratisha chama kilichokuwa kikiongozwa na Kayibanda, PARMEHUTU, badala yake akaunda Chama cha National Revolutionary Movement for Development MRND.
Miaka takriban 17 baadaye kutokana na kile kilichoonekana kama utawala wa kikandamizaji, Watutsi waliokuwa nje ya nchi walishirikiana na Wahutu wa ndani kuanza harakati za kuiangusha Serikali ya Habyarimana.
Harakati hizi ndizo zilizomwingiza madarakani Rais wa sasa, Paul Kagame. Malalamiko kama yale yaliyosababisha mapinduzi dhidi ya mtangulizi wa Habyarimana yakajitokeza tena.
Mtu anayeangalia na kuchambua hali ya mambo ilivyo hivi sasa hachelewi kung’amua kuwa hali kama ile iliyozikumba tawala za tangu utawala wa kifalme wa Watutsi na tawala za Kihutu zinajitokeza tena.
Na hii inaifanya hali iwe tete kuliko wakati wowote. Wengi wanaamini kama yatatokea mapigano au mabadiliko katika Serikali ya Kigali pengine hali inaweza kuwa mbaya kuliko ilivyowahi kushuhudiwa.
Hivi sasa Wanyarwanda hasa kutoka Kabila la Kitutsi na ambao walikuwa bega kwa bega na Rais Kagame, baadhi ya wasomi na maofisa wa juu kutoka jeshi la RPF wameikimbia Rwanda na tayari kuna kampeni za chini kwa chini kutoka makabila yote mawili kuupinga utawala wa Kagame.
Mbaya zaidi kuna kundi kubwa la vijana waliozaliwa baada ya mauaji ya Rwanda. Hili ni kundi kubwa na mtu yeyote ambaye amekuwa akitembelea kambi za wakimbizi kwa miaka mingi anaelewa ninachoelezea hapa.
Mwaka 1997 nikiwa na waandishi wenzangu tulitembelea kambi za wakimbizi kutoka Rwanda. Kulikuwa na idadi kubwa ya watoto. Mmoja wetu alimuuliza mmoja wa wakimbizi kwa utani “nyinyi mpo kwenye matatizo mbona mnazaa watoto wengi hivi, hamuoni ikiwa mnajiongezea mizigo”?
“Hawa ndio watakuja kuikomboa Rwanda,” alijibu kiongozi wa wakimbizi huku akipigiwa makofi na kundi la vijana waliokuwa pembeni kusikiliza mahojiano, katika kambi ya Mbuba wilayani.
Nadharia hii imekuwa ikiendelea kwa miaka mingi. Hata tulipotembelea kambi nyingine tukiandamana na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia wakimbizi Ulimwenguni (UNHCR), Antonio Guateres karibu waandishi wengi hawakuficha hisia zao za kushangazwa na kasi ya kuzaana katika kambi za wakimbizi.
Fikiria kwa utaratibu huu watoto waliozaliwa tangu mwaka 1994 ni watu wazima. Kama ni wanajeshi ni jeshi kubwa tena lenye hamasa kubwa ya kurudi katika nchi yao Rwanda katika wakati ambapo wanaona kikwazo ni Kagame na Serikali yake.
Hivi Kagame anajua kuwa kundi hili halibanwi na tuhuma za mauaji ya halaiki ya Rwanda ya mwaka 1994? Hata wale wanaotafutwa sio tena kitisho dhidi ya Serikali ya Kigali sababu ni wazee sasa, wa kuogopa ni jeshi hili kubwa la vijana.
Hawa Kagame anawabana na sheria gani? Isipokuwa kwamba wanajiandaa kupigana na Serikali yake kama yeye alivyofanya kuipindua Serikali ya Habyarimana akitokea Uganda?
Kibaya zaidi ni kuwa makundi haya katika ukanda wa Maziwa Makuu, wana mawasiliano na kwa nyakati fulani yanasaidiana.
