Pages

Waganga Wajitokeza Kupambana na Jini Mahaba Linalo Mtesa Lady J'dee

Lady J'dee
WAGANGA wanaodai kuwa ni wataalam na wana uzoefu wa kupambana na jini mahaba linalomsumbua Mwanamuziki Judith Wambura ‘Lady Jaydee’, wamejitokeza huku kila mmoja akiomba apewe nafasi ya kumtibu bure.

Mmoja wa wataalam hao aliyejitambulisha kwa jina la Jumaa wa Magomeni, Dar alisema: “Nimesoma habari kuhusu Jide, mimi naweza kumtibu tena bure, mpe namba yangu na mwambie anipigie.”

Mwingine ambaye hakupenda jina lake liandikwe alisema: “Nimesikitika sana kusoma hii habari ya huyu msanii Lady Jaydee, kwa kifupi naweza kumtibia free of charge.”

Kufuatia maombi ya wataalam hao, mwandishi wetu alijitahidi kumtafuta Jide bila mafanikio lakini juzikati kupitia kipindi chake cha Diary ya Lady Jaydee alionekana akipewa matibabu na ustaadhi mmoja, mazingira yanayoashiria kuwa huenda mambo yametulia.
CREDIT : GPL

Askari Aliyemwua kwa Risasi Mwalimu NMB Afukuzwa Kazi, Njombe

JESHI la Polisi mkoani Njombe, limemfukuza kazi askari wake PC Gelvas Joseph, mwenye namba 9790, kwa kosa la kufanya mauaji ya mwalimu wa Shule ya Sekondari Kitulo, wilayani Makete.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, Focus Malengo, alisema askari huyo alifanya kosa hilo Februari 27 mwaka huu kwa kumpiga risasi kifuani mwalimu Castory Sote (31), na kusababisha kifo chake papo hapo.

Alisema askari huyo amefukuzwa kazi baada ya uchunguzi wa tukio hilo kukamilika na kubaini alikiuka kanuni za utumishi ambapo hivi sasa anakabiliwa na mashtaka.

Aliongeza kuwa, kosa hilo alilifanya akiwa lindoni kwenye Benki ya NMB, tawi la Makete, ambapo marehemu alikuwa akichukua fedha katika mashine za benki hiyo.

Ilidaiwa kuwa, siku ya tukio hilo kulitokea malumbano kati ya mwalimu huyo na askari ambaye alimtuhumu marehemu kuendesha pikipiki bila kuvaa kofia ngumu (helmet) kichwani. Hali hiyo ilizua mzozo kati yao baada ya marehemu kudai kuwa, polisi huyo si askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani.
Imeandikwa na Mercy James, Njombe (via Majira)

CAR FOR SALE

Sale,Used Car
DETAILS
Year: 2003 (Imported this January, 2013), Mileage: Almost 52,000 km, Displacement (CC) 1,790 with VVT-i Engine, Body Type: Station Wagon, Color: Metallic Grey, Fuel: Gasoil/ Petrol, Gear box type: Automatic, Sitting capacity: 7, Motor vehicle license and Insurance validity: Expires January 2014, Other details: All duties paid, Good tires, New Break Pads, No mechanical problems, Serviced upon arrival, In very good shape and condition: Reason for Sale: Bought for a wife who wants 4x4. Needs 15 milion. (Tshilngs)
Sale,Used Car
Click read more for more pictures..

Blog Zote za Bongo, kwa Mablogger,Wasomaji na Wadau!!



Kama Unasumbuka kukumbuka majina ya blog uzipendazo hii itaksaidia!! 
Blog zote ndani ya Blog 1.
 Inapatikana Hapa >> http://bongoblogs.blogspot.com
Mwambie Rafiki Amwambie Rafiki..!!  

Mafunzo Muhimu Namna ya Kuswali (Video)

Mjadala Ughaibuni Kuhusu Kushuka kwa Elimu Tanzania, Sehemu ya Tatu


Video ya Kukamatwa kwa Lwakatare CHADEMA Yafafanua, CCM na Usalama wa Taifa Wahusika Wakuu

'' Tunamjua anayeendesha mbinu za kutuchafua-Dk Slaa.
polisi wapekua nyumba yake kwa mara ya pili, aendelea kushikiliwa na jeshi hilo.

