Pages

KUMBE PADRI ALIYEMWAGIWA TINDIKALI ZANZIBAR ALIONYWA KABLA YA TUKIO

Joseph Mwang’amba 
 Siku moja baada ya Padri wa Kanisa Katoliki Parokia ya Cheju, Mkoa wa Kusini Unguja, Joseph Mwang’amba kumwagiwa tindikali na watu wasiojulikana, imebainika kuwa alitishiwa kuuawa miezi mitatu kabla ya kukutwa na tukio hilo.
Wakati Padri huyo akieleza hayo, Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, ameijia juu polisi kwa kushindwa kudhibiti matukio ya viongozi wa dini na serikali visiwani humo, kushambuliwa kwa kumwagiwa tindikali huku akilitaka kuwakamata waliohusika na tukio hilo.
Kiongozi huyo wa dini, aliyejeruhiwa maeneo ya usoni, mikononi na kifuani baada ya kumwagiwa tindikali hiyo alisafirishwa jana na ndege ya kukodi ya Shirika la Coastal kutoka visiwani humo hadi Dar es Salaam na baadaye kupelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa matibabu zaidi.
Dk Shein alisema Polisi inatakiwa kuongeza nguvu za uchunguzi ili kukabiliana na matukio ya kikatili ya umwagaji wa tindikali, yanayoshamili visiwani humo hivi sasa.
“Hatuwezi kuviacha vitendo hivi viendelee … ni lazima Jeshi la Polisi lijitahidi kuwatafuta wahusika ili sheria ichukue mkondo wake,” alisema Dk Shein.
Dk Sheni alisema, kitendo hicho ni cha kikatili na kisichovumilika na kuongeza kuwa wahusika lazima wasakwe na kuchukuliwa hatua za kisheria.
Kwa upande wake, Padri wa Parokia ya Mtakatifu Joseph, Zanzibar, Thomas Assenga aliyefuatana na kiongozi huyo mpaka MNH, alisema siku za nyuma Padri Mwang’amba alitolewa vitisho na mtu ambaye hamfahamu wakati akienda kutoa huduma katika kituo cha wazee cha Welezo.
Alisema kabla ya kufika kituoni hapo, kuna eneo ambalo nyakati za asubuhi watu hufanya mazoezi barabarani ambapo kuna mtu mmoja alimtolea maneno ya vitisho.
“Unajua kawaida ya watu wa Zanzibar hufanya mazoezi barabarani, sasa kipindi anapita eneo hilo katika kilima, kuna mtu alimwambia atamfanyia kitu kibaya ambacho hatujui ndiyo hiki au la,” alisema Padri Assenga na kuongeza:
Alisema Juni mwaka huu mara baada ya kupewa vitisho hivyo alikwenda kutoa taarifa kwa Sheha wa eneo hilo na kituo cha polisi.
“Mara baada ya kutolewa vitisho hivyo Juni mwaka huu, alichukua jukumu la kwenda kutoa taarifa kwa mkuu wa eneo hilo (Sheha) na kituo cha polisi.”
Akielezea tukio la kumwagiwa tindikali Padri Mwang’amba, alisema alimwagiwa saa 9:45 alasiri juzi wakati akizungumza na simu nje ya internet cafĂ© iliyopo eneo la Mlandege.

Dream ft Syllabas - So Sweet (Audio)

Dream ft Syllabas

Flying Car Design Unveiled - Terrafugia Transition Ttreet-Legal Aircraft

New Flying Car Design Unveiled

Thadeo Mutembei Boosting Teachers Morale with a Trip to Dubai, Car and Laptop..!

Given the tough environment under which most teachers operate in the country, a private secondary school owner has awarded his 25 teachers a tour to Dubai where they would also engage in a shopping spree.

While in Dubai, the United Arab Emirates (U.A.E) each of them would be awarded a car worth Sh16 million plus a laptop. This means that a total of Sh400 would be spent for car purchase only. The teachers who are departing today on an Emirates flight would spend one week in the Gulf. The major objective of taking the teachers to Dubai is to give them an opportunity to widen their experience with their counterparts in the U.A. E.
Thadeo Mutembei, the director of St Mark Secondary School , told the 10th graduation ceremony at the school recently that he decided to take the teachers to Dubai as part of a study tour, something that would boost their working morale.

About 193 Form Four students graduated during the ceremony. “ I want to boost the morale of my teachers so that they can improve the performance in my schools,” the director underlined.

He said he had no plan to give priority in employing teachers from foreign countries since those from Tanzania were also capable of delivering quality service in his schools.

The noted entrepreneur owns four secondary schools located in Dar es Salaam, namely St Mark, St Mathew, St Victory and Ujenzi.

In an ongoing campaign of tracking illegal immigrants, his schools were not spared as government officials stormed in, taking away one teacher for questioning, an incident about which the director apologised at the graduation ceremony.

