Pages

Kobe Hoofin' It Around Italy With Busted Achilles

Kobe BryantWith his rehab in full swing, Kobe Bryant proved his achilles is healthy enough for tourist activity this weekend by strolling around Italy with his family.

Kobe -- along with his wife Vanessa and their daughters Natalia and Gianna -- were spotted walking around Capri like regular people.

Kobe recently told an Italian media outlet that he's in country for vacation -- but found some time to do some rehab at the Milanello Sports Centre, the training facility for famed Italian soccer club A.C. Milan.

As for Kobe and Vanessa ... we broke the story, VB called off the divorce back in January ... and it appears the two are just like peas and carrots again. TMZ reports

Promo ya Mkasi with Jokate

Young D -KIJUKUU (Audio)

Young D

Wake wa Viongozi wa Uamsho Wafunguka.

Viongozi wa Uamsho
Wake wa viongozi Jumuiya ya Uamsho Zanzibar, wameiomba serikali kuitazama kesi inayowakabili viongozi hao kwa jicho la uadilifu, haki na sheria ili kuonesha dhana ya utawala bora.

Wakizungumza na waandishi wa habari katika kongamano la wanawake wa Kiislamu lililofanyika msikiti wa Mbuyuni, kinamama hao wamelalamikia kesi hiyo kuchukua muda mrefu huku ikiwa hakuna hatua yoyote muhimu inayochukuliwa ili haki itendeke.

Wametaka vyombo vya sheria vifanye kazi kwa maadili, hasa ikizingatiwa kwamba Zanzibar ni mshiriki wa Muungano wa Tanzania ambayo ni mwanachama wa taasisi mbalimbali za kulinda na kuheshimu haki za binadamu ulimwenguni.

“Hatukusudii kuingilia kazi za mahakama, bali tunaeleza hali halisi ya uvunjwaji wa sheria na katiba ya nchi kwa vyombo vya sheria kufanya kazi kwa utashi bila ya kuzingatia haki za wanachi mbele ya sheria”, walidai wanawake hao.

Walidai kuwa, kitendo cha kunyima haki kinaweza kuitia doa kubwa mahakama na serikali mbele ya macho ya kimataifa.

Aidha, walitaja sababu za kuwekwa ndani waume zao kuwa ni harakati zakuongoza umma wa Wazanzibar kudai haki yao ya msingi juu ya hatima ya Zanzibar kuwa nchi yenye uhuru wa kujiamulia mambo yake.

Wameeleza kusikitishwa kwao kwa kusema kuwekwa ndani kwa waangalizi hao wa familia zao, kumewaathiri sana kisaikolojia na kiuchumi.

Pia wamesema mwenendo mzima wa taaluma za Kiislamu ambazo viongozi hao walikuwa wakifundisha katika madarsa mbalimbali kwenye misikitini na vyuo, umeathiriwa na kushikiliwa kwa viongozi hao.

Kwa hivyo wamevitaka vyombo vya sheria kufanya haki katika maamuzi yao ili kudumisha amani na utulivu uliopo pasi na kutia dosari serikali ya umoja wa kitaifa iliyowalea Wazanzibari pamoja.

Kupitia kongamano hilo, wanawake hao wameviomba vyombo vya sheria, kuwaruhusu viongozi hao kuonana na wake na ndugu zao wakati wanapofikishwa mahakamani kwa kusikilizwa kesi yao.

Katika hatua nyengine, kinamama hao wameunda kamati ya kufuatilia na kuratibu mwenendo wa kesi pamoja na kuonana na watendaji wa haki za binadamu.

East Africa Chamber of Commerce Trade Conference, Invitation

 East Africa Chamber of Commerce Trade Conference

Country Wiz Ft G Nako - Watch Me Mastering (Audio)

Country Wiz Ft G Nako - Watch Me Mastering

Quote of the Day

Quote

Wauza `Unga` Waiteka D`Salaam Airport

Oliver TamboNidhahiri kwamba Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), sasa ni kitovu cha kusafirisha dawa za kulevya nje ya nchi.
Katika kipindi cha takribani wiki mbili tu, Watanzania wanne wamekamatwa ughaibuni wakiwa na shehena ya dawa hizo ambazo walisafirisha kutoa Tanzania kwenda nje kupitia uwanja huo bila ya kukamatwa.

Mara ya kwanza walikuwa ni wasichana wawili, Agnes Jerald (25) na Melisa Edward (24), ambao walikamatwa Afrika Kusini na kushtakiwa nchini humo.
Walikamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo wakiwa na shehena ya kilo 150 ya dawa aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 6.8. Wasichana hao walikamatwa Julai 5, mwaka huu baada ya kuwasili Johannesburg wakitokea Tanzania wakisafiri kwa ndege ya Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) na walikamatwa na Maofisa wa Mamlaka ya Mapato ya nchi hiyo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo, uliopo eneo la Kempton Park.

Ijumaa wiki hii, Watanzania wengine wawili, walikamatwa Hong Kong wakiwa na dawa za kulevya aina ya cocaine na heroine zenye thamani ya bilioni 7.6 akiwamo mmoja aliyekamatwa akitokea Dar es Salaam kupitia Dubai hadi Honh Kong.