Ushauri wa Rais Kikwete
Ninaamini hiki ndicho kilichomsukuma Rais Kikwete kutoa ushauri kwa marais hawa majirani zetu kuwa wasifanye kosa wazungumze na waasi. Heri kupatana nao kwa sasa kuliko baadaye wakisharidhika kuwa wamejiandaa vizuri na wakaanza mapigano rasmi.
Kila mwenye macho ya kuona mbali hachelewi kumshauri Kagame chonde chonde ongea na waasi hawa, badala ya kujiridhisha kuwa ni watuhumiwa wa mauaji ya halaiki, wakati wengine mauaji hayo yalitokea wakiwa na umri wa miaka sita na kurudi chini, hawa ni jeshi kubwa lenye uwezo wa muda mrefu wa kukaa msituni, ni hatari.
Yapo maswali kadhaa ya kujiuliza, hivi kwa nini Rais Kagame hakioni hiki tunachokiona sisi? Kwa nini hakioni hiki ambacho amekiona Rais mwenzake Kikwete?
Ninaamini Rais Kikwete hakukurupuka, ana vyombo vya kiintelijensia vinavyomfahamisha kinachoendelea sio tu Tanzania, lakini hata katika mapori makubwa na Misitu ya DRC.
Kagame anapaswa kusoma alama za nyakati, asikimbilie kusema “watuache Rwanda tumalize matatizo yetu,” kwani baada ya mauaji ya mwaka 1994 nchi hiyo ililaumu jumuia ya kimataifakuwa haikuisaidia Rwanda kuepuka mauaji hayo.
Kama walivyosema Wahaya kuwa “ajuna akanyonyi ajuna akakyahalala” maana ukitaka kumsaidia ndege msaidie akiwa bado ana uwezo wake wa kupaa.
Badala yake ametoa lugha za matusi kashfa hadi kutoa vitisho dhidi ya Tanzania, ati kwa ushauri aliopewa na Rais Kikwete, kuwa azungumze na waasi wa Democratic Forces for The Liberation of Rwanda (FDLR).
Kikwete alitoa ushauri huo kwenye Kamisheni ya Ulinzi na Usalama ya Umoja wa Afrika wakati wa Mkutano wa wakuu wa nchi za umoja huo uliofanyika mwanzoni mwa Juni mwaka huu, mjini Addis Ababa, nchini Ethiopia.
Ushauri huo umegeuka mwiba na kitanzi dhidi ya uhusiano uliokuwepo kati ya Tanzania na Rwanda, ingawa wengine tunajua uhusiano huo haukuwa barabara tangu awali kwani kiongozi huyo wa Rwanda mara kwa mara amekuwa akiisimanga Tanzania hata kabla ya ushauri huo kutolewa.
Imekuwa kama vile jirani yetu huyu amepata turufu muhimu ya kuitishia Tanzania.
Kinachoshuhudiwa sasa ni vita ya maneno baina ya nchi hizi mbili yaani Tanzania na Rwanda.Vita ya maneno na majibizano ya namna hii mataifa hujikuta katika vita kamili.
Kwa upande mwingine wengi walishangaa kwa nini Kagame aonekane kukerwa sana wakati ushauri huo haukumhusu yeye peke yake?
Wakati Paul Kagame akikabiliwa na kundi linaloinyemelea nchi yake la FDLR, Joseph Kabila, wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) anapambana na waasi wa sasa wa M23, na Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda akitishiwa na makundi mawili. Allied Democratic Force (ADF) na Lord’s Resistance Army (LRA).
Hata hivyo, si Tanzania pekee ambayo imeona hatari inayoinyemelea Rwanda bali hata moja ya makanisa nchini Rwanda.