On her part St Mark’s Headmistress Leticia Joseph said in the past five years the performance of the school had improved tremendously, reaching a pass rate of 97.4 per cent, enabling many students to join A-level studies and technical institutions. The headmistress raised concern on the increase in the number of text books, saying the situation has been confusing students.

Dar es Salaam regional education officer Bernadetha Thomas, who was chief guest at the ceremony, said the government had learnt a lesson following the massive failures of form four students in national examinations last year, promising that such situations would not recur.

The director was yesterday flagging off his employees for their captivating trip to the Gulf, at St Victory Secondary School. At the graduation ceremony, he urged other employers to take up the idea of motivating their employees.

Observers said this might be the first time a local employer moves to motivate employees in that manner. A number of experts have a feeling that teachers, especially those in public schools need to be motivated considering that they face hardships in their conditions of work.
By Jimmy Mfuru
THE GUARDIAN ON SUNDAY

Tangazo: Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya waTanzania DMV

waTanzania DMV

MINISTRY OF ENERGY TO CANCEL MINING LICENCES

The government has put 102 companies on notice that it will withdraw their dormant mining licences, which were awarded between 2006 and 2012.

The licence holders have a month to show why they should not surrender the permits, minister for Energy and Minerals Sospeter Muhongo confirmed yesterday.

“They have up to October 9 to operationalise the dormant licences or the government will repossess and give them out to companies capable of rolling out the mining activities for which they were issued,” he told The Citizen on Saturday.

Sections 36 and 52 of the mining code provide for prospecting work to begin within three months of receiving mining rights. The firms must also stick to mining operations.

Permanent Secretary Eliakim Maswi issued the notice on Monday in a move seen as a clampdown on individuals who get mining licences only to turn around and hawk them to international prospecting firms for profit running into hundreds of millions of shillings.

Many of the speculators are influential politicians, businessmen and well-heeled individuals out to profiteer from the country’s huge mineral deposits. There has been widespread criticism of the manner in which the licences are given out, with claims of corruption.

Yesterday, Mr Muhongo said 98 per cent of the 102 licences are owned by Tanzanians who cannot develop them. Mr Maswi put the figure in Dar es Salaam at 94 and one in Boston in the US. The rest are spread in other areas of the country.

The government is concerned about the loss of revenue through hoarding of the licences, according to the minister.

At Mererani, for example, locals own 597 licences but only 10 pay taxes. Some of them sell to foreigners. Mr Muhongo reiterated that those who fail to implement the government’s order will have their mining blocks revoked.

In recent days, the minister and influential businessman Reginald Mengi have gone head to head over the ministry’s stance on gas, fuel and mining block licences.

Mr Mengi has pushed for a delay in issuing gas exploration licences, arguing that new policies should first be aligned with local participation and ownership in the lucrative industry.

But the minister has advanced the view that licences should be granted to those with the capital and technical know-how to develop the sector within the set deadlines and in keeping with national growth objectives.
THE CITIZEN

Clouds FM Wanawaibia Watanzania kwa Kutumia Ujumbe Mfupi wa Simu..!

 
Kampuni ya Clouds media kupitia makampuni yake ya clouds fm na clouds Tv wamebuni mbinu ya kuwaibia watanzania ambao wengi hawana uwelewa mkubwa wa matumizi ya teknolojia ya mawasiliano kwani wanakutumia ujumbe mfupi unaohusu shughuli za burudani wanazozifanya kisha wanakukata hela,pasipo wewe mpokea ujumbe wa simu kujiunga na huduma hizo kiasi wanachokata ni Tsh 150.Hili suala ni very sensitive kwani nimejaribu kuwapigia simu watu wa huduma kwa wateja na kuwalalamikia wao wamesema hawajui kitu zaidi ya kunishauri nitume neno STOP kwenda number 15556 Ili kusitisha ujumbe huo ambao unaiba pesa za watanzania,suala la kujiuliza hapa ni kuwa mimi ni mwelewa wa mabo ya mawasiliano je kwa mjomba wangu aliyepo kule kijijini Lukuredi kama atakuwa anatumiwa ujumbe na hawa watu kila siku na anakatwa hela pasipo ridhaa yake hawa watu watakuwa wanatengeneza mabilioni mangapi ya pesa?.Ufuatao ni copy ya ujumbe mfupi ambao hii kampuni inautuma ovyo kwa watanzania na kuwakata hela bila ridhaa yao

"CLOUDS TV:Angalia mkali wa ngolongolo Diamond Platnumz akiwasha moto Fiesta 2012.Diamond amewakilisha Tabora, Dodoma.SIMU.TV;Bofya; http://db.tt/CXiJhfHZ "
Nakala
i)Joseph Kusaga (Clouds media Group)
ii) Makamba J (Naibu waziri)
JamiiForums
>>> Bofya

Padre wa Kanisa Katoliki Zanzibar Anselmo Mwan'gamba Amwagiwa Tindikali (Video)

Kwa mara nyingine Zanzibar imeshuhudia tukio la kumwagiwa tindikali ambapo watu wasiojulikana wamemwagia tindikali Padri wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mpendae,Padri Anselmo Mwan'gamba na kumjeruhi sehemu ya uso na mwilini.

