
MADEREVA wa maroli ya mizigo na kwenda mikoani na nchi jirani sasa watakuwa hawana shida ya kupata maarifa, elimu na hudumu mbali mbali za Virusi vya UKIMWI—ikiwa ni pamoja na kupima kwa hiari ili kujua hali zao—kutokana na ufunguzi wa kituo cha maarifa ya udhibiti wa ugonjwa huo katika eneo la Mdaula, nje kidogo ya mji wa Chalinze, Mkoa wa Pwani.
Uzinduzi huo uliongozwa na Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) Dk. Fatma Mrisho na kushuhudiwa na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Bw. Ahmed Kipozi pamoja na viongozi mbalimbali wa wilaya na vijiji vya Mdaula, Matuli na Mbena.
Huduma zitakazotolewa na kituo hicho ambacho..