Hatimaye Absalom Kibanda Azungumzia Mkasa Wake
Aidha amesema kabla ya kushambuliwa na kujeruhiwa vibaya alikuwa muoga sana na kwamba hakupata kujua kama yeye ni jasiri kwa kiwango hicho.
Kibanda alisema hayo jana wakati akizungumza Dar es Salaam katika kipindi cha Jenerali On Monday na kuongeza kuwa kalamu yake ndiyo iliyomfikisha hapo na kwamba bado atajisemea mwenyewe huku akisema kweli daima.
Kibanda ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa New Habari Limited (2006), alijeruhiwa vibaya katika mkasa uliotokea Machi 6, mwaka huu na kumwacha na ulemavu wa jicho, kidole na mifupa kadhaa mwilini kuvunjika.
“Nilikuwa muoga sana kabla ya kupatwa madhala haya, nilikuwa nikiwaza jambo mara mbilimbili na sikupata kujua kama mimi ni jasiri kiwango hiki…kwani hata maneno ya madaktari waliokuwa wakinihudumia yalinifariji kuwa hata shinikizo la damu na sukari viko katika hali nzuri,” alisema Kibanda na kutaka uchunguzi zaidi ufanyike.
Alisema zipo taarifa mbalimbali za kutaka kupotosha ukweli kuhusu yeye lakini ukweli utabaki kuwa kweli na kwamba yapo mambo ambayo atayafanya tofauti na ilivyokuwa awali.
“Katika miezi mitatu niliyokuwa nikipatiwa matibabu nchini Afrika Kusini zipo lugha nyingi za kishabiki ziliandikwa…ni wakati wa kuchunguza kwa kina na kusema ukweli,” alisema Kibanda na kuongeza kuwa leo (jana) ni siku 100 tangu alipofanyiwa tukio hilo, lakini hakuna aliyekamatwa wala kufikishwa mahakamani. Kuhusu kupata ushirikiano katika shauri lake, alisema amekuwa akipata mawasiliano kutoka kwa viongozi mbalimbali wakiwemo pia viongozi wa ulinzi na usalama wa Taifa ambao wanachunguza suala hilo.
“Maofisa wa polisi wamekuwa wakiwasiliana nami na hata nilipokuwa Afrika Kusini Jeshi la Polisi lilimtuma ofisa wake na alifanya mahojiano nami kuhusu tukio hili,” alisema Kibanda na kusisitiza kuwa ifikie wakati serikali iwe inajali pindi yanapotokea matukio ya aina hiyo.
Aidha alisema tukio alilofanyiwa ni la kihalifu na anaamini kuwa aliumizwa kwa misimamo yake ya kazi, lakini bado anatoa wito kwa wadau mbalimbali kuendelea kuchunguza tukio hilo.
Kibanda alisema yapo mambo ambayo yalipindishwa kuhusu tukio hilo na kwamba atajisemea mwenyewe.
Akihitimisha kipindi hicho, Muandaaji, Jenerali Ulimwengu alisema matukio kama hayo yanapotokea yana tabia ya kukua, kusambaa na mwishowe kuota meno marefu na kuyaondoa huwa hayawezekaniki tena, hivyo matukio kama hayo yazuiwe yasijirudie.
VOTE FOR SPORAH SHOW
The Sporah Show is proud to have been nominated by the British Young Business Awards in the Best Social Enterprise category which will take place on the 12th August 2013.
Please vote for Sporah at
http://www.invinciblebusiness.com/british-young-business-awards/voting/
or you can vote via http://www.sporah.com/
DK. BILAL AKUTANA NA MKURUGENZI WA SHIRIKA LA UKIMWI LA KIMATAIFA ABUJA NIGERIA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Ukimwi, UNAIDS, Michel Sidibe, baada ya mazungumzo yao walipokutana katika Mkutano wa 12 wa Afrika unaojadili magonjwa ya Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria (Abuja +12) uliofanyika jana Julai 15, 2013 na kufunguliwa na Rais wa Nigeria Dkt. Goodluck Jonathan, mjini Abuja Nigeria na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Nchi za Afrika.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Ukimwi, UNAIDS, Michel Sidibe, wakati walipokutana katika Mkutano wa 12 wa Afrika unaojadili magonjwa ya Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria (Abuja +12) uliofanyika jana Julai 15, 2013 na kufunguliwa na Rais wa Nigeria Dkt. Goodluck Jonathan, mjini Abuja Nigeria na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Nchi za Afrika.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan na baadhi ya Marais wengine baada ya kufunguliwa mkutano wa 12 wa Afrika unaojadili magonjwa ya Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria (Abuja +12) uliofanyika jana Julai 15, 2013 na kufunguliwa na Rais wa Nigeria Dkt. Goodluck Jonathan, mjini Abuja Nigeria na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Nchi za Afrika.
Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais
Jackie Chan Adondosha Bonge la Party

Muigizaji wa filamu kutoka bara la Asia, Jackie Chan leo amewafanyia sherehe ya kuzaliwa midori yake miwili ambayo imetimiza umri wa miaka mitatu.
#Ameandika kwenye ukurasa wake wa facebook...

RIPOTI KAMILI KUHUSU MADAWA YA KULEVYA TZ
Na Mwandishi Wetu
WATANZANIA ambao idadi yao inaweza kupita mamia, wameshanyongwa nchini China kutokana na kupatikana na hatia ya kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya.
Ripoti maalum ya madawa ya kulevya, iliyofanyiwa kazi na gazeti hili kwa kukusanya taarifa ndani ya nchi, Afrika Kusini na China kwenyewe, inaweka hadharani siri ya mamia ya Watanzania kunyongwa.
Katika ripoti hiyo, inaonesha kwamba mataifa ya Afrika Kusini na Uganda, yapo mstari wa mbele kuripoti taarifa za raia wao kunyongwa China lakini Tanzania imekuwa ikisuasua.
“Huu ukimya wa serikali yetu, unafanya wengi kukosa taarifa sahihi, matokeo yake wanajiingiza kwenye biashara hiyo haramu ambayo mtu akikamatwa tu China na akikutwa na hatia lazima anyongwe,” alisema Joel Mabruki, mfanyabiashara wa nguo na simu kati ya Tanzania na China.
Mabruki aliongeza: “Kama serikali yetu ingekuwa na utaratibu wa kutangaza kila Mtanzania anayenyongwa China, pengine vijana wengine wangeogopa na baadhi yao wangeacha kabisa. Hivi sasa idadi inaongezeka kwa sababu hawaambiwi ukweli.”
KITENGO CHA MADAWA YA KULEVYA KINAJUA
Kwa mujibu wa Mkuu wa Jeshi la Polisi, Kitengo cha Kuzuia na Kudhibiti Madawa ya Kulevya, Godfrey Nzowa, ofisi yake inazo taarifa kuhusu Watanzania kunyongwa China lakini akatupa mpira kwa Mkurugenzi wa Kuzuia na Kudhibiti Madawa ya Kulevya, Christopher Shekiondo.
“Kuhusu idadi na majina, hilo suala aulizwe mkurugenzi. Ila ukweli ni kwamba Watanzania wengi wanakamatwa China na wananyongwa,” alisema Nzowa.
MAAFA PAKISTAN
Kwa upande mwingine, Nzowa alisema kuwa watu wanaizungumzia sana China lakini ukweli ni kwamba nchi nyingine ambayo inanyonga Watanzania wengi ni Pakistan.
Nzowa alisema kuwa pengine taarifa za Pakistan hazipatikani sana kutokana na mwingiliano wa Tanzania na nchi hiyo, tofauti na China ambayo Watanzania wanakwenda na kurudi kila siku iendayo kwa Mungu.
“Tunaposema madawa ya kulevya ni janga kubwa inafaa ieleweke hivyo. Watanzania wanaonyongwa China na Pakistan ni wengi sana. Tuwe makini juu ya hili na tuzingatie kwelikweli,” alisema Nzowa.
TAARIFA ZA MITANDAO YA KIJAMII
Tofauti na mataifa mengine ambayo ripoti za raia wao kukamatwa na kunyongwa China hutolewa rasmi na balozi zao, hapa Tanzania, habari huenezwa na mitandao ya kijamii.
Mfano; mitandao ya kijamii ndiyo pekee iliyoripoti kuhusu kunyongwa kwa mrembo mwanamitindo (jina tunalo) aliyeshiriki video ya wimbo Twende Zetu wa mwanamuziki Saidi Juma ‘Chegge’, aliyewashirikisha Amani James Temba ‘Mheshimiwa Temba’, Feruzi Mrisho Rehani ‘Ferouz’ na Yessaya Ambilikile ‘YP’.
