Pages

MAREKANI YAIONYA RWANDA KUACHA MARA MOJA KUWASAIDIA M23

 RWANDA
(Reuters) - The United States on Tuesday called on Rwanda to end support for M23 rebels in neighboring Democratic Republic of Congo, saying there was evidence Rwandan military officials were involved. "We call upon Rwanda to immediately end any support for the M23 (and) withdraw military personnel from eastern DRC," State Department spokeswoman Jen Psaki said.
She declined to say whether Rwandan President Paul Kagame was implicated. "I wasn't speaking to Kagame himself," she added.

The call comes two days before U.S. Secretary of State John Kerry leads a special session of the United Nations Security Council on Africa's Great Lakes region
Psaki said the concerns followed a "credible body of evidence" in a recent report by Human Rights Watch that said M23 rebels in Congo were to blame for executions, rapes and forcible recruitment of men and boys while receiving support from Rwanda.  RWANDA RWANDA
M23 began taking parts of eastern Congo early last year, accusing the government of failing to honor a 2009 peace deal.
(Reporting by Lesley Wroughton; Editing by Doina Chiacu)

ASKARI POLISI WATIMULIWA CHUONI HUKO MOSHI

ASKARI POLISI Wanafunzi 117 wa Polisi, wamefukuzwa katika Chuo cha Taaluma na Mafunzo ya Polisi (MPA), kilichopo Manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro.

Waliotupiwa virago na kufutwa kwenye kozi hiyo ni wale waliopoteza sifa za kuendelea na mafunzo ya kijeshi baada ya kukutwa na makosa ya utovu wa nidhamu, utoro na matatizo ya kiafya.

Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Matanga Mbushi, ambaye ni mkuu wa chuo hicho aliliambia NIPASHE katika mahojiano maalumu kwamba, waliotimuliwa chuoni ni kati ya askari wanafunzi 3,189 waliokuwa wamesajiliwa kuanza mafunzo ya kijeshi katika chuo hicho, Oktoba 25 mwaka jana.

Kati yao askari 115 ni wale wa Polisi na askari wawili wanatoka katika Idara ya Uhamiaji iliyopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani.

Kufukuzwa kwa wanafunzi hao , kuna akisi moja kwa moja jinsi menejimenti ya chuo hicho ilivyojipanga upya kupunguza wimbi la baadhi ya askari walioko kazini na ambao wanalipaka matope jeshi hilo kutokana na kupotoka kimaadili kwa kutaka kujinufaisha kimaslahi.

Askari hao walikuwa waungane na wenzao ambao wanatarajiwa kuhitimu mafunzo ya awali ya polisi na uhamiaji, Julai 26 mwaka huu baada ya kupatiwa mafunzo ya medani za kivita. Mgeni wa heshima atakayeshuhudia kuagwa kwa askari 3,092 ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi.

Kamishna Mbushi alisema askari hao pamoja na mambo mengine wamepatiwa mafunzo maalumu ya utunzaji wa amani ya nchi iliyopo, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT), Haki za Binadamu, Masuala ya mtambuka (Cross cutting issues), Usimamizi wa majanga na Usimamizi wa kazi za Polisi.

Mafunzo mengine ni pamoja na Polisi Jamii, Sheria ya ushahidi, Sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai, Upelelezi wa makosa ya jinai, Usalama barabarani na stadi za kazi.

Taarifa za awali kutoka ndani ya chuo hicho, zinaeleza kuwa mahafali hayo ya Polisi yatatanguliwa na medani za kivita yatakayofanyika Julai 25 huko katika Kijiji cha Kilele-Pori, Wilaya ya Siha.
HABARI LEO

Royal Baby. Here is the Family Tree

Royal baby: Family tree

Kipanya Leo

Kipanya

Final call for artists - 31 July deadline! -Sauti za Busara

BUSARA PROMOTIONS
Are you an African musician or group? Applications for local and international artists who want to perform at the 11th edition of Sauti za Busara are open until 31st of July. The festival will be held from 13-16 February 2014. The online application form is on our website HERE or a paper version can be collected at our offices in Maisara, opposite Golf Club, in Zanzibar.
Over the past ten years we have had more than 250 groups perform, in all musical genres, always 110% live.
Note that we receive many applications each year and we take the time to review each application carefully. Please be patient as we review the applications and we will inform applicants as soon as we can after the selection committee meets in early August.
Your application must include the following:
A completed online or paper form including a short biography (max 1000 words).
One or two recent recordings (CD or DVD)
One or two photographs (JPG or paper)
Please send your recordings, photographs and any other material to our office address below:

BUSARA PROMOTIONS PO BOX 3635 STONE TOWN, ZANZIBAR, TANZANIA
Please note we will not accept applications and application materials after 31 July. Make sure we have received your full application (including hard copies of recordings) by that date.
 For more information see www.busaramusic.org/callforartists

Dj Choches/tecdjs -Bongomania 5 (Audio Mixing)

Dj Choches/tecdjs,Bongomania 5, ,Audio Mixing

TMK Wanaume Family - Tunafurahi (Audio)

MJANE ALIYEFUKUZWA KATIKA MSIBA WA MWANAJESHI WA JWTZ AJITOSA TENA KUHUDHURIA MAZISHI

FAMILIA ya Marehemu, Fortunatus Msofe, ambaye ni mmoja wa wapiganaji wa JWTZ, waliofia Darfur, wamemzuia aliyekuwa mchumba wake Amina Juma kushiriki katika mazishi na kumfungia mlango wa nyumba ya marehemu asiingie ndani mara tu baada ya taarifa za kifo cha marehemu kuwafikia.
Hata hivyo Amina amelazimika kwenda Tanga kushiriki shuguli za mazishi ya marehemu pamoja na kwamba familia ya marehemu haitaki kumuona katika msiba huo.
JWTZ
Akizungumza na gazeti moja la kilasiku la kiswahili nchini Tanzania, Amina alisema kwamba ingawa awali alikata tamaa ya kumzika mwenzake, lakini jana aliamua kwenda Tanga kuhudhuria mazishi na kwamba hatua hiyo ilikuja baada ya kujishauri sana.

Baba wa marehemu, Wilbad Msofe aliiambia gazeti hilo kutoka Kange, Tanga kuwa alishangazwa na hatua ya Amina kutowafahamisha kuhusu msiba huo. Alisema hiyo ndiyo sababu za yeye kuamua kutaka mwanawe apelekwe Kange kwa mazishi.

Akizungumza na gazeti hilo akiwa njiani kwenda Kange, Amina alisema: “Nilikuwa ninataka sana kumzika mwenzangu lakini ile hali ilikuwa imenichanganya pamoja na kwamba nilishauriwa, sasa nimekata shauri nakwenda Tanga.

“Najua kuna kitu hapa, lakini ‘Fortu’ kwa kuwa nilikuwa naye, na wana ndugu wa upande wa wake wameshanikana, mimi nitamzika tu mwenzangu na kurudi,” alisisitiza.

Miili ya wapiganaji hao iliagwa jana katika Makao Makuu ya Jeshi, yaliyoko Upanga na Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu, Mkuu wa Majeshi, Davis Mwamunyange, makamanda na wanajeshi walishiriki kuwaaga wanajeshi hao.

Akizungumza kwa masikitiko na huku sauti ikiwa imemkauka kutokana na kulia muda mrefu, Amina alisema: “Siwazii mtafaruku uliopo, moyo umenituma kwenda kumzika mume wangu, niliwaza usiku kucha na leo (jana) Jumatatu asubuhi nikaamua kwenda Tanga.”

“Msofe amekufa tulikuwa tuna mipango mingi, tulipanga harusi kubwa lakini haikuwahi kufanyika, niliongea naye alfajiri ya Jumamosi ya Julai 13, akaniambia tutaongea baadaye maana wanakwenda kwenye operesheni...

“Unajua tuliishi maisha ya kipekee sana tulipendana kiukweli hata majirani tuliokuwa tukiishi nao Mbezi na Visiga wanajua hilo na wengi walikuwa wakinisihi sana nisije kumuudhi huyu kijana.

"Nafsi inauma sana. Nawashangaa wazazi wake kwa kunikana"