Matukio haya yote yanatokea wakati wakuu wa Uwanja wa ndege wa Julius Nyerere zinakopitishwa wakiwa hawana cha kusema juu ya uharamia huo unaotokea kwenye kitovu cha mawasiliano cha nchi.

Jana, Kamanda wa Polisi Kikosi cha Viwanja vya Ndege Nchini, Deusdedit Kato, alisema jalada la upelelezi kuhusu tukio la kukamatwa kwa wasichana Afrika Kusini litapelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) leo ingawa hakuwa tayari kutaja watuhumiwa ni nani hasa wanaoshirikiana na wafanyabiashara ya dawa hizo.

Kato alisema hawezi kutaja majina ya watu waliobainika kwa sababu kilichofanyika ni uchunguzi tu na kwamba DDP ndiye mwenye mamlaka ya kuamua juu ya uchunguzi huo.

“Siwezi kukuambia ni nini kimepatikana katika uchunguzi wala kutaja majina ya watu, kwa kuwa mimi ninapeleka nilichokichunguza kwa sababu naweza kukuambia lakini ikawa sio hivyo kwani huu ni uchunguzi tu,” alisema.

Aliongeza: “Naweza kupeleka jalada langu la uchunguzi kwa DDP lakini kutokana na utalaam wake akagundua kuna mapungufu, hapo tayari nitakuwa nimepotosha umma. Lakini pia akiona upelelezi unajitosheleza yeye ndiye anaweza kuamua kupeleka Mahakamani.”

Kuhusu taarifa za kukamatwa kwa Watanzania wengine na dawa za kulevya Julai 26, mwaka huu huko huko mjini Hong Kong, Kato alisema bado wanafanya jitahada za kupata kwa undani taarifa hizo.

“Na mimi nimesikia, lakini hatujapata taarifa zaidi ili kujua majina yao na kama kweli ni Watanzania. Inakuwa ngumu kupata taarifa kwa sababu aina ya mawasiliano wanayotumia hawa Polisi wa Kimataifa (Interpol ) ni tofauti na ya kwetu kwa hiyo tunategemea wao ndiyo watupe taarifa,” alisema Kato.

Naye Waziri wa Uchunguzi, Dk. Harrison Mwanyembe, ambaye amejipatia sifa za utendaji katika siku za hivi karibuni, kwa kuendesha timua timua katika taasisi zinazosimamiwa na wizara yake kwa tuhuma za uzembe, amekuwa kimya na pengine kukwepa kabisa kutia mguu katika sakata la dawa za kulevya JNIA.

Wiki iliyopita NIPASHE lilimtafuta Dk. Mwakyembe mwenye dhamana ya Viwanja vya Ndege nchini kujua ni hatua gani amechukua, lakini alijibu kwamba hana taarifa za kina kuhusu sakata hilo.

Uharamia huo wa dawa za kulevya umempa pia kigugumizi Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishna Robert Manumba, ambaye amekwepa kuzungumzia sakata hilo na kusema liko kwa Kamanda wa Polisi, Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Geofrey Nzowa.

Kamanda Nzowa alipoulizwa alisema upelelezi bado unaendaelea kubaini mambo mbalimbali yaliyoko nyuma ya tukio hilo.

Alipoulizwa ikiwa Polisi wamebaini mmiliki pamoja na maofisa walioruhusu kupitishwa kwa dawa, Nzowa alisema uchunguzi unaangalia mambo mengi na ndiyo huo utakuja na taarifa kamili.

Taarifa kutoka Hong Kong za Ijumaa wiki iliyopita zinaeleza kwamba, maofisa ushuru wa Uwanja wa Ndege wa Hong Kong (HKIA), walimkamata kijana mmoja mwenye umri wa miaka 26 akitokea Tanzania na alikuwa na dawa za kulevya aina ya heroin kilo 1.6 zenye thamani ya Sh. bilioni 1.5, kwenye mzigo wake wa mkononi.

Taarifa zilieleza kwamba baadaye jioni siku hiyo hiyo, maofisa hao walimkamata Mtanzania mwingine mwenye miaka 45 ambaye alipelekwa hospitali na kutolewa gramu 240 za dawa za kulevya aina ya heroin.
Taarifa zaidi zilieleza kuwa Mtanzania mwingine mwenye miaka 28 alikamatwa akiwa na kilo 2.03 za cocaine.

Takwimu zinaonyesha kumekuwa na wimbi kubwa la Watanzania wanaojiingiza katika biashara haramu ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi na kwamba, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, watuhumiwa 10,799 walikamatwa kwa kujihusisha na uharamia huo.

Katika kipindi hicho, Watanzania 240 walikamatwa katika nchi za Brazil, Pakistan na Afrika Kusini, na kuharibu taswira ya nchi na kusababisha Watanzania wasio na hatia kupata usumbufu na masharti magumu wanapotaka kusafiri kwenda nchi mbalimbali duniani.
NIPASHE

Watch Mkasi with Mh A.Mwinyi

Vunjika Mbavu KinaiJeria Style