Vilevile, alipokamatwa aliyewahi kushika nyadhifa za makamu mwenyekiti na katibu msaidizi kwenye Klabu ya Simba (jina tunalo), mitandao ya kijamii iliandika bila serikali kutoa tamko rasmi.
Hata hivyo, kutokana na kukosekana na taarifa rasmi kutoka serikalini, mitandao ya kijamii ilitoa habari zenye kushitua, nyingine ikidai mtu huyo aliyewahi kuwa kiongozi wa Simba alifungwa miaka 70 jela, nyingine ikieleza kwamba tayari alishanyongwa.
MWAKALEBELA ATOA USHUHUDA WAKE
Katibu Mkuu Mstaafu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Frederick Mwakalebela, alipozungumza na gazeti hili, alisema kuwa kati ya mwishoni mwa mwaka 2009 na mwanzoni mwa 2010, alikwenda China katika safari ya kikazi.
“Nikiwa kule, niliambiwa taarifa za Watanzania wengi ambao walinyongwa baada ya kukutwa na hatia ya kujishughulisha na biashara ya madawa ya kulevya,” alisema Mwakalebela.
Alipoulizwa kuhusu kiongozi huyo wa Simba, Mwakalebela alijibu: “Nikiwa China niliambiwa amenyongwa. Niliporudi hapa nchini ndiyo nikasikia amefungwa miaka 70.”
Mwakalebela aliongeza: “Ukweli ni kwamba kwa taarifa nilizopata nikiwa China, Watanzania wengi sana wananyongwa kwa sababu ya madawa ya kulevya. Naweza kusema ni mamia. Ikiwa kwa muda mfupi niliokuwepo pale nimeambiwa karibu watu 10, je mwaka mzima inakuwaje?”
WENGINE WANAPONZWA NA WANIGERIA
Mfanyabiashara Mtanzania, Hashim Rau, ambaye hufanya biashara zake kati ya Tanzania, Afrika Kusini na China, alisema kuwa kuna Watanzania walinyongwa baada ya kuponzwa na Wanigeria.
Rau alisema, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa O. R. Tambo, uliopo nje kidogo ya Jiji la Johannesburg, umewasababisha matatizo Watanzania wengi kutokana na tabia yao ya ukarimu.
Alisema: “Mtanzania anaweza kutoka na biashara yake kuja kuuza Afrika Kusini, baada ya hapo anapanda ndege ya moja kwa moja kwenda China. Akiwa uwanja wa ndege anakutana na Mnigeria muuza madawa ya kulevya.
“Mtanzania anakuwa hana mizigo mingi, kwa hiyo yule Mnigeria anamwomba Mtanzania amsaidie kupitisha begi lake moja kwenye mzani, akidai kuwa yeye mizigo yake ni mingi, anaogopa atatozwa fedha nyingi.
“Kumbe lile begi linakuwa na unga. Sasa Mtanzania kwa kutojua, atakubali, baada ya hapo lile begi litaandikwa jina la Mtanzania. Mbele ya safari kama litavuka salama, Mnigeria atamshukuru Mtanzania na kuchukua begi lake lakini likikamatwa, Mnigeria atakimbia, Mtanzania atabaki na mashtaka ambayo mwisho wake ni kunyogwa China.”
Akisimulia ushuhuda wake, Rau alisema kuwa aliwahi kuombwa msaada wa aina hiyo na Mnigeria mmoja lakini alipotaka kukagua begi lina nini ndani alikataa.
“Alipokataa nikague ndani ya begi kuna nini nami nikamkatalia kumsaidia kwa sababu naujua mchezo wao. Sasa pale uwanjani alikuwepo Mtanzania mwingine mwenye asili ya Tanga (jina tunalo), alipoombwa na yule Mnigeria alikubali.
“Nilijitahidi kumwonesha ishara hakunielewa, mwisho nikamwambia asikubali lakini hakunielewa. Tulipofika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Guangzhou Baiyun, China, yule Mtanga alikamatwa baada ya lile begi kukutwa na madawa ya kulevya mchanganyiko wa heroine, cocaine na methamphetamine.
“Kama kawaida, yule Mnigeria alitoweka. Mimi niliujua ule mchezo lakini nilijiweka pembeni kwa sababu ningejionesha najua chochote au namtambua yule Mtanga ningeshikiliwa. Tena pengine na mimi ningekuwa nimeshanyongwa siku nyingi zilizopita kwa sababu hiyo ni kesi ya mwaka 2008.