Kanisa hilo lilipeleka ujumbe hivi majuzi hadi Ikulu ya Kagame likitabiri kuwa Rwanda inakabiliwa na matatizo makubwa na kuwa inaweza tena kudidimia katika mgogoro mkubwa. Watumishi hao wa Mungu wameishia kukamatwa na kuambiwa wanataka kuvuruga amani kuleta mgororo wa kikabila.
Uasi zaidi
Kila kukicha wanajeshi wa Rwanda wanazidi kulikimbia jeshi lao na nchi yao, siku zilizopita walikuwa wakikimbilia Uganda siku hizi baada ya kuzidishwa ulinzi katika mpaka wa nchi hizo mbili sasa wanakimbilia Afrika Kusini, nchi ambayo inajua kwa hakika kitu gani kinaendelea nchini Rwanda. Inawapa hifadhi ya ukimbizi wa kisiasa.
Miongoni mwao ni aliyekuwa Mkuu wa Usalama katika Jeshi la RPF, Luteni Jenerali Faustin Kayumba Nyamwasa. Huyu alianza kutofautiana mapema na Kagame, baadaye akamsogeza mbali na nchi hiyo. Akamteua kuwa Balozi wa Rwanda nchini India.
Bado Kagame aliendelea kumwona ofisa huyo tishio, hivyo akamtuhumu kuwa alihusika na milipuko ya mabomu February 2010 mjini Kigali. Wakati Kagame akiandaa utaratibu wa kumkamata habari zikavuja, ofisa huyo akatoroka kutoka India hadi Afrika Kusini anapoishi sasa.
Inafahamika kuwa maofisa wenye uwezo kama wa Nyamwasa wakipata ushirikiano na wanamgambo wa Kihutu walio sehemu mbalimbali nje ya Rwanda ni rahisi kuishambulia Rwanda, ndio maana inasemekana wametumwa makachero kumuua Nyamwasa kule kule Afrika Kusini lakini ‘wakachemka’ na kuishia kwenye mikono ya polisi ambapo walikiri kutumwa na Serikali ya Kigali, kumuua Nyamwasa.
Mwezi Juni 2010, Kiongozi wa Timu ya mpira wa miguu wa Rwanda Brigedia Jenerali Jean Bosco Kazura, alikwenda Afrika Kusini kuangalia mashindano ya kombe la dunia, lakini aliporejea Rwanda akakamatwa kwa tuhuma kuwa akiwa huko alifanya mawasiliano na Nyamwasa na kwa maana hiyo akaingizwa katika kundi la wanaotaka kuiangusha Serikali ya Kagame.
Jean-Léonard Rugambage, mwandishi wa habari ameuawa na makachero ikisemekana kuwa alikuwa akitumiwa na Nyamwasa.
Maofisa wa Serikali ya Rwanda wanapotetea msimamo wa Rais Kagame wa kuikejeli Tanzania wanadai kilichomkasirisha bosi wao ni kushauriwa akae meza moja na wale anaowaona kama wauaji wa halaiki wa mwaka 1994, na kuwa ushauri huo ni sawa na kucheza juu ya makaburi ya Wanyarwanda waliopoteza maisha katika mauaji hayo.
Hata kama ingekuwa hivyo, basi angewachukia waasi wale lakini sio Tanzania kwa sababu baada ya mauaji ya Rwanda, iwe Kagame au waasi wenyewe hakuna upande wowote uliowahi kuituhumu Tanzania kuhusika kwa namna yoyote katika mauaji hayo, kwa sababu wanajua kuwa nchi hii ilikuwa ikijua kila kilichokuwa kikiendelea na kikifanywa na kila upande kabla na baada ya mauaji hayo.
Na hapo ndipo lilipo ‘fumbo la imani’ kwa nini Kagame amechukia sana kwa ushauri ule.
Sababu nyuma ya pazia
Udhaifu wa sababu ya chuki za Kagame unaashiria kwamba kilichoikasirisha Rwanda ni uamuzi wa Tanzania kupeleka jeshi lake lishiriki kulinda amani DRC, na sio ushauri ule.
