
Siku moja baada ya Dogo Janja kudaiwa kufukuzwa Tip Top Connection, ukweli halisi kuhusiana na uamuzi huo umewekwa wazi na yeye mwenyewe.Sababu zilizotajwa na Tip Top Connection ni kwamba Dogo Janja alilewa sifa na kuwa mtoro shuleni.
Kwa mujibu wa interview (ya pili
kufanyiwa baada ya kipindi cha Amplifaya cha jana) tuliyofanya naye kwa
simu saa moja asubuhi leo (June 14) akiwa stand kurejea nyumbani, uonevu
na dhuluma ndivyo vilivyomchosha kuishi Dar es Salaam.

Anasema tangu aje Dar es Salaam
hajawahi kusaidiwa chochote na Madee zaidi ya mambo ya muziki pekee huku
kula, malazi na ada ya shule vikifanywa na rafiki yake Madee aitwaye
Abdallah Doka ambaye (Dogo Janja) alikuwa akiishi kwake.
Anasema kutokana na ngoma zake
kujipatia umaarufu alikuwa akipata show nyingi nchini na zote alikuwa
halipwi chini ya milioni moja.Kilichokuwa kinamsikitisha anasema ni
kulipwa hela kidogo isiyozidi laki mbili na hivyo kumfanya aishi kwa
tabu licha ya kuingiza hela nyingi za show.
“Nilikuwa navumilia tu bro kwasababu kila nilipolalamika kuhusu mambo ya hela Madee alikuwa mkali sana,” ameongea uchungu.
Dogo anasema ilikuwa inafikia
wakati..