“Watanzania wajue kwamba China hakuna mchezo, hawana muda wa kufuatilia ushahidi, ukikutwa na unga, ikithibitika hivyo, kwao huo ni ushahidi tosha kwamba wewe ndiye mmiliki na unanyongwa,” alisema Rau.
PEMBE TATU HATARI
Uchunguzi wa gazeti hili kwa kufanyia kazi matukio ya Watanzania kukamatwa na madawa ya kulevya, umebaini kuwa pembe tatu hatari imetengenezwa na wauza unga katika nchi za Tanzania, Afrika Kusini na China.
Imebainika kwamba wafanyabiashara wa madawa ya kulevya, wamekuwa wakisafirisha idadi kubwa ya madawa hayo kwenda Afrika Kusini ambako husafirishwa kwa mafungu kwenda China.
Ripoti za hivi karibuni, zinaongeza nguvu katika madai kwamba Tanzania na Afrika Kusini, kuna udhaifu mkubwa wa udhibiti wa madawa ya kulevya ndiyo maana wafanyabiashara huingiza na kusafirisha mizigo mikubwa kwa urahisi.
Kutokana na hali hiyo, wafanyabiashara hao husafirisha madawa ya kulevya yenye uzani mkubwa tena kupitia katika viwanja vya ndege kisha kuziweka katika mafungu madogomadogo kwenda China na kwingineko ambako mahitaji ni makubwa na bei ni nzuri.
Uchunguzi umebaini kuwa sheria kali za China za kudhibiti madawa ya kulevya, zinasababisha uhaba mkubwa wa mihadarati ndani ya nchi hiyo, kwa hiyo anayefanikiwa kupitisha, huuza kwa bei kubwa sana.
WATUMWA WENGI NI WANAWAKE
Mwanamke, Janice Bronwyn Linden, 38, raia wa Afrika Kusini, alinyongwa China mwaka 2011, baada ya kukutwa na hatia ya kusafirisha madawa ya kulevya aina ya methamphetamine yenye uzito wa kilogramu tatu.
Nobanda Nolubabalo, 23, raia wa Afrika Kusini, alikamatwa Uwanja wa Ndege wa Suvarnabhumi, Bangkok, Thailand, akiwa ameficha cocaine zenye uzani wa kg 1.5.
Watanzania, Agnes Gerald na Melisa Edward, hivi karibuni walikamatwa Afrika Kusini, wakiwa na mzigo wa madawa ya kulevya aina ya methamphetamine, yenye thamani ya shilingi bilioni 6.8.
Mtanzania mwingine, Sharifa Mahmoud, yupo nchini Misri akisubiri adhabu ya kunyogwa, baada ya kukutwa na hatia ya kuingiza nchini humo, madawa ya kulevya aina ya heroine.
Saada Ally Kilongo, ni mwanamke mwingine wa Kitanzania ambaye hivi karibuni alikamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam, akiwa na madawa ya kulevya aina ya methamphetamine yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 170.
Zahra Thomas, kutoka Visiwa vya Sao Tome, alikamatwa mwaka jana, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hong Kong, akiwa na mzigo wa heroine wenye uzito wa kilogramu 12.
Mnigeria, Helen Okechukwu, alinaswa Falme za Kiarabu akiwa na madawa ya kulevya aina ya cocaine, uzani wa kg 20.
Mifano hiyo, inatosha kuonesha jinsi wanawake wanavyotumiwa na wauza unga kusafirisha mizigo yao kwa imani kwamba mwanamke ni rahisi kupita sehemu za ukaguzi bila kushtukiwa, vilevile kukwepa dhuluma.
MSEMAJI WA POLISI
Msemaji wa polisi nchini, Advera Senso, aliliambia gazeti hili wiki iliyopita kuwa Watanzania wengi wananyongwa China kwa sababu ya hatia ya kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya.
“Majina ya wahusika kwangu hayapo. Ila nafahamu kuwa wengi wananyongwa,” alisema Senso.
NI SIRI KUBWA
Habari zinasema kuwa mara nyingi utekelezaji wa adhabu ya kifo China ni siri lakini ubalozi wa Tanzania hujulishwa.
