KAMPUNI ya Lakeland Africa kesho itaanza safari ya ‘Mtanzania tembelea Tanzania’ kwa siku 14 kwa lengo la kukuza utalii wa ndani na kujenga utamaduni wa Watanzania kutembelea vivutio vya utalii nchini.
Safari hiyo itakayoanzia Mlimani City Dar es Salaam kesho inatoa fursa kwa watanzania kutembelea vivutio mbalimbali ikiwemo Hifadhi ya Saadan, Pangani, Lushoto, Tarangile, Olduvai Gorge, Lake Manyara, Ngorongoro na Serengeti na pia watapata nafasi ya kutembelea kijiji cha Butiama alikozaliwa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Nyerere na kuzuru katika kaburi lake.
“Lakeland Africa sasa itaendesha safari za namna hii kuhimiza watu kutembelea vivutio vya utalii nchini kwa kauli mbiu ya ‘kuwa mtalii ndani ya nchi yako”
Kuanzia mwezi januari mwakani Lakeland Africa itaendesha safari za..