Behind the Rhymes of Khaligraph Jones #theTrend

Larry Madowo spoke to Brian Robert Ouko otherwise known as Khaligraph Jones, the HipHopper about his life and music.

Ottomatic and Khaligraph Jones - Beat goes on (Feat. Shamir)

KAMATA FURSA TWENDZETU KWA VIJANA SEMINA ILIYOFANYIKA DODOMA

Mrisho mpoto
Msanii mahiri wa Kughani Mashairi kwa mtindo wa kisasa kabisa,Mrisho mpoto akizungumza mbele ya sehemu ya wakazi wa Mkoa wa Dodoma na vitongoji vyake waliojitokeza mapema leo asubuhi kwenye semina ya kamata Fursa twendzetu,iliofanyika ndani ya moja ya ukumbi wa hotel ya Africans dream,iliyoko nje kidogo ya mji wa Dodoma. Semina ya Kamata Fursa twendzetu inayoratibiwa na Clouds Media Group,imekwishafanyika mikoa zaidi ya mitano ikiwemo Kigoma,Tabora,Singida,Mtwara,Mbeya,Iringa sambamba na leo ndani ya Dodoma,ambo semina hizo zote zimeonesha mafanikio makubwa kwa vijana kwali walikuwa wakijitokeza kwa wingi kwenye ushiriki.
Sehemu ya washiriki wa semina hiyo ilipokuwa ikiendelea mapema leo asubuhi.
KAMATA FURSA TWENDZETU
KAMATA FURSA TWENDZETU
Wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye semina hiyo ya kamata fursa twendzetu,mapema leo asubuhi mkoani Dodoma.
KAMATA FURSA TWENDZETU
Mwakilishi wa NSSF-Makao Makuu,Salim Khalfan akifafanua masuala mbalimbali yatokanayo na faida za kujiunga na shirika hilo la NSS,ndani ya semina ya kamata fursa twendzetu iliofanyika mapema leo kwenye moja ya ukumbi wa hotel ya Africans dream,iliyoko nje kidogo ya mji wa Dodoma.
kwa picha zaidi bofya soma zaidi

KAMATA FURSA TWENDZETU
Sehemu ya ya watu wakifuatilia kwa umakini yaliyokuwa yakijiri kwenye semina hiyo.
KAMATA FURSA TWENDZETU
Meneja wa NSSF mkoani Dodoma,Bwa.Kirondera Nyabuyenze akizungumza fursa mbalimbali zitokanazo na shirika la NSSF,Nyabuyenze amewataka watu mbalimbali wajitokeze kwa wingi kujiunga na NSSF,ili kujipatia fursa mbalimbali zikiwemo mikopo,matibabu na mambo mengiyo mbalimbali.

Mwakilishi wa Kampuni ya Maxmalipo,Renard Munuri akizungumza kwenye semina ya Kamata Fursa Twenzetu kwa vijana,kuhusiana na masuala mbalimbali yanayofanywa na kampuni yake katika kusaidia huduma za jamii,ndani ya moja ya ukumbi wa hotel ya Africans dream,iliyoko nje kidogo ya mji wa Dodoma.
KAMATA FURSA TWENDZETU
Mmoja wa Watangazaji mahiri wa Clouds FM,akizungumzia fursa mbalimbali alizokumbana nazo na namna alivyozifanyia kati na kujipatia sehemu ya mafanikio katika kupambana na maisha.Semina ya Kamata Fursa twendzetu inayoratibiwa na Clouds Media Group,imekwishafanyika mikoa zaidi ya mitano ikiwemo Kigoma,Tabora,Singida,Mtwara,Mbeya,Iringa sambamba na leo ndani ya Dodoma,ambo semina hizo zote zimeonesha mafanikio makubwa kwa vijana kwali walikuwa wakijitokeza kwa wingi kwenye ushiriki.
KAMATA FURSA TWENDZETU
Baadhi ya wasanii ambao wamenufaika mara baada ya kujiunga na Shirika la NSSF,shoto ni Queen Doreen na Mwasiti wakijadiliana jambo na mdau Phillipon mapema leo,wakati semina ya Kamata fursa twendzetu ilipokuwa ikiendelea.
KAMATA FURSA TWENDZETU
Sehemu ya wakazi wa mji wa Dodoma wakiwa wamejitokeza mapema leo asubuhi kwenye semina ya fursa kwa vijana
KAMATA FURSA TWENDZETU
Sehemu ya meza kuu ya watoaji mada wakishangilia jambo.