“Ila mara nyingi wauza madawa ya kulevya husababisha mkanganyiko wa uraia kutokana na kuwa na hati hata tatu, hii husababisha ubalozi wa Tanzania China ubaki na siri ya mtu aliyenyongwa bila kujulishwa ndugu zake,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
“Ikitokea ndugu wanaulizia hapo hupewa taarifa kamili kuhusu taarifa za ndugu yao kama ameshanyongwa au bado anatumikia kifungo.”
Chanzo chetu kilibainisha kuwa mbali na kunyongwa, vilevile hutokea vifo vya kimafia, kwani wauza unga huuana wao kwa wao ili kudhulumiana.
“Ikitokea mtu ameuawa, taarifa zikifika ubalozini, zinafuatiliwa lakini kama hazieleweki hubaki siri,” kilisema chanzo.
STORI YA MKUMBUKWA
Aprili mwaka jana, kijana wa Kitanzania, Mkumbukwa John Shayo, aliuawa China na maiti yake ilikaa mochwari mwaka mzima, kabla ya kuletwa nchini mwaka huu na kuzikwa mkoani Mwanza.
Mkumbukwa, anasadikiwa kuuawa na mtandao wa wauza madawa ya kulevya, ingawa haijulikani sababu yake ni nini.
TUNACHUNGUZA
Gazeti hili linaahidi kupita kila panapotakiwa ili kukamilisha orodha kamili ya Watanzania walionyongwa China kisha ripoti hiyo, tutaichapisha katika matoleo yajayo.
CHINA YAONGOZA KWA KUNYONGA
Chati iliyopo ukurasa wa kwanza ni takwimu za Shirika la Kimataifa la Haki za Binadamu, Amnesty International mwaka jana ambayo inaonesha kwamba China ndiyo kinara wa kunyonga watu duniani ambapo inanyonga maelfu kila mwaka kwa makosa mbalimbali ikiwemo kusafirisha madawa ya kulevya, ikifuatiwa na Pakistan na Falme za Kiarabu.
GPL
WATANZANIA ambao idadi yao inaweza kupita mamia, wameshanyongwa nchini China kutokana na kupatikana na hatia ya kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya.
Ripoti maalum ya madawa ya kulevya, iliyofanyiwa kazi na gazeti hili kwa kukusanya taarifa ndani ya nchi, Afrika Kusini na China kwenyewe, inaweka hadharani siri ya mamia ya Watanzania kunyongwa.
Katika ripoti hiyo, inaonesha kwamba mataifa ya Afrika Kusini na Uganda, yapo mstari wa mbele kuripoti taarifa za raia wao kunyongwa China lakini Tanzania imekuwa ikisuasua.
“Huu ukimya wa serikali yetu, unafanya wengi kukosa taarifa sahihi, matokeo yake wanajiingiza kwenye biashara hiyo haramu ambayo mtu akikamatwa tu China na akikutwa na hatia lazima anyongwe,” alisema Joel Mabruki, mfanyabiashara wa nguo na simu kati ya Tanzania na China.
Mabruki aliongeza: “Kama serikali yetu ingekuwa na utaratibu wa kutangaza kila Mtanzania anayenyongwa China, pengine vijana wengine wangeogopa na baadhi yao wangeacha kabisa. Hivi sasa idadi inaongezeka kwa sababu hawaambiwi ukweli.”
KITENGO CHA MADAWA YA KULEVYA KINAJUA
Kwa mujibu wa Mkuu wa Jeshi la Polisi, Kitengo cha Kuzuia na Kudhibiti Madawa ya Kulevya, Godfrey Nzowa, ofisi yake inazo taarifa kuhusu Watanzania kunyongwa China lakini akatupa mpira kwa Mkurugenzi wa Kuzuia na Kudhibiti Madawa ya Kulevya, Christopher Shekiondo.
“Kuhusu idadi na majina, hilo suala aulizwe mkurugenzi. Ila ukweli ni kwamba Watanzania wengi wanakamatwa China na wananyongwa,” alisema Nzowa.
MAAFA PAKISTAN
Kwa upande mwingine, Nzowa alisema kuwa watu wanaizungumzia sana China lakini ukweli ni kwamba nchi nyingine ambayo inanyonga Watanzania wengi ni Pakistan.
Nzowa alisema kuwa pengine taarifa za Pakistan hazipatikani sana kutokana na mwingiliano wa Tanzania na nchi hiyo, tofauti na China ambayo Watanzania wanakwenda na kurudi kila siku iendayo kwa Mungu.