Polisi wambana Lwakatare. -Dk. Slaa: Video ya Lwakatare ni Feki


Lwakatare alikamatwa juzi makao makuu ya chama hicho na kupelekwa katika Makao Makuu ya Polisi kwa mahojiano.
Polisi wamezidi kumbana Mkuu wa Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare baada ya kupekua nyumbani kwake kwa siku ya pili mfululizo.

Lwakatare, ambaye ni mbunge wa zamani wa Jimbo la Bukoba Mjini kupitia CUF, alikamatwa juzi mchana kwa kutuhumiwa kwa kufanya uchochezi wa uvunjifu wa amani baada ya kunaswa kwenye picha ya video iliyorushwa kwenye mitandao ya kijamii

Upekuzi wa pili
Nyaronyo Kicheere, ambaye ni Mwanasheria wa Lwakatare, aliliambia gazeti hili jana kuwa mteja wake, ambaye anashikiliwa na polisi hao, alipelekwa nyumbani kwake Kimara-King’ong’o jijini Dar es Salaam kwa ajili ya upekuzi huo.

Ilikuwa mara ya pili kwa Lwakatare kupekuliwa kwani mara ya kwanza ilikuwa juzi jioni baada ya kuhojiwa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi. Lwakatare, ambaye alitolewa Kituo cha Kati cha Polisi, alipelekwa jana kwa msafara wa magari mawili ya polisi chini ya ulinzi mkali.

Nyaronyo alisema kuwa msafara huo uliondoka saa 10.00 jioni kwa ajili ya safari hiyo ya Kimara wakitokea katikati ya Jiji la Dar es Salaam kilipo Kituo cha Kati cha Polisi. Alisema kuwa uamuzi huo ulifikiwa baada ya...

Rais Kikwete Amezindua Jengo la Kitivo cha Sayansi Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro.

 Morogoro
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua pazia kuzindua rasmi jengo la Kitivo cha Sayansi la Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro leo Machi 14, 2013 mjini Morogoro. Kushoto kwake ni Mkuu wa Chuo hicho Mama Mwantumu Malale.
Jengo la Kitivo cha Sayansi Chuo Kikuu cha Kiislamu
 Juma Mikidadi Mtupa
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo juu ya ujenzi wa jengo la kitivo cha Teknohama toka kwa Bw. Hamza Mustafa Njozi kabla ya kuzindua rasmi jengo la Kitivo cha Sayansi la Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro leo Machi 14, 2013 mjini Morogoro. Kushoto kwake ni Mkuu wa..

Balozi Apokonywa Ubalozi Baada ya Kutembea Uchi

Afrika Kusini nchini China,
Lassy Chiwayo ambae ni balozi wa Afrika Kusini nchini China, amerudishwa nyumbani baada ya mkataba wake kukatishwa kutokana na kukumbwa na kile kinachodaiwa kuwa matatizo ya kiafya.
Gazeti la Daily Teleghraph limeripoti kwamba moja kati ya sababu kubwa ni tatizo kwenye akili yake ambapo inadaiwa balozi huyo ilifikia mpaka kutembea mtaani bila nguo.

Magazeti mbalimbali yameripoti kwamba balozi huyo alikua na mtindo wa kupotea nyumbani huko China alikokua anaishi, alikua anapotea kwa siku kadhaa alafu baadae anakuja kukutwa akiwa mtupu bila nguo.

Lassy mwenye umri wa miaka 44 akiwa ni mmoja wa watu wa karibu ambao waliwahi kufungwa gereza moja na rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela, amekanusha taarifa zake za kuwa na matatizo ya akili pamoja na kutembea uchi, akisema hayo yote ni mambo mapya kuyasikia.

Imeripotiwa kwamba Lassy ambae ni baba wa watoto watatu amekumbwa na mfululizo wa matukio hivi karibuni ambapo la mwisho linalokumbukwa ni moto kulipuka nyumbani kwake na kuteketeza mali kama gari la kifahari la Porsche, quad bike na mali nyingine