Alijua kuwa sasa mengi yatafumuka, ambayo tayari Tanzania inayafahamu ikichanganya na yale itakayoyagundua DRC.
Nina mifano mingi na ushahidi wa kimazingira hebu nitaje mmoja na kumalizia makala yangu.
Yaliyotokea 1994
Rwanda inajua, Kagame anajua, na dunia nzima inajua kuwa mauaji ya kimbali ya Rwanda yalikolezwa zaidi ya kutunguliwa ndege ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo wakati huo, Habyarimana.
Habyarimana na mwenzake wa Burundi, Syprian Ntaryamirwa walikuwa wakitoka Arusha nchini Tanzania katika mojawapo ya mikutano yenye lengo la kuangalia namna ya kugawana madaraka baina ya Serikali ya Kigali ya wakati ule na kundi la waasi siku zile RPF.
Kikundi hiki cha RPF kikiwa na Watutsi wengi kilikuwa kimeanzisha mapigano dhidi ya Serikali ya Habyarimana miaka miwili kabla wakipigana kutokea nchini Uganda wakitaka Serikali itoe nafasi kwa Watutsi karibu lakini tano waliokuwa wakiishi nje ya Rwanda.
Licha ya Serikali ya Habyarimana kusaini makubaliano ya kuwaingiza waasi wa RPF katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa, Wahutu ambao ndio walio wengi walikuwa hawakubaliani na jambo hili.Kwa hiyo, fikiria inakuja kufahamika kuwa Watutsi wale walioanzisha mashambulizi kutokea nchini Uganda, wametungua ndege ya Rais wa kabila lao na kumuua pamoja na makamanda wa ngazi za juu wa jeshi la Rwanda la wakati ule.
Ndio maana baada ya kutunguliwa ndege hiyo Aprili 1994 mauaji ya kutisha yaliyodumu kwa siku mia moja yaliendelea na kugharimu maisha ya Wanyarwanda laki nane, wengi wao wakiwa Watutsi na Wahutu wenye msimamo wa wastani.
-Imeandikwa na Christopher Buke wa gazeti la mwananchi.
Je Askari Polisi Akikosea, Ashtakiwe Wapi?
Kimaadili, kazi ya msingi ya askari polisi ni kulinda raia na mali zao, wajibu wa msingi ambao umedumu kwa miaka mingi.
Hata hivyo, dhana ya polisi nchini kuwa walinzi wa raia na mali zao imeanza kukosa uhalisia na huenda huko tuendako ikapotea na askari haoi kuchukuliwa kama adui wa raia na mali zao.
Ninasema hivi kutokana na matukio ya uonevu wa wazi unaofanywa na askari hao dhidi ya raia wasio na hatia. Ipo mifano mingi ya unyanyasaji wa polisi dhidi ya raia.
Hapa ninazungumzia askari wa usalama barabarani, askari wa doria, askari wa upelelezi au hata askari wa vyeo vya juu ambao wengi wao hutumia nguvu nyingi na wakati mwingine silaha kupambana na mwananchi wasio na silaha.
Yaani, kila mmoja kwa nafasi yake anapuuza kwa makusudi wajibu wake kuwalinda raia na mali zao, badala yake anaamua kutumia mabavu ili kujinufaisha huku akimdidimiza mwananchi. Ipo mifano ya wazi. Ni matukio ya matumizi ya nguvu dhidi ya wananchi yanayofanywa na askari wetu katika sehemu mbalimbali za nchi.
Mfano hai ambao hautafutika mioyoni mwa wananchi ni mauaji ya kikatili yaliyofanywa hadharani na askari polisi dhidi ya mwandishi wa habari wa kituo cha runinga cha Channel Ten, Daudi Mwangosi ambaye aliuawa hadharani na askari polisi kule Nyololo, Mufindi mkoani Iringa mwaka jana kwa kutupiwa bomu la kutoa machozi.