“Tunaposema madawa ya kulevya ni janga kubwa inafaa ieleweke hivyo. Watanzania wanaonyongwa China na Pakistan ni wengi sana. Tuwe makini juu ya hili na tuzingatie kwelikweli,” alisema Nzowa.
TAARIFA ZA MITANDAO YA KIJAMII
Tofauti na mataifa mengine ambayo ripoti za raia wao kukamatwa na kunyongwa China hutolewa rasmi na balozi zao, hapa Tanzania, habari huenezwa na mitandao ya kijamii.
Mfano; mitandao ya kijamii ndiyo pekee iliyoripoti kuhusu kunyongwa kwa mrembo mwanamitindo (jina tunalo) aliyeshiriki video ya wimbo Twende Zetu wa mwanamuziki Saidi Juma ‘Chegge’, aliyewashirikisha Amani James Temba ‘Mheshimiwa Temba’, Feruzi Mrisho Rehani ‘Ferouz’ na Yessaya Ambilikile ‘YP’.
Vilevile, alipokamatwa aliyewahi kushika nyadhifa za makamu mwenyekiti na katibu msaidizi kwenye Klabu ya Simba (jina tunalo), mitandao ya kijamii iliandika bila serikali kutoa tamko rasmi.
Hata hivyo, kutokana na kukosekana na taarifa rasmi kutoka serikalini, mitandao ya kijamii ilitoa habari zenye kushitua, nyingine ikidai mtu huyo aliyewahi kuwa kiongozi wa Simba alifungwa miaka 70 jela, nyingine ikieleza kwamba tayari alishanyongwa.
MWAKALEBELA ATOA USHUHUDA WAKE
Katibu Mkuu Mstaafu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Frederick Mwakalebela, alipozungumza na gazeti hili, alisema kuwa kati ya mwishoni mwa mwaka 2009 na mwanzoni mwa 2010, alikwenda China katika safari ya kikazi.
“Nikiwa kule, niliambiwa taarifa za Watanzania wengi ambao walinyongwa baada ya kukutwa na hatia ya kujishughulisha na biashara ya madawa ya kulevya,” alisema Mwakalebela.
Alipoulizwa kuhusu kiongozi huyo wa Simba, Mwakalebela alijibu: “Nikiwa China niliambiwa amenyongwa. Niliporudi hapa nchini ndiyo nikasikia amefungwa miaka 70.”
Mwakalebela aliongeza: “Ukweli ni kwamba kwa taarifa nilizopata nikiwa China, Watanzania wengi sana wananyongwa kwa sababu ya madawa ya kulevya. Naweza kusema ni mamia. Ikiwa kwa muda mfupi niliokuwepo pale nimeambiwa karibu watu 10, je mwaka mzima inakuwaje?”
WENGINE WANAPONZWA NA WANIGERIA
Mfanyabiashara Mtanzania, Hashim Rau, ambaye hufanya biashara zake kati ya Tanzania, Afrika Kusini na China, alisema kuwa kuna Watanzania walinyongwa baada ya kuponzwa na Wanigeria.
Rau alisema, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa O. R. Tambo, uliopo nje kidogo ya Jiji la Johannesburg, umewasababisha matatizo Watanzania wengi kutokana na tabia yao ya ukarimu.
Alisema: “Mtanzania anaweza kutoka na biashara yake kuja kuuza Afrika Kusini, baada ya hapo anapanda ndege ya moja kwa moja kwenda China. Akiwa uwanja wa ndege anakutana na Mnigeria muuza madawa ya kulevya.
“Mtanzania anakuwa hana mizigo mingi, kwa hiyo yule Mnigeria anamwomba Mtanzania amsaidie kupitisha begi lake moja kwenye mzani, akidai kuwa yeye mizigo yake ni mingi, anaogopa atatozwa fedha nyingi.
“Kumbe lile begi linakuwa na unga. Sasa Mtanzania kwa kutojua, atakubali, baada ya hapo lile begi litaandikwa jina la Mtanzania. Mbele ya safari kama litavuka salama, Mnigeria atamshukuru Mtanzania na kuchukua begi lake lakini likikamatwa, Mnigeria atakimbia, Mtanzania atabaki na mashtaka ambayo mwisho wake ni kunyogwa China.”
Akisimulia ushuhuda wake, Rau alisema kuwa aliwahi kuombwa msaada wa aina hiyo na Mnigeria mmoja lakini alipotaka kukagua begi lina nini ndani alikataa.
