Producer mkongwe na mmiliki wa studio ya Mj Records Joakim Kimaryo aka Master J, amesema studio za muziki zimekuwa nyingi mno kiasi cha kufanya biashara hiyo kuwa ngumu.
Alisema ongezeko la studio za kurekodi muziki nchini ambazo hazina bei moja inayofanana limefanya biashara ya muziki kuzorota kila kukicha.
Akiongea na kipindi cha Bongo Fleva cha Clouds FM jana, Master J ambaye pia ni jaji wa Bongo Star Search aliongeza kuwa tatizo kubwa linatokana na kutokuwepo kwa ushirikiano kati ya wamiliki/maproducer wa studio hizo ili kupanga bei moja ya kurekodia.
“Kuna studio zinarekodi wimbo mpaka kwa elfu..