Mbali na mauaji ya Mwangosi, yapo matumizi ya nguvu na mauaji kadhaa kwa raia yanayofanywa na polisi dhidi ya raia ambayo yanamweka askari mbali na mwananchi na kuifuta ile dhana iliyozoeleka kuwa Jeshi la Polisi ni walinzi wa raia na mali zao.
Mbali na hayo matukio yanayolalamikiwa kila kukicha na wananchi pamoja na watetezi wa haki za binadamu, upo unyanyasaji mkubwa unaofanywa na askari polisi dhidi ya raia mmoja mmoja ambao usipopigiwa kelele au kukemewa au kuingilia kati na Mkuu wa Jeshi hilo, IGP Said Mwema huenda kukajengeka uadui mkubwa kati ya raia na askari polisi nchini kote.
Mbali na matukio hayo makubwa, yapo matukio mbalimbali ya unyanyasaji yanayofanywa na askari polisi katika vituo vya polisi ambapo huwapiga watuhumiwa, kuwapora fedha zao pale wanapofika kama watuhumiwa wa uhalifu katika vituo vidogo.
Askari polisi wa vituo vidogo nchini wanawatambia raia na watuhumiwa kuwa mtu yeyote anapokuwa chini ya polisi hana haki yoyote na anaweza kupigwa hata kuuawa na hakuna sheria yoyote inayoweza kuchukuliwa dhidi ya muuaji kwa kuwa eti, yeye askari yupo kazini.
Kitendo cha polisi kupiga na kuua, iwe kwa raia asiye na tuhuma au mtuhumiwa si moja ya kazi ya askari. Mabango mengi yaliyoandikwa na kubandikwa katika vituo vya polisi yakielekeza mambo mbalimbali yamebakia kama ya biashara barabarani na hakuna ukweli wowote wa kile kinachoandikwa maana yameandikwa nao wenyewe.
Askari wanatafsiri kinyume maneno ‘police force’ kuwa yana maana ya askari kutumia nguvu na kwamba wanapoua mtuhumiwa au raia yeyote iwe kituoni au mahali pengine popote, hakuna utaratibu ulio wazi wa kuwachukulia hatua eti kwa kuwa hiyo ni moja ya kazi ya askari polisi anapovaa magwanda ya jeshi hilo.
Jukumu muhimu na la msingi walilo nalo askari kwa jeshi lao ni kutambua kuwa wapo kwa ajili ya ulinzi wa raia na mali zao, basi! Na raia anapokumbana na uonevu badala ya kupambana au kutumia nguvu kupata haki yake anapaswa kukimbilia polisi kutafuta msaada wa ulinzi na usalama wake na mali zake na si vinginevyo
Mwananchi
Ninasema hivi kutokana na matukio ya uonevu wa wazi unaofanywa na askari hao dhidi ya raia wasio na hatia. Ipo mifano mingi ya unyanyasaji wa polisi dhidi ya raia.
Hapa ninazungumzia askari wa usalama barabarani, askari wa doria, askari wa upelelezi au hata askari wa vyeo vya juu ambao wengi wao hutumia nguvu nyingi na wakati mwingine silaha kupambana na mwananchi wasio na silaha.
Yaani, kila mmoja kwa nafasi yake anapuuza kwa makusudi wajibu wake kuwalinda raia na mali zao, badala yake anaamua kutumia mabavu ili kujinufaisha huku akimdidimiza mwananchi. Ipo mifano ya wazi. Ni matukio ya matumizi ya nguvu dhidi ya wananchi yanayofanywa na askari wetu katika sehemu mbalimbali za nchi.
Mfano hai ambao hautafutika mioyoni mwa wananchi ni mauaji ya kikatili yaliyofanywa hadharani na askari polisi dhidi ya mwandishi wa habari wa kituo cha runinga cha Channel Ten, Daudi Mwangosi ambaye aliuawa hadharani na askari polisi kule Nyololo, Mufindi mkoani Iringa mwaka jana kwa kutupiwa bomu la kutoa machozi.