“Alipokataa nikague ndani ya begi kuna nini nami nikamkatalia kumsaidia kwa sababu naujua mchezo wao. Sasa pale uwanjani alikuwepo Mtanzania mwingine mwenye asili ya Tanga (jina tunalo), alipoombwa na yule Mnigeria alikubali.
“Nilijitahidi kumwonesha ishara hakunielewa, mwisho nikamwambia asikubali lakini hakunielewa. Tulipofika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Guangzhou Baiyun, China, yule Mtanga alikamatwa baada ya lile begi kukutwa na madawa ya kulevya mchanganyiko wa heroine, cocaine na methamphetamine.
“Kama kawaida, yule Mnigeria alitoweka. Mimi niliujua ule mchezo lakini nilijiweka pembeni kwa sababu ningejionesha najua chochote au namtambua yule Mtanga ningeshikiliwa. Tena pengine na mimi ningekuwa nimeshanyongwa siku nyingi zilizopita kwa sababu hiyo ni kesi ya mwaka 2008.
“Watanzania wajue kwamba China hakuna mchezo, hawana muda wa kufuatilia ushahidi, ukikutwa na unga, ikithibitika hivyo, kwao huo ni ushahidi tosha kwamba wewe ndiye mmiliki na unanyongwa,” alisema Rau.
PEMBE TATU HATARI
Uchunguzi wa gazeti hili kwa kufanyia kazi matukio ya Watanzania kukamatwa na madawa ya kulevya, umebaini kuwa pembe tatu hatari imetengenezwa na wauza unga katika nchi za Tanzania, Afrika Kusini na China.
Imebainika kwamba wafanyabiashara wa madawa ya kulevya, wamekuwa wakisafirisha idadi kubwa ya madawa hayo kwenda Afrika Kusini ambako husafirishwa kwa mafungu kwenda China.
Ripoti za hivi karibuni, zinaongeza nguvu katika madai kwamba Tanzania na Afrika Kusini, kuna udhaifu mkubwa wa udhibiti wa madawa ya kulevya ndiyo maana wafanyabiashara huingiza na kusafirisha mizigo mikubwa kwa urahisi.
Kutokana na hali hiyo, wafanyabiashara hao husafirisha madawa ya kulevya yenye uzani mkubwa tena kupitia katika viwanja vya ndege kisha kuziweka katika mafungu madogomadogo kwenda China na kwingineko ambako mahitaji ni makubwa na bei ni nzuri.
Uchunguzi umebaini kuwa sheria kali za China za kudhibiti madawa ya kulevya, zinasababisha uhaba mkubwa wa mihadarati ndani ya nchi hiyo, kwa hiyo anayefanikiwa kupitisha, huuza kwa bei kubwa sana.
WATUMWA WENGI NI WANAWAKE
Mwanamke, Janice Bronwyn Linden, 38, raia wa Afrika Kusini, alinyongwa China mwaka 2011, baada ya kukutwa na hatia ya kusafirisha madawa ya kulevya aina ya methamphetamine yenye uzito wa kilogramu tatu.
Nobanda Nolubabalo, 23, raia wa Afrika Kusini, alikamatwa Uwanja wa Ndege wa Suvarnabhumi, Bangkok, Thailand, akiwa ameficha cocaine zenye uzani wa kg 1.5.
Watanzania, Agnes Gerald na Melisa Edward, hivi karibuni walikamatwa Afrika Kusini, wakiwa na mzigo wa madawa ya kulevya aina ya methamphetamine, yenye thamani ya shilingi bilioni 6.8.
Mtanzania mwingine, Sharifa Mahmoud, yupo nchini Misri akisubiri adhabu ya kunyogwa, baada ya kukutwa na hatia ya kuingiza nchini humo, madawa ya kulevya aina ya heroine.
Saada Ally Kilongo, ni mwanamke mwingine wa Kitanzania ambaye hivi karibuni alikamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam, akiwa na madawa ya kulevya aina ya methamphetamine yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 170.
Zahra Thomas, kutoka Visiwa vya Sao Tome, alikamatwa mwaka jana, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hong Kong, akiwa na mzigo wa heroine wenye uzito wa kilogramu 12.
Mnigeria, Helen Okechukwu, alinaswa Falme za Kiarabu akiwa na madawa ya kulevya aina ya cocaine, uzani wa kg 20.