NGURUMO ANATESEKA NA MARADHI KITANDANI,WENZAKE WADAIWA KUMTENGA

Muhidin Maalim Gurumo.
KILA binadamu hutamani kuwa na mwisho mzuri. Hakuna apendaye kupatwa na misukosuko ya kiafya, awe dhaifu hata kushindwa kutoka ndani angalau akajitafutie riziki.
Waja hupanga na kupangua tu lakini mwamuzi wa leo na kesho ni Mungu aliye juu! Tafakari leo upo vema, una siha njema, tena barabara kabisa. Ikifika nyakati upo ndani huwezi kutoka itakuwaje? Usimcheke anayelia leo, hujui kesho yako itakuwaje.
Muhidin Maalim Gurumo, 72, alipata kuwa mwanaume shupavu sana. Mungu akamjalia kipaji cha muziki, akabarikiwa nyota ya kupendwa. Asimamapo jukwaani basi mashabiki ni hoihoi na raha tupu.
Tangu miaka ya 1960 kama ungethubutu kutamka humjui Gurumo, ungeonekana mshamba mwenye tongotongo nyingi, mjini ungechekwa. Alikuwa staa mkubwa sana wa muziki. Jina lake limebaki juu kuanzia nyakati hizo mpaka sasa.
Ni kamanda hodari, aliyeifanya Bendi ya Msondo ‘Msondo Ngoma’ ipate heshima kubwa mpaka ikaitwa Baba ya Muziki Tanzania. Tungo zake nyingi ni lulu ambayo haitafutika kamwe. Kinachoumiza kwa sasa ni kuona Gurumo hawezi tena kusimama jukwaani.
Hana uwezo wa kutoa burudani iliyozoeleka. Ile sauti yake yenye mawimbi haipatikani tena katika majukwaa ya muziki. Kikubwa kinachotesa moyo ni kwamba Msondo ambayo ni bendi yake, akimiliki hisa za kutosha kama mmoja wa wamiliki, haina msaada wowote kwake.
Mzee analalamika. Msondo hii ndiyo ile aliyoivusha kupitia majina ya Nuta, Juwata,  na Ottu, ikiwa inamilikiwa na Chama cha Wafanyakazi. Hakujua kama mambo yangekuwa hivi leo.
Itambulike kuwa yeye akiwa na wenzake kama marehemu Shaaban Mhoja Kishiwa  maarufu kama ‘TX Moshi William’, Saidi Mabera, marehemu Suleiman Mbwembwe, Othuman Momba, Joseph Maina na wengineo, ndiyo waliounganisha nguvu na kuimiliki, baada ya chama cha wafanyakazi kujiondoa katika uendeshaji wa bendi.
Mzee analia ukata. Maradhi yanamtesa lakini shida za dunia na msongo wa mawazo ambao anao kutokana na kutengwa na wenzake, ni hatari kubwa inayofupisha siku zake za kuishi.
Muhidin Maalim Gurumo.ANAUMWA NINI? ALIANZA KUUMWA LII?
Katika mahojiano na mwandishi wetu, nyumbani kwake, Ubungo Garage, Dar es Salaam, Gurumo anasema: “Ninasumbuliwa na maradhi ya moyo. Nakumbuka  nilianza kuumwa yapata miaka mitatu iliyopita. Kipindi hicho ndipo nilipatwa matatizo ya kushindwa kuimba kwa sauti ya juu.
“Kila nilipojitahidi kuimba kwa sauti ya juu, nilijikuta nikichoka sana. Niliendelea...

JENGO LA OFISI YA MALKIA WA NYUKI MLEZI WA SIMBA LABOMOLEWA

Rahma Al Kharusi, maarufu kama Malkia wa Nyuki.
UTEKELEZAJI wa amri ya Waziri wa Ujenzi na Miundombinu, John Pombe Magufuri, umemuathiri Mlezi wa Simba, Rahma Al Kharusi, maarufu kama Malkia wa Nyuki, baada ya moja ya ofisi zake jijini Dar es Salaam kubomolewa.

Ofisi hiyo ambayo ilikuwa inaendesha shughuli za kampuni ya kuuza mafuta ya RPB Oil inayomilikiwa na Malkia wa Nyuki, imebomolewa.

Bomoabomoa hiyo ya Magufuri imepamba moto katika Barabara ya Old Bagamoyo na majumba kadhaa yamebomolewa kwa kuwa kuna ujenzi wa kuitanua barabara hiyo.

Ofisi ya Malkia wa Nyuki ilikuwa katika ghorofa ya kwanza ya jengo la Green Acres, katikati ya makumbusho na Victoria na imevunjwa.

Ingawa jengo hilo halijavunjwa lote, lakini sehemu ya ofisi ya RPB Oil iliyokuwa upande wa barabarani imebomolewa yote.
Malkia ndiye mwanamama aliyetikisa katika soka mwishoni mwa msimu uliopita baada ya kuilipia Simba zaidi ya Sh milioni 70 kwenda kuweka kambi nchini Oman.

Akalipa tena zaidi ya Sh milioni 50 kumpa kocha Milovan Cirkovic aliyekuwa anaidai Simba bila ya mafanikio. Baada ya hapo, Malkia amekuwa kimya na mashabiki wengi wamekuwa wakihoji kutaka kujua aliko.

Taarifa zinaeleza yuko nchini Oman anakoendelea na biashara zake, lakini ndugu yake mwingine alisema amebanwa na majukumu ya kampuni zake nchini Marekani.
 Na Saleh Ally