Mbali na mauaji ya Mwangosi, yapo matumizi ya nguvu na mauaji kadhaa kwa raia yanayofanywa na polisi dhidi ya raia ambayo yanamweka askari mbali na mwananchi na kuifuta ile dhana iliyozoeleka kuwa Jeshi la Polisi ni walinzi wa raia na mali zao.
Mbali na hayo matukio yanayolalamikiwa kila kukicha na wananchi pamoja na watetezi wa haki za binadamu, upo unyanyasaji mkubwa unaofanywa na askari polisi dhidi ya raia mmoja mmoja ambao usipopigiwa kelele au kukemewa au kuingilia kati na Mkuu wa Jeshi hilo, IGP Said Mwema huenda kukajengeka uadui mkubwa kati ya raia na askari polisi nchini kote.
Mbali na matukio hayo makubwa, yapo matukio mbalimbali ya unyanyasaji yanayofanywa na askari polisi katika vituo vya polisi ambapo huwapiga watuhumiwa, kuwapora fedha zao pale wanapofika kama watuhumiwa wa uhalifu katika vituo vidogo.
Askari polisi wa vituo vidogo nchini wanawatambia raia na watuhumiwa kuwa mtu yeyote anapokuwa chini ya polisi hana haki yoyote na anaweza kupigwa hata kuuawa na hakuna sheria yoyote inayoweza kuchukuliwa dhidi ya muuaji kwa kuwa eti, yeye askari yupo kazini.
Kitendo cha polisi kupiga na kuua, iwe kwa raia asiye na tuhuma au mtuhumiwa si moja ya kazi ya askari. Mabango mengi yaliyoandikwa na kubandikwa katika vituo vya polisi yakielekeza mambo mbalimbali yamebakia kama ya biashara barabarani na hakuna ukweli wowote wa kile kinachoandikwa maana yameandikwa nao wenyewe.
Askari wanatafsiri kinyume maneno ‘police force’ kuwa yana maana ya askari kutumia nguvu na kwamba wanapoua mtuhumiwa au raia yeyote iwe kituoni au mahali pengine popote, hakuna utaratibu ulio wazi wa kuwachukulia hatua eti kwa kuwa hiyo ni moja ya kazi ya askari polisi anapovaa magwanda ya jeshi hilo.
Jukumu muhimu na la msingi walilo nalo askari kwa jeshi lao ni kutambua kuwa wapo kwa ajili ya ulinzi wa raia na mali zao, basi! Na raia anapokumbana na uonevu badala ya kupambana au kutumia nguvu kupata haki yake anapaswa kukimbilia polisi kutafuta msaada wa ulinzi na usalama wake na mali zake na si vinginevyo
Mwananchi
Tindikali Yaendelea Kuuzwa Kama Njugu Mitaani Dar
Dar es Salaam. Siku chache baada ya wasichana wawili raia wa Uingereza kumwagiwa tindikali mjini Zanzibar, imebainika kuwa, tindikali za aina mbalimbali zinauzwa kiholela kama njugu jijini Dar es Salaam.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili unaonyesha kuwa jijini Dar es Salaam yapo maduka mengi yanayouza tindikali ya kila aina na bidhaa hiyo inauzwa bila ya udhibiti wowote kuanzia Kariakoo hadi Vingunguti.
Wiki iliyopita, Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele alitoa miezi mitatu kwa wafanyabiashara wa tindikali kujisajili ili kuzuia kuongezeka kwa matukio ya uhalifu kwa kemikali hiyo nchini.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika mitaa ya Dar es Salaam, umebaini kuwa tindikali za aina mbalimbali zinapatikana kwa wingi katika maduka ya rejareja na jumla, huku wauzaji wa bidhaa hizo wakishindwa kutoa tahadhari yoyote kwa wateja wao.