Mifano hiyo, inatosha kuonesha jinsi wanawake wanavyotumiwa na wauza unga kusafirisha mizigo yao kwa imani kwamba mwanamke ni rahisi kupita sehemu za ukaguzi bila kushtukiwa, vilevile kukwepa dhuluma.
MSEMAJI WA POLISI
Msemaji wa polisi nchini, Advera Senso, aliliambia gazeti hili wiki iliyopita kuwa Watanzania wengi wananyongwa China kwa sababu ya hatia ya kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya.
“Majina ya wahusika kwangu hayapo. Ila nafahamu kuwa wengi wananyongwa,” alisema Senso.
NI SIRI KUBWA
Habari zinasema kuwa mara nyingi utekelezaji wa adhabu ya kifo China ni siri lakini ubalozi wa Tanzania hujulishwa.
“Ila mara nyingi wauza madawa ya kulevya husababisha mkanganyiko wa uraia kutokana na kuwa na hati hata tatu, hii husababisha ubalozi wa Tanzania China ubaki na siri ya mtu aliyenyongwa bila kujulishwa ndugu zake,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
“Ikitokea ndugu wanaulizia hapo hupewa taarifa kamili kuhusu taarifa za ndugu yao kama ameshanyongwa au bado anatumikia kifungo.”
Chanzo chetu kilibainisha kuwa mbali na kunyongwa, vilevile hutokea vifo vya kimafia, kwani wauza unga huuana wao kwa wao ili kudhulumiana.
“Ikitokea mtu ameuawa, taarifa zikifika ubalozini, zinafuatiliwa lakini kama hazieleweki hubaki siri,” kilisema chanzo.
STORI YA MKUMBUKWA
Aprili mwaka jana, kijana wa Kitanzania, Mkumbukwa John Shayo, aliuawa China na maiti yake ilikaa mochwari mwaka mzima, kabla ya kuletwa nchini mwaka huu na kuzikwa mkoani Mwanza.
Mkumbukwa, anasadikiwa kuuawa na mtandao wa wauza madawa ya kulevya, ingawa haijulikani sababu yake ni nini.
TUNACHUNGUZA
Gazeti hili linaahidi kupita kila panapotakiwa ili kukamilisha orodha kamili ya Watanzania walionyongwa China kisha ripoti hiyo, tutaichapisha katika matoleo yajayo.
CHINA YAONGOZA KWA KUNYONGA
Chati iliyopo ukurasa wa kwanza ni takwimu za Shirika la Kimataifa la Haki za Binadamu, Amnesty International mwaka jana ambayo inaonesha kwamba China ndiyo kinara wa kunyonga watu duniani ambapo inanyonga maelfu kila mwaka kwa makosa mbalimbali ikiwemo kusafirisha madawa ya kulevya, ikifuatiwa na Pakistan na Falme za Kiarabu.
GPL
MUGABE AMEWATAKA MSHOGA NA WASAGAJI NCHINI MWAKE WAZALIANE LASIVYO ATAWAFUNGA JELA

Mugabe ametoa kali hiyo Ijumaa wakati akizindua kampeni za chama chake cha kwa ajili ya uchaguzi utakaofanyika mwezi huu.
Isome taarifa nzima ya rais huyo mwenye umri mkubwa aliye madarakani duniani na ambaye wazungu wanamgwaya kwa misimamo yake isiyoyumba.
President Robert Mugabe on Friday threatened to jail gay and lesbian couples who fail to conceive any offspring as he launched his party’s campaign for this month’s general election.
The Zanu PF leader also attacked bitter rival and coalition partner Morgan Tsvangirai for his bed-hopping habits saying it was inconceivable that such a character could want to lead the country.Mugabe, a rabid critic of homosexuality returned to the theme as he addressed thousands of supporters in Harare’s Highfield township.He said he was shocked to learn that US President Barack Obama had called on African countries to embrace the practice.
The Zanu PF leader said in Shona: “Ndakanzva Obama achiti ah, daimuno muAfrica mabvuma kuti murume nemurume vachate, mukadzi nemukadzi vachate, ndikati nhai nhai, taitoti baba vako zvaari mutema, iwe uneruva neruzivo netsika dzevatema waakunotora zvevarungu futi!
Apparently joking Mugabe added: “So how would they (gay couples) have children?
Subscribe to:
Posts (Atom)