SOMA ZAIDI
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili unaonyesha kuwa jijini Dar es Salaam yapo maduka mengi yanayouza tindikali ya kila aina na bidhaa hiyo inauzwa bila ya udhibiti wowote kuanzia Kariakoo hadi Vingunguti.
Wiki iliyopita, Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele alitoa miezi mitatu kwa wafanyabiashara wa tindikali kujisajili ili kuzuia kuongezeka kwa matukio ya uhalifu kwa kemikali hiyo nchini.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika mitaa ya Dar es Salaam, umebaini kuwa tindikali za aina mbalimbali zinapatikana kwa wingi katika maduka ya rejareja na jumla, huku wauzaji wa bidhaa hizo wakishindwa kutoa tahadhari yoyote kwa wateja wao.
SOMA ZAIDI
Google Blackout Sees Global Web Traffic Plunge by 40% -Internet apocalypse
Worldwide internet traffic plunged by about 40 per cent as Google services suffered an ‘unprecedented’ black-out, web experts have revealed.

The Google data center in Douglas Country, Georgia. The company is refusing to reveal what caused the ‘unprecedented’ blackout
The tech company said all of its services from Google Search to Gmail to YouTube to Google Drive went down for between one and five minutes last night but it refused to elaborate on the reasons why.
According to web analytics firm GoSquared, global internet traffic fell by around 40% during the black-out, reflecting Google’s massive grip on the web.
‘That’s huge,’ GoSquared developer Simon Tabor told Sky News. ‘As internet users, our reliance on Google.com being up is huge.
‘It’s also of note that pageviews spiked shortly afterwards, as users managed to get to their destination.’
A message on the Google Apps Dashboard showed all of its services were hit.
‘We’re aware of a problem with Gmail affecting a significant subset of users. The affected users are able to access Gmail, but are seeing error messages and/or other unexpected behaviour,’ it said.
A later message said: ‘Between 15:51 and 15:52 PDT, 50% to 70% of requests to Google received errors; service was mostly restored one minute later, and entirely restored after four minutes.’
Experts said the outage had cost the company about £330,000 and that the event was unheard of. They are baffled by the cause.
Computer website writer Neil McAllister added said technical experts would be ‘nervous’ as they sought to find out what happened.
‘Exactly how an operation like Google’s can even go dark like that, all at once, is anybody’s guess,’ he said.
By In2EastAfrica Reporter
The Google data center in Douglas Country, Georgia. The company is refusing to reveal what caused the ‘unprecedented’ blackout
The tech company said all of its services from Google Search to Gmail to YouTube to Google Drive went down for between one and five minutes last night but it refused to elaborate on the reasons why.
According to web analytics firm GoSquared, global internet traffic fell by around 40% during the black-out, reflecting Google’s massive grip on the web.
‘That’s huge,’ GoSquared developer Simon Tabor told Sky News. ‘As internet users, our reliance on Google.com being up is huge.
‘It’s also of note that pageviews spiked shortly afterwards, as users managed to get to their destination.’
A message on the Google Apps Dashboard showed all of its services were hit.
‘We’re aware of a problem with Gmail affecting a significant subset of users. The affected users are able to access Gmail, but are seeing error messages and/or other unexpected behaviour,’ it said.
A later message said: ‘Between 15:51 and 15:52 PDT, 50% to 70% of requests to Google received errors; service was mostly restored one minute later, and entirely restored after four minutes.’
Experts said the outage had cost the company about £330,000 and that the event was unheard of. They are baffled by the cause.
Computer website writer Neil McAllister added said technical experts would be ‘nervous’ as they sought to find out what happened.
‘Exactly how an operation like Google’s can even go dark like that, all at once, is anybody’s guess,’ he said.
By In2EastAfrica Reporter
Subscribe to:
Posts (Atom)